FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 100,506
- 123,776
Tatizo si majina dada angu, ila hoja. Inakuwaje hoja hiyo hiyo unaikubali kwa kuwa kuhisi imewakilishwa na mbunge wa chama chako, unapotekea ushahihisho kuwa ni mbunge wa chama kingine unaikataa? Hii ni ajabu kweli yani rafiki yako akisema embe tamu unasema ndio, asie rafiki yako akisema embe tamu unasema sio? Tuache ushabiki wa kichama wabunge wengi wapo pale kimwili tu lakini fikra hazipo wana jaza vitu tu hata hawafuatilii kinachoendelea na ndio maana wengi hawendi bungeni bila sababu za msingi, bunge la sasa ni la bajeti ya mwaka mzima lakini bajeti inapitishwa na wabunge hawazfiki hadi robo yao? Jamani nani sasa atatetea maslahi ya wananchi wakati wao ndio wametumwa. Hii nchi hatuko makini ndio maana umaskini hauishi, ujanja ujanja mwingi kwenye maisha.
Ewe punguani haujuwi kuwa pale kuna wanachama wa kambi tofauti?
Sasa mbunge wako kama ana akili anachotakiwa ni awakinaishe wa chama kingine wamuunge mkono. Na tumeshawahi kuona kuna hoja wabunge wa vyama vyote wanaziunga mkono wakiona zina maslahi ya jumla kwa Taifa. Hujayaona wewe?
Lakini hivi vi hoja vya mradi tu mpinzani anapinga kwa kuwa ni mpinzani, hivyo tunawahenyesha tu.