Waandi wa habari wa Tanzania

Waandi wa habari wa Tanzania

Daata

JF-Expert Member
Joined
Dec 24, 2012
Posts
4,762
Reaction score
2,069
Wakuu haki na amani iwe kwenu.

Kwa kipindi kirefu sasa kumekuwa na lawama kwa waandishi wa habari wa Tanzania baada watu kuona kuwa wanaripoti habari zenye mwelekeo moja wa kuitetea serikali na kunyamazia habari zote zinazokosoa au zenye tafsiri hasi kwa serikali.

Habari za kiuchunguzi dhidi ya matendo ya watendaji wa serikali zinakwepwa kwa kila namna lakini zenye kuipamba serikali zitaandikwa kwa wino mnene.

Sababu ni moja kuwa wahariri wa vyombo vyetu vya habari wameshasoma mwelekeo wa serikali, hivyo ili kuwa salama na kuendelea kuwepo inabidi kufuata kile serikali kinataka.

Wanaelewa kuwa wakijaribu kuandika habari zinakosoa serikali watakutana na TCRA kukisimamisha chombo hicho kwa miezi kadhaa au hata kukifutia usajili bila kukisikiliza .

Nimeona maoni ya watanzania kuwa wanatamani mwandishi wa CNN Larry Madowo aje Tanzania halafu wabadiliashane na wa Tanzania kadhaa.

Ukweli ni kwamba haitafanya kazi kwa sababu akija Tanzania atakutana na serikali ambayo habari kama hizo hazitakiwi na mwishowe ataufyata na kuwa kama waandishi wetu waliounga juhudi.
Nawasilisha.
 
NI KWELI TUNATAKA DIAMOND, MILLARD AYO TUWAONGEZE NA MAULID KITENGE
Akija bongo mazingira yake ya kufanya kazi yatakuwa magumu na mwishowe atabaki kasuku wa serikali.
 
Sasa mbona wanaandika ya serikali na kuitetea uozo wake. Mfano Ezekiel Kamwaga yule anayetumika kama dekio.
Mi nina imani kuwa pamoja na waandishi wanaoitetea serikali moja kwa moja, bado tuna hazina ya waandishi wenye uzalendo wa kutoa taarifa za kiuchambuzi lakini mazingira yamewalazimu kuwa wa upande moja.
Nchi hii ukisubiri taarifa upewe na serikali utapata iliyochujwa, lakini waandishi wetu hawathubuti kuchimba zaidi maana wataishia kuambiwa nani amekupa ruhusa ya kupata hizi taarifa bila kujali ukweli wa taarifa yenyewe.
 
Back
Top Bottom