Wabunge wa CCm waliotia sahihi maisha yao hatarini.

Sitachoka

JF-Expert Member
Nov 17, 2011
3,030
1,303
BAADHI ya wabunge wa Chama cha Mapinduzi, walioshiriki kusaini hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu kwa nia ya kushinikiza kujiuzulu kwa mawaziri wanaotuhumiwa kufuja mabilioni ya fedha, wametishiwa maisha.

Habari za kuaminika zilizothibitishwa na mmoja wa wabunge hao, zimesema kuwa wabunge wawili kati ya wanne wa chama hicho wamelazimika kuukimbia mji wa Dodoma na kujificha kwa muda kusikojulikana. Wabunge hao (majina yao tunayo) waliondoka mjini Dodoma mara baada ya kupewa taarifa na watu wao wa karibu kuwa walikuwa wakisakwa kwa vile baadhi ya wakubwa ndani ya CCM walikuwa wamechukizwa na kitendo hicho.

Akizungumza na Tanzania Daima, mmoja wa wabunge waliokimbia na kujificha, amedai kuwa alilazimika kufanya hivyo baada ya kushauriwa sana na rafiki zake, ingawa awali aligoma kuondoka akisema angekuwa tayari kukabiliana na lolote hata kufa kwa vile anaamini hajafanya kosa lolote la kuhatarisha amani ya nchi. "Ni kweli niko nje ya Dodoma, nimefanya hivi baada ya kuwepo kwa hisia hizo, maana naziita hivyo kwa sababu binafsi siogopi kutishwa," alisema mbunge huyo.

Kwa upande wake, Mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe (CCM) ambaye ni mmoja wa wabunge
wa chama hicho waliotia saini hoja hiyo, alikiri kupigiwa simu za shutuma na lawama kwa madai ya kukisaliti chama na kuunga mkono hoja ya wapinzani ya kutaka kuwawajibisha mawaziri wanaoitumikia serikali ya chama hicho. Filikunjombe alisema ingawa hajapata vitisho rasmi, lakini alijua hatua hiyo ingemgharimu. Alisema kuwa hajutii hatua hiyo kwa sababu ndiyo mahali pekee pa kusemea na kwamba kama asipoyasema yeye machungu ya Watanzania, hajui nani atayasema.

Mbunge huyo machachali na asiye na woga aliongeza kuwa ni wajibu wake kukisadia chama chake kwa moyo mnyoofu na kuwasilisha kilio cha Watanzania na cha wananchi wa Ludewa. Alizidi kumshambulia Waziri wa Kilimo na Chakula, Jumanne Maghembe, kwa kuzembea na kupeleka mbolea ya kupandia
jimboni kwake Ludewa mwezi Machi badala ya mwezi Oktoba, tena ikiwa feki. "Katika hali ya hovyo kiasi hiki, walitaka nicheke na kutetea upuuzi eti kwa sababu nalinda chama? Nimechaguliwa na watu kuwalinda na kuwaletea maendeleo sio umaskini. Kibaya wamewakopa hata mawakala. Badala ya kunisaidia na kuwawajibisha waliofanya uzembe huu eti nalaumiwa mimi," alisema.

Lugola apigiwa simu ya vitisho Katika hali isiyokuwa ya kawaida, Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola, alipigiwa simu juzi saa saba za usiku na kiongozi mmoja wa juu wa CCM akimtaka ajiandae kwa mapambano kwa kile kilichoelezwa kuwa amekisaliti chama. Akithibitisha tukio hilo, Lugola alisema kuwa kiongozi huyo mzito (jina tunalo) ambaye ni bingwa wa kufoka na kutukana vyombo vya habari vinavyomkosoa, alimwita mbunge huyo mnafiki, mzandiki na kwamba kwa hatua yake ya kusaini hoja ya kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu atambue kuwa ametangaza vita. "Ni kweli nilipigiwa simu na.. (anamtaja) na kuanza kunifokea na kunitukana. Nilishindwa kuamini kama kiongozi mzito kama yeye anaweza kuniambia maneno hayo. Nami nilimwambia kwa kuwa sina kosa na nimetumia haki yangu, afanye lolote analoweza." Mbunge huyo alisema pamoja na kuambiwa kuwa leo kigogo huyo wa CCM atafika Dodoma kumshughulikia na wale wote tuliotia saini, haogopi lolote na yuko tayari kukabiliana na
magumu kwa ajili ya maslahi ya Watanzania. "Hata wakiniua, sitaogopa naamini katika ukweli na ni kilio cha wengi. Lakini wengi wananiunga mkono, na wamenipigia simu na wanakubali kuwa wako nyuma
yangu.

