X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,810
Amri za Allaah (Subhaanahu wa Taala) tumeziacha nyuma ya migongo yetu na kuyafanya matashi yetu kuwa ndio muongozo wa maisha yetu.
Uzinifu tumeufanya kuwa ni ada yetu na pombe ndio muongozo wa maisha ya leo. Imefika hadi ya kuona haramu kuwa halali na halali kuwa ni haramu. Tumejikubalisha kuwa akiba haina faida bila ya riba. Mauziano yasiyokuwa na uongo, utapeli sasa yamepitwa na wakati.
Imekuwa ni desturi kuona kila kona za majengo na sehemu za mikusanyiko ya watu pamoja na barabarani kuwepo picha za utupu zenye kuamsha hisia za uzinifu. Sio matangazo ya biashara halali wala haramu zenye uadilifu wa kutilia mkazo ubinaadamu na haki za imani zisiopendelea picha hizo.
Matangazo ya pombe yameshika kasi huku simu, sigara, vyakula na kadhalika vikiwa havipo nyuma kurusha mabomu ya uzinifu.
Matokeo yake hayo, ni kubakia jamii kwenye matatizo na udhaifu wa mwaadamu wa uchu wa kutosheleza hisia zake kwa kujamiiana tu. Utakuta kwa mfano tangazo la simu lenye msichana aliyevaa jeans yenye kubana akiwa na mvulana aliyesokota nywele zake kwa mtindo wa rasta. Huku ujumbe wa tangazo hilo likisomeka:
Nini tunawafunza vijana wetu kwa matangazo kama hayo? Na yareiti tangazo hilo lingelikuwa ni moja, lakini kona za barabara nzima zimetapakaa matangazo mfano wa hayo. Lahaula! Kama vijana hawakutoroka shule, tutegemee kutumbukia kwenye uzinifu wa kuiga hizo picha.
Alhamdulillaah, tumepewa macho lakini hakika atakayeyakemea mambo hayo kwa sauti kali ndio ataambiwa kuwa ni kipofu, mpinga maendeleo, mjinga, hafai katika jamii, mshamba na kadhalika. Wale Waislamu wenye imani zisizoeleweka, ndio wataanza kumuita kwa istihzai na kejeli; Ustadh, Shaykh na kadhalika.
Tuikumbuke kauli ya Mola (Subhaanahu wa Taala) Aliposema kuwa tuna viungo lakini hatuvitumii:
Na Tumeiumbia Jahannamu majini wengi na watu. Wana nyoyo, lakini hawafahamu kwazo. Na wana macho, lakini hawaoni kwayo. Na wana masikio, lakini hawasikii kwayo. Hao ni kama nyama howa, bali wao ni wapotofu zaidi. Hao ndio walioghafilika
Al-A'araaf: 179
Yote yametokana na wigo wa kuwaiga wasio kuwa Iman Juu ya Mwenyezi Mungu na kuanza kidogo kidogo kufuata tabia na vitendo vyao. Mtume (Swalla Allaahu alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((Mtafuata nyendo za wale waliokuja kabla yenu hatua kwa hatua mpaka itafika hadi wakiingia katika shimo la kenge, na nyinyi mtaingia pia)) Wakasema (Maswahaba): Ewe Mtume! Je, unamaanisha Mayahudi na Manaswara? Akasema: (Hivyo nani basi mwengine?)
Al-Bukhariy na Muslim
Uzinifu tumeufanya kuwa ni ada yetu na pombe ndio muongozo wa maisha ya leo. Imefika hadi ya kuona haramu kuwa halali na halali kuwa ni haramu. Tumejikubalisha kuwa akiba haina faida bila ya riba. Mauziano yasiyokuwa na uongo, utapeli sasa yamepitwa na wakati.
Imekuwa ni desturi kuona kila kona za majengo na sehemu za mikusanyiko ya watu pamoja na barabarani kuwepo picha za utupu zenye kuamsha hisia za uzinifu. Sio matangazo ya biashara halali wala haramu zenye uadilifu wa kutilia mkazo ubinaadamu na haki za imani zisiopendelea picha hizo.
Matangazo ya pombe yameshika kasi huku simu, sigara, vyakula na kadhalika vikiwa havipo nyuma kurusha mabomu ya uzinifu.
Matokeo yake hayo, ni kubakia jamii kwenye matatizo na udhaifu wa mwaadamu wa uchu wa kutosheleza hisia zake kwa kujamiiana tu. Utakuta kwa mfano tangazo la simu lenye msichana aliyevaa jeans yenye kubana akiwa na mvulana aliyesokota nywele zake kwa mtindo wa rasta. Huku ujumbe wa tangazo hilo likisomeka:
Leo nitakosa masomo, nahitaji kupunga upepo.
Nini tunawafunza vijana wetu kwa matangazo kama hayo? Na yareiti tangazo hilo lingelikuwa ni moja, lakini kona za barabara nzima zimetapakaa matangazo mfano wa hayo. Lahaula! Kama vijana hawakutoroka shule, tutegemee kutumbukia kwenye uzinifu wa kuiga hizo picha.
Alhamdulillaah, tumepewa macho lakini hakika atakayeyakemea mambo hayo kwa sauti kali ndio ataambiwa kuwa ni kipofu, mpinga maendeleo, mjinga, hafai katika jamii, mshamba na kadhalika. Wale Waislamu wenye imani zisizoeleweka, ndio wataanza kumuita kwa istihzai na kejeli; Ustadh, Shaykh na kadhalika.
Tuikumbuke kauli ya Mola (Subhaanahu wa Taala) Aliposema kuwa tuna viungo lakini hatuvitumii:
Na Tumeiumbia Jahannamu majini wengi na watu. Wana nyoyo, lakini hawafahamu kwazo. Na wana macho, lakini hawaoni kwayo. Na wana masikio, lakini hawasikii kwayo. Hao ni kama nyama howa, bali wao ni wapotofu zaidi. Hao ndio walioghafilika
Al-A'araaf: 179
Yote yametokana na wigo wa kuwaiga wasio kuwa Iman Juu ya Mwenyezi Mungu na kuanza kidogo kidogo kufuata tabia na vitendo vyao. Mtume (Swalla Allaahu alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((Mtafuata nyendo za wale waliokuja kabla yenu hatua kwa hatua mpaka itafika hadi wakiingia katika shimo la kenge, na nyinyi mtaingia pia)) Wakasema (Maswahaba): Ewe Mtume! Je, unamaanisha Mayahudi na Manaswara? Akasema: (Hivyo nani basi mwengine?)
Al-Bukhariy na Muslim