Wabeba mabango Tabora wamkera Rais Magufuli

Naona Mkuu wa Mkoa Aggrey Mwanri imembidi kuinuka kwenda kuweka mambo sawa. Maana yeye kama mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama walitakiwa kujua uwepo wa jambo lolote lenye lengo la kumkera Mkubwa. Nakumbuka May Mosi kule Kilimanjaro mabango mengi ilibidi yakamatwe na vyombo vya ulinzi ili yasiingie uwanjani lakini mtaani yalipita. Siku chache baadae Mkuu Mkoa Meck Sadik anaamua kupumzika ili kuwapisha vijana wenye nguvu zaidi. Ndio wakaja vijana wakina Anna Mghwira kuchukua nafasi
 
Juzi PM alipokuwa Mbozi kuna mama mkeleketwa wa chama kjana, aliandaa bango lakn alzuiwa asingie nalo kwa nguvu kubwa.
 
Kwa Tabora kafanya kazi kubwa sn hakuna km barabara na Maji ilo ndo lilikuwa tatizo kubwa kwa wana nchi wa Tabora hao wa mabango itakuwa waloambiwa kutoka ktk eneo la Rayrway station ili iweze kutanuliwa yan kuvunja nyumba zao na wapishe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom