Ni njia sahihi duniani kote ya kuendesha nchi..ndio ukienda marekani wana CIA, ukienda urusi kuna KGB..sio kila mtuhumiwa anafikishwa mahakamani..huo ni mfumo rasmi kabisa wa dunia..mtapiga sana kelele ila hakuna namna..ukishajitengenezea mazingira ya kutekwa we subiri kutekwa tu.Kwa hiyo UTEKAJI ndio mfumo sahihi wa CCM kushughulika na wakosaji badala ya kuwashtaki mahakamani?
Huyo msomali aende kwao akasaidie peace keeping..siasa za Tanzania za kulazimisha kutekwa hataziweza.Yaani unaleta habari za Ulimboka?alipojitokeza Kijo bisimba mlilalamika kuwa ametengeneza picha ya Dr kutekwa? Leo Bashe anazungumzia haya unasema ni ghost member wa ccm acha upuuzi wewe kijana
Humjui Bashe wewe, huyu mzalendo ameanza kupiga kelele siku nyingi tangu sakata la Dk Ulimboka na pia alikuwa mstari wa mbele pale Absalom Kibanda alipojeruhiwaNaamini malengo ya utekaji ni kupeleka ujumbe wa hofu zaidi ya kudhuru au kuua. Utawala huu naona unafanyia kazi dhana ya kuwa ukifanikiwa kuwajengea maadui wako hofu, tayari una nusu ya ushindi. Mfano maandamano ya UKUTA yalizimwa kwa mazoezi yaloyolenga kujenga hofu. Kauli mbalimbali za watawala mfano kuvitishia vyombo vya habari, kamata kamata ya wapinzani na kesi zisizoisha zina nia ya kujenga hofu nk.
Dalili ya mtawala aliye na hofu na asiyejiamini ni kutishia na kufanya na kuamuru matendo yanayolenga kuleta hofu kwa anaowaongoza. Mtu jasiri anatakiwa awe huru kupambana na hofu kama Tundu Lissu. Kama ni kutekwa na kukamatwa huwa namwona Tundu Lissu akikamatwa kila siku. Ila bado sijaona mwanachama wa chama cha kijani akilala sero hata lisaa limoja tu la mfano.
Huyu Bashe bado anaamini kuwa akivaa kijani basi yeye ni nusu mungu au "untouchable" hagusiki!!. Ni wakati sasa ajifunze na aachane na huo mtazamo. Anatakiwa kwanza kutambua kuwa binadamu wote ni sawa. Watanzania wote ni sawa, wana thamani iliyo sawa. Haijalishi kama anaunga mkono upinzani au ccm.
Kama ni mkweli, Hussen Bashe tungemwona anapinga matendo yote machafu ya utawala kuanzia mwanzo. Sio mpaka achukuiwe kwa mahojiano masaa machache, ndio aanze kupiga kelele kama mtoto aliyezaliwa jana.
G
Nina wasiwasi ni condom ilipasuka sio bure. mtu mwenye akili timamu na aliyezaliwa kwa 'mpango' hawezi kusema haya yako.Huyo msomali aende kwao akasaidie peace keeping..siasa za Tanzania za kulazimisha kutekwa hataziweza.
Kwa hiyo unatilia shaka uzalendo wa Katibu Mkuu wetu wa chama Kamaradi Kinana?Msomali tangu lini akawa mzalendo?
Kumbe ndo siasa zenu za kuteka watu? Haya mrudisheni na KinanaHuyo msomali aende kwao akasaidie peace keeping..siasa za Tanzania za kulazimisha kutekwa hataziweza.
We need people like Bashe.Bashe anawakilisha sauti ya umma.Bashe ni mzalendo na anajielewa kuzidi wabunge wengi wa CCM
Haya CCM endeleeni kuteka, kutesa, na kung'oa meno na macho. Ifikapo 2020 msisahau kutupa mrejesho mmeua wangapi.Ni njia sahihi duniani kote ya kuendesha nchi..ndio ukienda marekani wana CIA, ukienda urusi kuna KGB..sio kila mtuhumiwa anafikishwa mahakamani..huo ni mfumo rasmi kabisa wa dunia..mtapiga sana kelele ila hakuna namna..ukishajitengenezea mazingira ya kutekwa we subiri kutekwa tu.
