Sasa mbona wakizikuta wanakaa kimya? Hawasemi wanazitumia vipi kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wao.
Kwani wazee Wa Magamba huwa unawasikia wanasema wanazitumbuaje???
Jamani wabongo, m2 kukwambia kuwa huku kuna mwizi anakuibia inatosha, kumbuka wanao hangaika ni walala hoi, na wala si wabunge wa CDM, so CDM were right to inform the majority who is suffering, then people coult take decion, na si mpaka,walewle walio kufundisha au kufichulia siri ndo wafnye maamuzi,
Hii kitu inanikumbusha chengi ya rada, wabongo tuliambiwa kuwa tumeibiwa, lakini tukawa tunakataa, mbaya zaiadi tukaambiwa hadi mwizi lakina tukataka waingereza ndo wafanye maamuzi, mpaka walipo ona yakuwa tumekuwa wajinga, wakaamua kuwapeleka mahakamani wezi kwa upande wao, nasi ndio tukajifanya kudai chenji
Ninacho sema nikwamba, CDM walitustua wabongo, lakini badala ya kufuatilia jinsi ya kuziokoa hizo hela walau tununue madawa, sisi tumebaki kuwalaumu, tumesahau kuwa nao ni binadamu na pesa ni tamu kwakila m2,
Wbongo tulitakiwa baada ya kuambiwa na CDM, tufanye mikakati ya kuihoji government, na tuangalie jinsi ya kuziokoa, so ukisema eti CDM wanazifanyia nini unakosea eg
wewe umeenda shambani kwa mkulima, umekuta nyani anatafuna mahindi yake, umemwambia mkulima, kuwa ndani ya shamba kuna nyani anatafuna mahindi, bahati mbaya mkulima hajakujibu wala hajachukua hatua nawe uko karibu na shamba, je huoni kuwa nawe utajikuta huna la kufanya? na badala ya mkulima kumfukuza yule nyani nae anaanza kukulaumu
So waTZ tulitakiwa baada ya kuambiwa tuchukue hatua, na sio kuwalaumu CDM, wakati walio na hela na wanao gawa zile posho tunesha ambiwa
Hakika wameonesha udhaifu mkubwa na uongo kwa wananchi hata hizi posho zilizopandishwa siku za karibuni wamekaa kimya kama siyo wao!!Kwa bahati nimeamua kuwa siyo mwanachama wa chama chochote cha siasa bali ni shabiki wa siasa na baadhi ya wanasiasa. Mfano halisi wanasiasa ninao wakubali bila kujali itikadi zao ni Mbowe, Slaa, Mnyika, Lissu, Magufuli, Lowassa nk. Napata fursa ya kuwa makini na kauli za wanasiasa wa nchi hii bila kujali chama atokacho. Wabunge wa CDM Wamekuwa na msimamo wa kutopokea posho zao katika vikao vya bunge. Msimamo ambao wananchi tulio wengi tunauunga mkono mia kwa mia. Lakini utaratibu wa malipo ya posho hizo ni halali kwa mujibu wa kanuni za bunge. Na bahati mbaya hawapewi mkononi hivyo huingizwa moja kwa moja kwenye akaunti zao. Kwa maana ya kwamba watake watapata, wasitake watapata. Ule msimamo wa dhati upo kweli? Manake sijasikia tena wakija na mpango hasi kuhusu posho hizo kuwa, kwa sababu tulizikataa lakini mnatulazimisha. Tunaziingiza katika mradi fulani wa wananchi. Vinginevyo tunarudi kulekule kuwa. Kauli zitokazo midomoni mwa wanasiasa ni tamu masikioni mwa wananchi, lakini kuna dhamira tofauti katika mioyo yao.
Ilipo sema shibuda akaonekana msaliti alipo sema joseph selasini na akunaay wakaonekana ni mashujaa kuhusu ongezeko la posho.tatizo la watanzania ni ushabiki wa vyama ongezeko la posho hoja imeletwa na shibuda,selasini na akunaay na mpaka sasa ni zitto pekee ambaye hachukui posho sasa kuna mpumbavu mmoja anasema eti wanalazimishwa kuchukua posho mbona hawamlazimishi zitto?acheni ujinga mara hatumtambui rais ila tunataka juice za ikulu na picha na rais.mnyika kasign muafaka na nchimbi leo anakuja kutudanganya watanganyika tuipende nchi kuliko haya makampuni yanayojiata vyama vya siasa.
Ni nani aliyekuambia kuwa Zitto hapokei posho? Alijuaje kuwa posha imeongezeka kama hakukuta mabadiliko kwenye akaunti yake.Posho zinaingizwa mojamoja kwa moja kwenye akaunti bila kujali kuwa huitaki au unaitaka.Anachofanya Zitto ni kuipeleka hiyo posho kwenye NGO kama sijakosea.Nadhani wewe ndio juha zaidi kwa kuandika upuuzi bila kutumia akili yako.Farouk sana wewe tena Karim!
