Wabunge wa CCM msimuige Hussein Bashe

Wabunge wa CCM msimuige Hussein Bashe

2010 wakati wa uchaguzi mkuu Zitto Kabwe alimpigia chapuo JK kuwa apewe kura za urais tokea kipindi hicho Zitto hakuishi tena kwa amani CHADEMA hadi alipoondoka.

Kwa kauli za Bashe hata kufikia kuomba afukuzwe ni wazi ana uhakika wa uanachama wa chama kingine ambapo boss wake na ambaye yeye ni msemaji wake mkuu yupo.
Mbona uchaguzi wa 2015 Mrema alisema Kura za Ubunge apewe yeye na za urais apewe Magufuli ingawaj kulikuwa na mgombea wa chama chake?!
 
Kwani akikaa kimya ndio atapona!
amesema yupo kwenye list ya kupotezwa, sasa kipi salama kwake, kuficha siri ya vitisho dhidi yake au kuweka bayana mapema ili kuweka kumbukumbu sawa kwa walinzi wa usalama wa raia wampe special protection ili madhara Zaidi yasimkute?
kama kweli wako desperate kummaliza hata baada ya kuweka haya yote bayana then hana sababu ya kuficha, wasingemsamehe hata kama angekaa kimya!

Naamini malengo ya utekaji ni kupeleka ujumbe wa hofu zaidi ya kudhuru au kuua. Utawala huu naona unafanyia kazi dhana ya kuwa ukifanikiwa kuwajengea maadui wako hofu, tayari una nusu ya ushindi. Mfano maandamano ya UKUTA yalizimwa kwa mazoezi yaloyolenga kujenga hofu. Kauli mbalimbali za watawala mfano kuvitishia vyombo vya habari, kamata kamata ya wapinzani na kesi zisizoisha zina nia ya kujenga hofu nk.

Dalili ya mtawala aliye na hofu na asiyejiamini ni kutishia na kufanya na kuamuru matendo yanayolenga kuleta hofu kwa anaowaongoza. Mtu jasiri anatakiwa awe huru kupambana na hofu kama Tundu Lissu. Kama ni kutekwa na kukamatwa huwa namwona Tundu Lissu akikamatwa kila siku. Ila bado sijaona mwanachama wa chama cha kijani akilala sero hata lisaa limoja tu la mfano.

Huyu Bashe bado anaamini kuwa akivaa kijani basi yeye ni nusu mungu au "untouchable" hagusiki!!. Ni wakati sasa ajifunze na aachane na huo mtazamo. Anatakiwa kwanza kutambua kuwa binadamu wote ni sawa. Watanzania wote ni sawa, wana thamani iliyo sawa. Haijalishi kama anaunga mkono upinzani au ccm.

Kama ni mkweli, Hussen Bashe tungemwona anapinga matendo yote machafu ya utawala kuanzia mwanzo. Sio mpaka achukuiwe kwa mahojiano masaa machache, ndio aanze kupiga kelele kama mtoto aliyezaliwa jana.

G
 
Hivi tunaweza kupewa uhalisia WA maisha ya yule baba ambae video yake ilitembea sana akikata mauno ya kale kawimboo ka hayati....hv anaishije kwa sasa? Kuna uwezekano kweli Jamii forum wote duniani hamna anaejua yule baba alikuwa mkoa gani tumtafute tumchezee tena kale kawimbo tuone mauno ya sasa na ya 2015 yanafanana.

# mtoa mada Mungu anakuona.
 
Mbona uchaguzi wa 2015 Mrema alisema Kura za Ubunge apewe yeye na za urais apewe Magufuli ingawaj kulikuwa na mgombea wa chama chake?!
Sababu alijua chama chake ni kivuli cha vyama..unajua hata ofisi zao zilipo??
 
