Mukama ameishiwa baada ya kushindwa hata kupambana na kivuli cha Yusuf Makamba. Inashangaza ule ujasiri aliokuwa nao wakati akiwa Mkuu wa jiji umeyeyukia wapi.
CCM iko kwenye hatua za mwisho kuelekea kufa, ni ngumu sana kuinusuru. Nimemsifu Lugola kwa kuliweka hilo hadharani ili wananchi wajue kwamba CCM inaongozwa na watu wa namna gani.
Mukama alipopewa kuongoza Kamati ya kuchunguza CCM kufanya vibaya alimkandia sana Makamba. JK akasema ngoja nimpe yeye mwenyewe ili aje anyooshe mambo. Alipokabidhiwa mikoba akakuta ni ya moto. Kauli alizotoa Dodoma baada ya NEC zilianza kubadilika taratibu na mpaka sasa hata hajui Operation Vua Gamba ilikuwa inahusu nini.
Sasa anavyomtishia Lugola ina maana anahalalisha ufisadi ambao amekuwa akituaminisha kila siku kwamba CCM inapiga vita ufisadi?
Kwa kadri wanavyochelewa kuchukua hatua ndio wanavyozidi kujipaka matope. Maana Wizara ya Viwanda na Biashara washapakana matope tayari na Ekelege naye kashasilibwa.
Wizara ya Uchukuzi nayo vingunge wake wote wa juu wameishapakana matope. So, kama kufanya mabadiliko, then Waziri, Naibu Waziri na Katibu Mkuu wote wanatakiwa kuondolewa. Kaazi kweli kweli! Hapo bado hawajaenda kwenye Management ya TPA na Bodi yake.