Ni vizuri kusema ukweli au kukaa kimya kama hujui ukweli. Toka tarehe 8 Juni 2011 sichukui posho za vikao. Posho haiingizwi kwenye akaunti kwa lazima kama tunavyoambiwa hapa jukwaani. Mbunge husaini fomu maalumu za kuonyesha amehudhuria kikao na kutokana na fomu hizo hulipwa posho. Mimi nimekataa kusaini fomu hizo ili Ofisi ya Bunge isiwe njia ya kuniingia fedha hizo kwenye akaunti yangu. Hivyo sipokei Posho za Vikao kwa kuwa sisaini fomu za maalumu za posho.
Sio kwenye Bunge tu, sipokei posho kwenye viako vyote ninavyoalikwa kama Mbunge au ambavyo mimi ni mjumbe kutokana na wadhifa wangu. Nimekataa posho ya kikao katika kikao cha Bodi ya Barabara Kigoma, Kamati ya Ushauri ya Mkoa Kigoma na Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya Kigoma. Vilevile nimekataa posho za kikao kwenye semina ya CAG kuhusu kamati za Bunge. Ukipenda kuona ushahidi wa risiti (stakabadhi) za posho nilizokataa nenda katika blogu yangu Zitto na Demokrasia
Uamuzi wa kukataa malipo makubwa kwa wabunge ni uamuzi wa kisera wa chama chetu. Mimi ninatakeleza maagizo ya chama kwa mujibu wa Ilani ya Uchaguzi ya CHADEMA. Hili sio suala la Zitto ni suala la chama. Zitto ni msemaji tu wa suala hili kwa sababu ni Waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi na kwa kweli lazima niwe mbele kutekeleza maamuzi ya chama kivitendo.
Nimejuaje kama posho zilipanda? Nilijuaje mkataba wa Buzwagi umesainiwa? Slaa alijuaje kuna wizi wa EPA Benki Kuu? Nilijuaje kuna mabilioni yamechotwa kupitia kampuni ya meremeta? Nadhani hapa utajua kuwa Mbunge yeyote makini ana vyanzo vingi vya habari
Nduguyo Zitto
Ni vizuri kusema ukweli au kukaa kimya kama hujui ukweli. Toka tarehe 8 Juni 2011 sichukui posho za vikao. Posho haiingizwi kwenye akaunti kwa lazima kama tunavyoambiwa hapa jukwaani. Mbunge husaini fomu maalumu za kuonyesha amehudhuria kikao na kutokana na fomu hizo hulipwa posho. Mimi nimekataa kusaini fomu hizo ili Ofisi ya Bunge isiwe njia ya kuniingia fedha hizo kwenye akaunti yangu. Hivyo sipokei Posho za Vikao kwa kuwa sisaini fomu za maalumu za posho.
Sio kwenye Bunge tu, sipokei posho kwenye viako vyote ninavyoalikwa kama Mbunge au ambavyo mimi ni mjumbe kutokana na wadhifa wangu. Nimekataa posho ya kikao katika kikao cha Bodi ya Barabara Kigoma, Kamati ya Ushauri ya Mkoa Kigoma na Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya Kigoma. Vilevile nimekataa posho za kikao kwenye semina ya CAG kuhusu kamati za Bunge. Ukipenda kuona ushahidi wa risiti (stakabadhi) za posho nilizokataa nenda katika blogu yangu Zitto na Demokrasia
Uamuzi wa kukataa malipo makubwa kwa wabunge ni uamuzi wa kisera wa chama chetu. Mimi ninatakeleza maagizo ya chama kwa mujibu wa Ilani ya Uchaguzi ya CHADEMA. Hili sio suala la Zitto ni suala la chama. Zitto ni msemaji tu wa suala hili kwa sababu ni Waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi na kwa kweli lazima niwe mbele kutekeleza maamuzi ya chama kivitendo.
Nimejuaje kama posho zilipanda? Nilijuaje mkataba wa Buzwagi umesainiwa? Slaa alijuaje kuna wizi wa EPA Benki Kuu? Nilijuaje kuna mabilioni yamechotwa kupitia kampuni ya meremeta? Nadhani hapa utajua kuwa Mbunge yeyote makini ana vyanzo vingi vya habari
Nduguyo Zitto
Hapa tunachanganyikiwa kidogo. Siku ya mdahalo kati ya Lissu na Myaa, Lissu alitamka wazi kuwa wao posho huzikuta tayari zimeingizwa kwenye akaunti kwa maana hiyo hakuna namna ya kuzikwepa. Tupeni kauli moja yenye msimamo ili kuondoa utata mkuu.
Kwa hiyo mkulima akikaa kimya nawe unaungana na nyani kuanza kula hayo mazao badala ya kumfukauza nyani na kumsadia ulinzi mkulima mpaka atakapoamka kutoka usingizini.