Hata we ukitaka kutekwa utatekwa tu..jitokeze kisha tengeneza mazingira..sasa hivi tupo kwenye Ujenzi wa nchi wa kiwango cha kimataifa..leo tunazindua reli ya umeme kitu ambacho hadi babu yako anakufa hakuwai kukiota..kisha mnataka kututoa kwenye reli kwa upuuzi wenu..mtanyooka tu taratibu.Kumbe ndo siasa zenu za kuteka watu? Haya mrudisheni na Kinana
Wenye akiki nyingi pekee ndio watanielewa jibu nililokujibu sio wewe kichwa box,hata namna ya ujibuji wako yaonyesha huna cheti...Akili fupi sana ...hizo ndoto mnazoota zitawapa uchizi.
Toka lini wehu wakashika dola???
Utawala wa jpm ni tofauti na tawala zilizopita!Mtanyooka tu
Nani anakutoa kwenye reli wewe mbigwa? Yaani una kila kitu bado unalalamika kama mke wa kambo? Ebhooo jitahidi kutatua changamoto na sio kuzikimbia na kuteka watu najua unafanya hayo ya kifala kwa upuuzi huo ,babu yangu haote nini sasa yaani nilipe kodi kukuzidi wewe alafu uje na lugha za kipuuziHata we ukitaka kutekwa utatekwa tu..jitokeze kisha tengeneza mazingira..sasa hivi tupo kwenye Ujenzi wa nchi wa kiwango cha kimataifa..leo tunazindua reli ya umeme kitu ambacho hadi babu yako anakufa hakuwai kukiota..kisha mnataka kututoa kwenye reli kwa upuuzi wenu..mtanyooka tu taratibu.
Ndiyo maana namzungumzia huyu Njonjo wa Tz ninapimkumbuka Alphonse Mawazo , Ben Saanane , Marehemu wa sandarus za mto Ruvu etc. Njonjo walitumika kuratibu huo utekaji na mauaji hayo.Wakumbushe wako wapi wanasiasa wazuri wa Kenya kama :
1. Tom Mboya alipigwa risasi mwaka 1969
2. J,M. Kariuki alitekwa na kuuawa mwaka 1975
3. Robert Ouko alitekwa na kuuawa mwaka 1990
OMG...! Hivi komredi is still missing?!Kwa hiyo unatilia shaka uzalendo wa Katibu Mkuu wetu wa chama Kamaradi Kinana?
Una weka uthibitisho kuwa ili uwe mwanachama mtiifu wa CCM lazima uwe muongo na mnafiki....Hii ni sawa na mtu mwenye uraia wa nchi mbili ambaye akiharibu nchi moja anaweza kwenda nchi nyingine.
Katika hali isiyo ya kawaida uchaguzi mkuu uliopita Bashe alisikika akisema kura za ubunge apewe yeye na za urais apewe Lowassa.
2010 wakati wa uchaguzi mkuu Zitto Kabwe alimpigia chapuo JK kuwa apewe kura za urais tokea kipindi hicho Zitto hakuishi tena kwa amani CHADEMA hadi alipoondoka.
Kwa kauli za Bashe hata kufikia kuomba afukuzwe ni wazi ana uhakika wa uanachama wa chama kingine ambapo boss wake na ambaye yeye ni msemaji wake mkuu yupo.
Bashe ni kama ghost member ambaye hata leo CCM ikifa au kuharibikiwa yeye hana cha kupoteza na ndio maana alitoa go ahead kwa wapiga kura wake kumpa kura Lowassa hali akijua kupoteza urais ni mwanzo wa kufifia na kukosa nguvu kwa chama ambacho anajaribu kuaminisha watu yumo.
Wito wangu ni makada wa CCM wasiokuwa na uraia wa vyama viwili kukaa mbali na Bashe na kumuachia ngoma acheze mwenyewe kama alivyoicheza kwenye kampeni maana yeye akikosa huku anako kule ambapo moyo wake ( Lowassa) upo.