Waandishi wengine mnajidhalilisha

emalau

JF-Expert Member
Apr 25, 2009
2,775
3,100
Wadau,

Leo asubuhi nilikuwa nikiangalia kipindi cha jicho letu ndani ya habari ambacho hurushwa na Star TV kila Jumamosi. Wageni waalikwa kwa upande wa DSM alikuwa Pascal Mayala na mwingine simkumbuki jina.

Kwa upande wa Mwanza, walikuwepo vijana wachambuzi wazuri na wanaonekana wana weledi mkubwa wa mambo ya habari, ulipofika wakati wa fursa ya upande wa DSM, nimewashangaa waandishi hawa Pascal Mayala na mwenzake ambao wameamua kwa makusudi kujitoa ufahamu wakitetea kwamba Mkapa kuwaita watu wapumbavu na malofa si tusi!

Hisia niliyopata ni kwamba CCM wamepanga watu wao katika baadhi ya vyombo vya habari ambao watakuwa wanachambua lakini kwa kuwatetea, pamoja na kwamba inawezekana ni mkakati wa kisiasa lakini binadamu unapolazimika kutamka kitu ambacho kinaenda tofauti na dhamira yako unakuwa mtumwa.

Kwa kweli kwa mara ya kwanza nimemuona Pascal Mayala akijivisha nafsi isiyo ya kwake. Waandishi msijidhalilishe kiasi hiki, uchaguzi utapita lakini madoa na makovu ya kujidhalilisha huchukua muda mrefu kwisha.

Nawasilisha
 
Mkapa hajatukana wananchi. Wananchi tunafahamu nchi imeshakombolewa na tulishiriki kikamilifu kuikomboa. Wewe unadharau juhudi za wananchi
 
muhindo

Nikusahihishe kwanza, hatutaki mabadiliko tu Bali mabadiliko ya vitu, hatutaki wala rushwa, hatutaki mafisàdi, tunataka mabadiliko, hatutaki mabwanyenye na wenye ndimi mbili, tunataka Wa kututumikia na siyo wa kutumikiwa, tunataka wanaoweza kukemea rushwa ..hayo ndo mabadiliko ya kweli na rais bora atatoka CCM
 
Last edited by a moderator:
Nikusahihishe kwanza, hatutaki mabadiliko tu Bali mabadiliko ya vitu, hatutaki wala rushwa, hatutaki mafisàdi, tunataka mabadiliko, hatutaki mabwanyenye na wenye ndimi mbili, tunataka Wa kututumikia na siyo wa kutumikiwa, tunataka wanaoweza kukemea rushwa ..hayo ndo mabadiliko ya kweli na rais bora atatoka CCM

BORA RAIS atatoka CCM. Na RAIS BORA atatoka UPINZANi:whoo::high5:
 
hata hivyo ni rahisi sana kufuta neno fisadi kwenye ubongo wa watanzania lakini pia ni kazi kubwa na vigumu sana kufuta maneno kama wapumbavu na malofa
 
Back
Top Bottom