Maslahi ya taifa yapi anayopigania bashe?? Yeye kusema 'alitekwa' na tiss kuna maslahi yoyote hapo??
eti bhana wakati tiss ipo kwa usalama wa taifa. polisi na mahakama ni kama wavu wakati mwingine hatari inapenya. usalama wa taifa (tiss)ndio mwokozi.
 
Mtoa mada look before you leap hapa hakuna cha u CCM, Chadema ama Lowassa hapa ni maslahi ya taifa kwanza. Haya masuala ya utekaji na utesaji tulikuwa tunasikia huko Kenya wakati wa Moi (Nyayo House) ni wakati muafaka kuibana serikali la sivyo it will be too late.
Kwa kutaja tu siasa za enzi za Nyayo na enzi za Mzee Jomo Kenyatta namkumbuka Charles Njonjo alivyokuwa akicheza kama Bashite naona ndiko tulikoelekea

Mbaya zaidi tuna u Kagameism (Twafwa)
 
Si raia ndo mnalijua leo? Weita niletee kasichana na maji kubwa barrrrrid.
Wapi nimesema bashe si raia..??we endelea kuleweka tu..humu hutaelewa kitu
 
Hii ni sawa na mtu mwenye uraia wa nchi mbili ambaye akiharibu nchi moja anaweza kwenda nchi nyingine.

Katika hali isiyo ya kawaida uchaguzi mkuu uliopita Bashe alisikika akisema kura za ubunge apewe yeye na za urais apewe Lowassa.

2010 wakati wa uchaguzi mkuu Zitto Kabwe alimpigia chapuo JK kuwa apewe kura za urais tokea kipindi hicho Zitto hakuishi tena kwa amani CHADEMA hadi alipoondoka.

Kwa kauli za Bashe hata kufikia kuomba afukuzwe ni wazi ana uhakika wa uanachama wa chama kingine ambapo boss wake na ambaye yeye ni msemaji wake mkuu yupo.

Bashe ni kama ghost member ambaye hata leo CCM ikifa au kuharibikiwa yeye hana cha kupoteza na ndio maana alitoa go ahead kwa wapiga kura wake kumpa kura Lowassa hali akijua kupoteza urais ni mwanzo wa kufifia na kukosa nguvu kwa chama ambacho anajaribu kuaminisha watu yumo.

Wito wangu ni makada wa CCM wasiokuwa na uraia wa vyama viwili kukaa mbali na Bashe na kumuachia ngoma acheze mwenyewe kama alivyoicheza kwenye kampeni maana yeye akikosa huku anako kule ambapo moyo wake ( Lowassa) upo.
Chai ya Lumumba ni tamu sana, mengine waachieni wenye uchungu na Taifa hili.
 
Go on Bashe, msema kweli ni mpenzi wa Mungu kwani ni wachache wenye ujasiri wa kuusema ukweli kisa wanaogopa vyama vyao. Ndo maana kwenye katiba mpya tulilia sana ugombea binafsi. Kwani hivyo vyama vinawabana baadhi ya watu.
 
Naamini malengo ya utekaji ni kupeleka ujumbe wa hofu zaidi ya kudhuru au kuua. Utawala huu naona unafanyia kazi dhana ya kuwa ukifanikiwa kuwajengea maadui wako hofu, tayari una nusu ya ushindi. Mfano maandamano ya UKUTA yalizimwa kwa mazoezi yaloyolenga kujenga hofu. Kauli mbalimbali za watawala mfano kuvitishia vyombo vya habari, kamata kamata ya wapinzani na kesi zisizoisha zina nia ya kujenga hofu nk.

Dalili ya mtawala aliye na hofu na asiyejiamini ni kutishia na kufanya na kuamuru matendo yanayolenga kuleta hofu kwa anaowaongoza. Mtu jasiri anatakiwa awe huru kupambana na hofu kama Tundu Lissu. Kama ni kutekwa na kukamatwa huwa namwona Tundu Lissu akikamatwa kila siku. Ila bado sijaona mwanachama wa chama cha kijani akilala sero hata lisaa limoja tu la mfano.

Huyu Bashe bado anaamini kuwa akivaa kijani basi yeye ni nusu mungu au "untouchable" hagusiki!!. Ni wakati sasa ajifunze na aachane na huo mtazamo. Anatakiwa kwanza kutambua kuwa binadamu wote ni sawa. Watanzania wote ni sawa, wana thamani iliyo sawa. Haijalishi kama anaunga mkono upinzani au ccm.

Kama ni mkweli, Hussen Bashe tungemwona anapinga matendo yote machafu ya utawala kuanzia mwanzo. Sio mpaka achukuiwe kwa mahojiano masaa machache, ndio aanze kupiga kelele kama mtoto aliyezaliwa jana.

G
Labda huna record sahihi za Bashe au unaamua tu kujipotosha!
Bashe hakuanza leo kubishia uonevu, hata 2010 walimkata wenzake kutokana na misimamo yake!
na toka ameingia bungeni yupo wazi misimamo yake, labda ujiulizi kwanini sasa aliingizwa kwenye hiyo blacklist, definitely anafahamika misimamo ndio maana akawa wanted, na angeweza ku-opt kukaa kimya na wala isingekula kwake!
Lissu ni mpinzani, chochote anachofanya ndio kazi yake number 1, bashe hana jukumu la lazima la kupambana na uonevu wa ccm, so chochote anachofanya ni kujitoa kafara Zaidi!
Zitto did this na mkamfukuza (hata nyinyi hamuwezi kuvumilia criticism), mtu from within akiwatingisha ni kujitoa kafara Zaidi kuliko your opponent! tazama mh. Zungu na team ya serikali wote walianza kumdai zitto vithibitisho, lkn alipoongea Bashe wote wali-paralyze! ni easy kumsema mpinzani wako kuwa anakuchafua, lkn kujibu shutuma za family member kunahitaji uwezo wa ziada!
 
Kwa kutaja tu siasa za enzi za Nyayo na enzi za Mzee Jomo Kenyatta namkumbuka Charles Njonjo alivyokuwa akicheza kama Bashite naona ndiko tulikoelekea

Mbaya zaidi tuna u Kagameism (Twafwa)
Wakumbushe wako wapi wanasiasa wazuri wa Kenya kama :
1. Tom Mboya alipigwa risasi mwaka 1969
2. J,M. Kariuki alitekwa na kuuawa mwaka 1975
3. Robert Ouko alitekwa na kuuawa mwaka 1990
 
Hata Nape hakuwahi kudhani ipo siku atfanyiwa vitendo vya kihuni. Alijua KwaZulu kuwa ameipigania sana CCM basi hakuna atakaemgusa. Alijua hayo yalikuwa kwa ajili ya wapinzani tu. Lakini Leo ameanza kuguswa tena kwa staili ya ajabu. Hata mleta maada Leo uko salama, kesho yako huijui. Tena nadhani hujawahi Hata kuwa na cheo kikubwa ndani ya chama kama akina Nape. Chukua hatua sio kila lifanywalo na uwapendao ni sahihi. Ikibidi sote tukemee maovu haya kwa usalama wa Taifa letu.
 
naunga mkono hoja ili kuendelea kutumikia matumbo yenu msimuige bashe...
 
