Vyuma vilikaza enzi hizo!

Vyuma vilikaza enzi hizo!

.....Nilikuwa natumwa dukani, kuweka foleni, unaweza kuweka jiwe, au kopo kusubili mgawo wa sulari....na ukipata sukari, unalazimishwa kununua usivyobihitaji kama nyembe, viberiti nk...
"Ama kweli mchonga meno nchi ilimshinda"
 
Leo nimekuelewa wewe jamaa, ukiwaona utacheka asee watu wanapiga starehe wanalia vyuma vimekaza

tusidanganyane, watu waliomaliza chuo 2016 kuja mbele wanajuaje kua vyuma vimekaza? wakati walikua wanakula pesa kwa mrija?
 
Wanasema vyuma vimekaza lkn wanacheza tatu mzuka,wanacheza biko,wanapata hela za kununua bando kila siku nakushinda Facebook na insta ,soko la smart phone kila siku linazidi kukua nchini Tanzania.
 
Unajua nimekuja kuhitimisha kuwa sisi Watanzania tuko ‘soft’ sana, hususan nyakati hizi.

Unakuta mtu ana likitambi lake likubwa tu halafu eti analalamika vyuma vimekaza.

Watu wanakula bata kila kona huku wanalalamika vyuma vimekaza.

Wakati mwingine huwa nikiwaangalia naishia kucheka na kuwaambia ‘mnacheza nyie’.

Wahenga wenzangu watakubaliana nami kuwa kuna kipindi nchi hii vyuma vilikaza kweli kweli.

Enzi za miaka ya 80, hususan mwanzoni hadi katikati.

Enzi za maduka ya ugawaji. Watu mnajipanga mstari kusubiri kununua bidhaa kama sukari, unga, mafuta, mchele, miche ya sabuni, na vitu vinginevyo.

Bidhaa hizo za kila siku zilikuwa adimu. Sabuni za kuogea kama vile Imperial Lather na Palmolive zilikuwa hazipatikani kirahisi nchini. Kuzipata ilibidi mtu aende nje ya nchi kama Kenya au Ulaya huko. Watu tulikuwa tunaogea sabuni za Mbuni. Sabuni hiyo hiyo unaoshea vyombo, hiyo hiyo unaogea na hiyo hiyo unafulia nguo.

Hata dawa za mswaki zilikuwa adimu. Kunywa hata soda lilikuwa ni jambo la anasa. Watu mnaweza kupitisha hata miezi sita hamjanywa soda. Hata kula mkate wa siha ilikuwa nadra.

Kula pilau nako hivyo hivyo. Kula kuku pia.

Kunywa bia ndo kabisa! Kukaza huko kwa vyuma kulifanya pombe za kienyeji zipande chati, hususan wanzuki na kangala.

Sasa leo nikiona hivi vitoto vya miaka ya 90 vikijiliza liza eti vyuma vimekaza huku majumbani kwao kuna DSTV, maduka yamejaa kila aina ya bidhaa, vikienda baa vinakunywa Smirnoff, Savanna nini sijui, Hennessy V nini sijui, vinavaa nguo za madizaina [hata kama ni feki], yaani starehe mwanzo mwisho!

Nikiona hivyo huwa najiuliza sana...kama sasa hivi vyuma vimekaza...enzi zile vilikuwa vimefanya nini sasa!

Nani humu kaenda dukani akakosa Colgate, kwa mfano?

Nani hajanywa soda mwaka mzima? Nani hajanywa Fursana au Mo Orange kisa kashindwa kununua kwa sababu vyuma vimekaza?

Nani kaenda dukani kununua Rinju akakosa?

Tumekuwa watu walaini mno sisi. Watu wa kudekadeka tu.

Vyuma vilikaza miaka hiyo. Hakuna vyuma vilivyokaza miaka hii.

Acheni usleki mayai.


Nyani mbona unakua dishonest namna hii ndugu?

Kwahiyo unaturudisha 1980's?

Really?
 
Kwani ni Lazima Kila muda uanzishe Uzi Mzee!!??Au unapata Malipo?Kwahiyo kama kipindi cha Nyuma Uchumi uliyumba zaidi ya Leo watu wasilalamike leo simply because Kipindi cha Nyuma ilitokea zaidi ya Hivi??Wee Jamaa
 
Nilikuwa najua kuwa platinum member ni mtu mwenye uwezo wa hali ya juu kifikra na hoja loooo!!! kumbe hata jingalao yupo vizuri.
Mtu anayeishi utumwani lazima awe ni mtumwa, huyu alikuwa kinara wa UKUTA akichochea kuni kutokea America kama afanyavyo Mange sasa!
 