Alisema maisha ya Watanzania ni mabaya, shuleni hakuna walimu wala madawati, hospitali ziko taabani kwa kukosa dawa huku madaktari wakililia maslahi, na kila wakati serikali imekuwa ikidai haina fedha kumbe, zipo na zinaliwa na wajanja. "Hakuna cha kunitisha katika hali kama hii. Wanaonitisha ndiyo wasioitakia mema CCM na Watanzania na hao lazima tuwashughulikie mchana kweupe. Na katika hili, lazima wote bila kujali wao ni nani lazima wajiuzulu bila kusubiri eti wajipime na kutafakari," alisema
Lugola.
 
Hii sio Breaking News bali ni HABARI ILIYOVUNJIKA VIPANDE VIPANDE...

We unategemea nini katika kundi la wachawi anapotokea mmoja ameokoka watamuacha, watatumia kila hila kumuangamiza ili siri zao zisivuje
 
Mungu husimamia haki kila wakati. Msiwe na mashaka coz hamna atake ishi milele
baadhi ya wabunge wa chama
cha mapinduzi, walioshiriki
kusaini hoja ya kutokuwa na
imani na waziri mkuu kwa nia ya
kushinikiza kujiuzulu kwa
mawaziri wanaotuhumiwa
kufuja mabilioni ya fedha,
wametishiwa maisha.
Habari za kuaminika
zilizothibitishwa na mmoja wa
wabunge hao, zimesema kuwa
wabunge wawili kati ya wanne
wa chama hicho wamelazimika
kuukimbia mji wa dodoma na
kujificha kwa muda
kusikojulikana.
Wabunge hao (majina yao
tunayo) waliondoka mjini
dodoma mara baada ya kupewa
taarifa na watu wao wa karibu
kuwa walikuwa wakisakwa kwa
vile baadhi ya wakubwa ndani ya
ccm walikuwa wamechukizwa na
kitendo hicho.
Akizungumza na tanzania daima,
mmoja wa wabunge waliokimbia
na kujificha, amedai kuwa
alilazimika kufanya hivyo baada
ya kushauriwa sana na rafiki
zake, ingawa awali aligoma
kuondoka akisema angekuwa
tayari kukabiliana na lolote hata
kufa kwa vile anaamini hajafanya
kosa lolote la kuhatarisha amani
ya nchi.
“ni kweli niko nje ya dodoma,
nimefanya hivi baada ya kuwepo
kwa hisia hizo, maana naziita
hivyo kwa sababu binafsi siogopi
kutishwa,” alisema mbunge
huyo.
Kwa upande wake, mbunge wa
ludewa deo filikunjombe (ccm)
ambaye ni mmoja wa wabunge
wa chama hicho waliotia saini
hoja hiyo, alikiri kupigiwa simu
za shutuma na lawama kwa
madai ya kukisaliti chama na
kuunga mkono hoja ya
wapinzani ya kutaka
kuwawajibisha mawaziri
wanaoitumikia serikali ya chama
hicho.
Filikunjombe alisema ingawa
hajapata vitisho rasmi, lakini
alijua hatua hiyo ingemgharimu.
Alisema kuwa hajutii hatua hiyo
kwa sababu ndiyo mahali pekee
pa kusemea na kwamba kama
asipoyasema yeye machungu ya
watanzania, hajui nani
atayasema.
Mbunge huyo machachali na
asiye na woga aliongeza kuwa ni
wajibu wake kukisadia chama
chake kwa moyo mnyoofu na
kuwasilisha kilio cha watanzania