Go on Bashe, go on Nape .Na wengine wabunge ccm ungeni tela ili tupate nguvu ya kuinyoosha serikal
 
Mfano tosha kama Nape alitishiwa Bastola na yeye ndio alikuwa mstari wa mbele kumweka Rais Magufuli madarakani nani atakuwa salama ?
Kama unaamini Nape alikuwa mstari wa mbele kumuweka Magufuli,utasema nini kuhusu Kikwete
 
YAANI MTOA POST UMEKAA NA ROHO MBAYA HIVI BASHE LEO NDO MNAJUA SIYO RAIA?...MIMI SINA CHAMA LAKINI NATAMANI NINGEKUJUA VIZURI NA NINGEWAJUA HAO WATEKAJI NINGEWAAMBIA WAKUTEKE WAKUFANYE FANYE MAZUURI YOTE HALAFU UKITOKA HUKO UJE UIMBE KIDUMU CHA CHA KIJANI AU ZIDUMU FIKRA ZA M/KITI....
WATU WANAONGELEA MASLAHI YA NCHI WEWE UMETANGULIZA TUMBO ETI BASHE ANA PAKUKIMBILIA AKIHARIBU HUKU....
HAKUNA WATU WENYE ROHO MBAYA KM WATEKAJI WALIOTUMWA
Mkuu, huyu mtu anachukulia jf kama kijiwe cha fb cha kupoteza muda. Hakuna mtu mwenye akili stahili anaweza kusema eti ana pa kukimbilia akiharibu huku. Ni lazima kila mtu ii aishi lazima awe na chama cha siasa au awe mshabiki wa chama fulani? Kwamba bila chama hawezi kuishi?

Fikra kama za huyu jamaa zinadumaza sana juhudi za ukombozi. Ni nani aliyepigiliwa misumari kwenye chama kiomoja kwamba hatakiwi kuhama ama kuanzisha ha kwake kwa mujibu wa ktiba ya Jmt?

Akili za jnisi hii zinatakiwa kubaguliwa katika mipango madhubuti ya ukombozi. Huwezi kutegemea mchango sahii kwa mtu anayesema "wale wanaokosoa serikali ama kutetea taifa, wanaharibu". Watu kama hawa ni wa kuwekwa kando kwanza halafu wapate mbinu na muda maalumu wa kuwaelimisha ili washiriki katika harkati kama ni lazima.

Kweli jamaa ubashite wake ni wa kiwango cha juu sana.
 
Mtu yeyote anayeweka mbele maslahi ya cha badala ya yale ya nchi mtu huyu amepotoka na hajitambui hata chembe.

Ningefurahi kuona Wabunge 50 wasio wanafiki na wanaoweka mbele maslahi ya Taifa badala ya yale ya MACCM kama Bashe na kufukuza wengine wote ambao wamepoteza hadhi ya kuwa Wabunge kwa sababu wao siku zote maslahi ya MACCM yana kipaumbele kikubwa kuliko ya Tanzania na Watanzania.

Hii ni sawa na mtu mwenye uraia wa nchi mbili ambaye akiharibu nchi moja anaweza kwenda nchi nyingine.

Katika hali isiyo ya kawaida uchaguzi mkuu uliopita Bashe alisikika akisema kura za ubunge apewe yeye na za urais apewe Lowassa.

2010 wakati wa uchaguzi mkuu Zitto Kabwe alimpigia chapuo JK kuwa apewe kura za urais tokea kipindi hicho Zitto hakuishi tena kwa amani CHADEMA hadi alipoondoka.

Kwa kauli za Bashe hata kufikia kuomba afukuzwe ni wazi ana uhakika wa uanachama wa chama kingine ambapo boss wake na ambaye yeye ni msemaji wake mkuu yupo.

Bashe ni kama ghost member ambaye hata leo CCM ikifa au kuharibikiwa yeye hana cha kupoteza na ndio maana alitoa go ahead kwa wapiga kura wake kumpa kura Lowassa hali akijua kupoteza urais ni mwanzo wa kufifia na kukosa nguvu kwa chama ambacho anajaribu kuaminisha watu yumo.

Wito wangu ni makada wa CCM wasiokuwa na uraia wa vyama viwili kukaa mbali na Bashe na kumuachia ngoma acheze mwenyewe kama alivyoicheza kwenye kampeni maana yeye akikosa huku anako kule ambapo moyo wake ( Lowassa) upo.
 
Back
Top Bottom