Hoja hizi hazina mashiko...
Mambo yamebadilika kuanzia vizazi, teknolojia, pato la taifa, ufikiri wa raia, population, exploration of natural resources nk
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Unajua kitanda usicholalia huwezi jua kunguni wake bwana Ng'abu hiki kilio wanacholia wenzio hakigusi ndio maana.
 
mkuu nyani ngabu mimi nikisoma thread zako nakumbuka ile blog ya dada NANCY tuuuu.... daaa ngoja nilie kwanza maana siku hizi imekuwa kama pagara hamna kitu

hata vile vitu vyako hatuvipati...

nyani ngabu mpiganaji hahahah
 
Mkuu kunautofauti hapo maana Zaman hela ilikuwepo ila vitu vilikuwa hadimu. Na Sasa hivi hela hakuna ila vitu/bidhaa zipo.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Kweli waTanzania wengi hawanaga akili especially mtoa mada.


Yani unalinganisha mwaka 1980 NA 2018 unahitaji kupimwa akili sio bure.

Kwa mawazo yako bado tunasafari.

Nyie ndo wale mnawaambia watoto wenu mlikuwa mnatembea miguu peku kwenda shule. Zama zimabadilika

KUBALI MABADILIKO UENDANE NA MABADILIKO AU MABADILIKO YAKUBADILISHE.
 
Unajua nimekuja kuhitimisha kuwa sisi Watanzania tuko ‘soft’ sana, hususan nyakati hizi.

Unakuta mtu ana likitambi lake likubwa tu halafu eti analalamika vyuma vimekaza.

Watu wanakula bata kila kona huku wanalalamika vyuma vimekaza.

Wakati mwingine huwa nikiwaangalia naishia kucheka na kuwaambia ‘mnacheza nyie’.

Wahenga wenzangu watakubaliana nami kuwa kuna kipindi nchi hii vyuma vilikaza kweli kweli.

Enzi za miaka ya 80, hususan mwanzoni hadi katikati.

Enzi za maduka ya ugawaji. Watu mnajipanga mstari kusubiri kununua bidhaa kama sukari, unga, mafuta, mchele, miche ya sabuni, na vitu vinginevyo.

Bidhaa hizo za kila siku zilikuwa adimu. Sabuni za kuogea kama vile Imperial Lather na Palmolive zilikuwa hazipatikani kirahisi nchini. Kuzipata ilibidi mtu aende nje ya nchi kama Kenya au Ulaya huko. Watu tulikuwa tunaogea sabuni za Mbuni. Sabuni hiyo hiyo unaoshea vyombo, hiyo hiyo unaogea na hiyo hiyo unafulia nguo.

Hata dawa za mswaki zilikuwa adimu. Kunywa hata soda lilikuwa ni jambo la anasa. Watu mnaweza kupitisha hata miezi sita hamjanywa soda. Hata kula mkate wa siha ilikuwa nadra.

Kula pilau nako hivyo hivyo. Kula kuku pia.

Kunywa bia ndo kabisa! Kukaza huko kwa vyuma kulifanya pombe za kienyeji zipande chati, hususan wanzuki na kangala.

Sasa leo nikiona hivi vitoto vya miaka ya 90 vikijiliza liza eti vyuma vimekaza huku majumbani kwao kuna DSTV, maduka yamejaa kila aina ya bidhaa, vikienda baa vinakunywa Smirnoff, Savanna nini sijui, Hennessy V nini sijui, vinavaa nguo za madizaina [hata kama ni feki], yaani starehe mwanzo mwisho!

Nikiona hivyo huwa najiuliza sana...kama sasa hivi vyuma vimekaza...enzi zile vilikuwa vimefanya nini sasa!

Nani humu kaenda dukani akakosa Colgate, kwa mfano?

Nani hajanywa soda mwaka mzima? Nani hajanywa Fursana au Mo Orange kisa kashindwa kununua kwa sababu vyuma vimekaza?

Nani kaenda dukani kununua Rinju akakosa?

Tumekuwa watu walaini mno sisi. Watu wa kudekadeka tu.

Vyuma vilikaza miaka hiyo. Hakuna vyuma vilivyokaza miaka hii.

Acheni usleki mayai.
We fala achana na thread za kijinga
 
Sasa na wewe kumbe nyumbu tuuu!!!! Izoo enzi unazoniletea apa mi nilikuwepo!?? Mi nimezaliwa nimekuta watu wanamaisha mazur sio hayo unayoyazungumza wewe, kama wewe ulipata tabu uko nyuma usitake kufananisha na huu wakati uliopo,, ndo harakat zenu muturudishe huko kwenye miaka ya 80 huko ya kutoka dar mpaka mtwara wiki sita uko njian!!!? Toa upuuzi wako peleka kwa watoto wako uko
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Miaka ya 80 ilieleweka kwa mini na tulishatoka...history....this is 2000yrs
 
Back
Top Bottom