na cha wananchi wa ludewa.
Alizidi kumshambulia waziri wa
kilimo na chakula, jumanne
maghembe, kwa kuzembea na
kupeleka mbolea ya kupandia
jimboni kwake ludewa mwezi
machi badala ya mwezi oktoba,
tena ikiwa feki.
“katika hali ya hovyo kiasi hiki,
walitaka nicheke na kutetea
upuuzi eti kwa sababu nalinda
chama? Nimechaguliwa na watu
kuwalinda na kuwaletea
maendeleo sio umaskini. Kibaya
wamewakopa hata mawakala.
Badala ya kunisaidia na
kuwawajibisha waliofanya
uzembe huu eti nalaumiwa
mimi,” alisema.
Lugola apigiwa simu ya vitisho
katika hali isiyokuwa ya kawaida,
mbunge wa mwibara, kangi
lugola, alipigiwa simu juzi saa
saba za usiku na kiongozi mmoja
wa juu wa ccm akimtaka
ajiandae kwa mapambano kwa
kile kilichoelezwa kuwa
amekisaliti chama.
Akithibitisha tukio hilo, lugola
alisema kuwa kiongozi huyo
mzito (jina tunalo) ambaye ni
bingwa wa kufoka na kutukana
vyombo vya habari
vinavyomkosoa, alimwita
mbunge huyo mnafiki, mzandiki
na kwamba kwa hatua yake ya
kusaini hoja ya kura ya
kutokuwa na imani na waziri
mkuu atambue kuwa
ametangaza vita.
“ni kweli nilipigiwa simu na..
(anamtaja) na kuanza kunifokea
na kunitukana. Nilishindwa
kuamini kama kiongozi mzito
kama yeye anaweza kuniambia
maneno hayo. Nami nilimwambia
kwa kuwa sina kosa na
nimetumia haki yangu, afanye
lolote analoweza.”
mbunge huyo alisema pamoja na
kuambiwa kuwa leo kigogo huyo
wa ccm atafika dodoma
kumshughulikia na wale wote
tuliotia saini, haogopi lolote na
yuko tayari kukabiliana na
magumu kwa ajili ya maslahi ya
watanzania.
“hata wakiniua, sitaogopa
naamini katika ukweli na ni kilio
cha wengi. Lakini wengi
wananiunga mkono, na
wamenipigia simu na
wanakubali kuwa wako nyuma
yangu.
Alisema maisha ya watanzania ni
mabaya, shuleni hakuna walimu
wala madawati, hospitali ziko
taabani kwa kukosa dawa huku
madaktari wakililia maslahi, na
kila wakati serikali imekuwa
ikidai haina fedha kumbe, zipo
na zinaliwa na wajanja.
“hakuna cha kunitisha katika hali
kama hii. Wanaonitisha ndiyo
wasioitakia mema ccm na
watanzania na hao lazima
tuwashughulikie mchana
kweupe. Na katika hili, lazima
wote bila kujali wao ni nani
lazima wajiuzulu bila kusubiri eti
wajipime na kutafakari,” alisema
lugola.
 
Hii sio Breaking News bali ni HABARI ILIYOVUNJIKA VIPANDE VIPANDE...

We unategemea nini katika kundi la wachawi anapotokea mmoja ameokoka watamuacha, watatumia kila hila kumuangamiza ili siri zao zisivuje

imeandikwa uckizoeze kinywa chako kutamka maneno ya ovyo ndani yake kuna matusi na maudhi
 
Katika lichama la majambazi kama ccm ulitegemea nini kitokee? Wauaji wakubwa hawa!
 
Back
Top Bottom