Vyuma vilikaza enzi hizo!

Vyuma vilikaza enzi hizo!

mkuu naona mabandiko yako, unajitahidi kutumia nguvu kubwa sana kudhihirisha serikali ya ccm chini ya raisi JPM mambo yako poa tu ajira zipo, maisha hayana gharama, uhuru wa maoni upo, demokrasia ipo, yaani kila kitu kipo, sera za ccm zinatimizwa zote tena kwa wakati n.k.

inahitaji kujitoa akili ili mtu usome na kuelewa unachokipigania hivi karibuni kupitia sredi zako uchwara zenye ukakasi mwingi... kama wewe unapata milo mitatu kwa siku na ukakula hizo unazoziita bata sio wote wako hivo...
 
Maisha yapo kawaida tuu...

Enzi unazozungumzia nadhani ni baada au kipindi cha vita ya kagera, kama sijakosea... ndiyo nchi ilifunga mkanda na vyuma kukazika kisawa sawa...

Wanaolalamika vyuma kukaza bado hawajaona maana halisi ya vyuma kukaza, waache sasa wafanye haya maandamano wanayotaka kufanya alafu waone vyuma vitakavyokaza...

cc: mahondaw
 
Kweli kabisa watu walikua wanatafuta majani yakitoa povu tu wanafulia,hivi sasa wengi baba zao ndio walioangusha mashirika wanawakejeli wabongo kujidai wazalendo!

sasa wewe unawalalamikia nini.kama wemangusha mashirika wakat wewe na famillia yako mna uwezo wa kutafuta majani mkafulia nguo
 
watu wanacompare awamu hii na awamu iliyopita
wewe unaturudisha awamu ya kwanza!!!awamu ya vita ya kagera!!!!
Awamu ya mwanzo Pesa haikuwa msingi sana maana vitu vingi vilikuwa bure,mfano kuni,MAJI,mboga,mapenzi nk mvua ilikuwa ya kutosha chochote panda nguvu yako tu,tofauti na siku hizi no money no life.
 
baba yangu Nyani Ngabu, hiyo enzi unayosema ilikuwa Sera ya kijinga ya ujamaa
huenda ingekua sera nyingine nchi ingekuwa mbali sana,Mwl alichangia pakubwa kudidimiza hii nchi
 
Mwaka 1986 hakukuwa na vita na ugawaji ulikuwepo.
fananisha kisomi:
pato la taifa lilikuaje
ukuaji wa uchumi..
makusanyo ya kodi
idadi ya watu nk..sio kufanani mambo ya bar na dukani

kumlisha mwanao ni wajibu na sio fadhila.
 
We shukuru tu una kazi yenye pesa inayokufanya uone vyuma vimelegea... Mambo sio mazuri mkuu mie mkulima gunia la mahindi 20,000 we unafikiri mie naishije hapo sasa
 
kwahiyo kwa sababu nyie mlipanga foleni za kununua sukari mnataka na sisi tupange foleni za kununua sukari, with this mentality bado tuna safari ndefu sana.

Kuna aspect nyingi kwenye accessibility ya kitu fulani, eti kwa sababu kiko mahali fulani basi hali ni nzuri, Je umejiuliza kama kila mtu anamudu kukipata hicho kitu kwa urahisi, bei nafuu, na ukaribu/uharaka.

Kuna vitu vya msingi zaidi vya kuangalia kama Elimu, Afya, Freedom of speech than hizo colgate, savanna sijui Mo orange
 
Kwa hiyo tuishi maisha ya kijima kisa zamani tulipitia hiyo hali? Binadamu anatakiwa kupiga hatua ya maendeleo kwenda mbele na sio kurudi nyuma.
Kabisa, eti kwa sababu wao wameteseka wanataka na wengine wapitie maisha kama yao, si maajabu haya
 
Watu tulipanga foleni maduka ya ugawaji lkn wakat ule ilikuwa bidhaa ndio ngumu kupatikana sio kuwa watu walikuwa hawana uwezo wa kununua...na hao wenye vitambi na magari mazuri walikuwepo hata enzi hizo
 
Ngabu hukupaswa kuuliza kwamba nani ametaka kwenda dukanj kununua hiki ama kile dukani akakosa,ulipaswa kuuliza nani ametaka kwenda dukani kununua hiki ama kile akashindwa kwenda kununua kwa kuwa hana fedha na vitu vimepanda bei.
 
Ngabu hukupaswa kuuliza kwamba nani ametaka kwenda dukanj kununua hiki ama kile dukani akakosa,ulipaswa kuuliza nani ametaka kwenda dukani kununua hiki ama kile akashindwa kwenda kununua kwa kuwa hana fedha na vitu vimepanda bei.
 
Soft mko nyie mnaoosha vyombo na kuwaogesha wazee wa kizungu huko ughaibuni!
Kwa hili nakuunga mkono, Hata weekend kama leo Bar zipo full, Jumamosi ndio usiseme watu wanakula bata, Tatizo mafisadi na wezi ndio wanalalamika

Eti maandamano wanapanga kisa Baba zao pesa imekata

Hivi kama mtu ulikuwa hutegemei dhuluma na semina huwezi lalamika
 
.....Nilikuwa natumwa dukani, kuweka foleni, unaweza kuweka jiwe, au kopo kusubili mgawo wa sulari....na ukipata sukari, unalazimishwa kununua usivyobihitaji kama nyembe, viberiti nk...
"Ama kweli mchonga meno nchi ilimshinda"
Wazungu walimbana. Hakushindwa.
 
Back
Top Bottom