Vyombo vya ulinzi mmewashindwa Panya Road?

Vyombo vya ulinzi mmewashindwa Panya Road?

Dawa yao ipo sema wa Tz hatueleweki .....ikiputa operation utasikia haki za binadamu.....
 
Naona wamerudi Kwa Kasi Tena, wanapora, wanajeruhi, ni huzuni.

Jamaa yetu juzi Goba Kwa Madawa wamevamiwa mtaa mzima wamepigwa vibaya. Wameporwa pesa simu na vingine vya thamani. Wamefanyiwa ukatili, hawajali mjamzito Wala mzee wanapiga vibaya. Hili kundi walikua kama 20-30 Kwa idadi halafu mijibaba.

Kesho yake tena yani jana kundi jingine la wadogo wadogo wamevamia mtaa huko eneo linaitwa Kwa Mzungu, wamejeruhi, wamepora.

Wana silaha za jadi, marungu, mapanga, shoka, visu nk.

Wanavamia usiku wa manane, wanavunja milango watu wanaamriwa wavue nguo wanabaki Uchi huku wanapigwa vibaya.

Now haijulikani mtaa gani unafuatia
Fanyeni kikao Cha mtaa!wanaume wahusike ulinzi shirikishi!!

Kwa Sasa kama nchi na taifa kuna kipindi kigum Dana tunaenda pitia!!

Msitegemee polisi!ugum wa maisha plus ajira hamna ni tatizo kubwa !polisi wamechoka na ni kama Kuna sabotage inafanyika Kwa aliekalia kiti!!
 
Tanzania ni nchi inayoparaganyika Kwa Kasi sana.

Sijui kama utawala na siasa hizi za CCM zikidumu miaka 10 ijayo mbele na Katiba iliyopo Hali itakuawaje.

Kwa Sasa WanaCCM na watawala akiwemo Naibu waziri mkuu msimamizi Wa shughuli za Serikali anawakejeli watu wanapinga utafutaji Wa Mali Kwa njia haramu kama wanavyofanya Panya Rodi.
Sasa kama Kiongozi mkuu Wa Serikali na Waziri Wa Madini anasimama hadharani na kuwakejeli wananchi 80% kuwa ni wajinga na wana Roho mbaya na hawajui watu wanaotafuta Mali Kwa njia halali na wale wanaotafuta Kwa njia haramu .

Jambo la kukera zaidi Kutoka Kwa Naibu Waziri Mkuu ni Kuwa amejawa na dharau na kiburi na kujifanya KUWA hajui Kuwa watanzania wengi ni maskini na wanafahamu wazi Kuwa wanaowapendelea Wageni na kuwekeza mapesa Mengi yanayotokana na ufisadi ni watawala akiwemo yeye na Sio Kuwa watanzania Wanyonge wanawapenda watu kutoka nje.

Anajifanya Kuwa haoni Kuwa waliowanyanganya Wazawa Bandari na kuwapa Wageni ni yeye na Serikali yake na Sio wananchi . Hivyo wenye raho Mbaya ni watawala akiwemo yeye na Sio Wananchi ambao wakipinga kupewa Wageni .

Hoyo Naibu waziri mkuu ametoa kauli ya kejeli sana Kwa watanzania .
Kauli yake ya kejeli anajua wazi Kuwa unatokana na kiburi anachokipata Toka Kwa wale walioshika Dola na waliompa Cheo kinyume na Katiba Ili aje kuwadharau na kuwatukana wanyonge katika nchi Yao.
Hivi ni Nani aliyewanyanganya wamasai Ardhi Yao akawapa Wageni ?
Hapo nani mwenye roho mbaya Kwa watanzania Kati ya Serikali yake ya CCM na Wananchi aliposema Kuwa Wana roho mbaya na wanawapenda zaidi Wageni wafanikiwe kuliko wazawa?

Hivi mmasai mwenye n'gombe 5 unaweza ukamwita maskini Kwa sababu tu ya kujiona Bora ndani ya V8 la serikali linalonunuliwa Kwa Kodi ya Wananchi huku Hospitali zikiwa zinashindwa Hata kutoa Chanjo ya Homa ya ini.

Doto awaombe radhi watanzania na afute kauli yake inayochochea uhalifu na Wizi Wa Mali za umma na kuwafanya Wananchi waadilifu kuitwa wenye roho Mbaya.
Hivi Kama watu watakaa kimya wanapoona wajanja wanakwapua Mali za umma na kujilimbikizia Mali Nani atalinda Mali za umma.?
Yaani Kwa Sasa wanaowindwa na kukamatwa ni vidagaa na Sio mapapa . Mapapa yanachekelea pelee wakijiona wao Wana roho nzuri.

Hivi Nani mwenye roho Mbaya Kati ya Yule anayeua Ili apate madaraka au mwananchi anayewapinga Hao wauaji wanaosaka madaraka?

Hivi Kwa tafsiri ya Doto Naibu Waziri Mkuu roho Mbaya ni ipi Kati ya kukosa pesa au kuzipata Kwa kudhulumu wengine?
Mwenye roho Mbaya ni Yupi Kati ya Yule anayechukua mabilioni ya fedha za umma na kwenda Kununua magari ya kifahari Kila mwaka ilihali Wananchi wake wanalipa pesa ya chanjo ya Homa ya ini ambayo Hata Bima inagoma .?

Yaani Naibu waziri mkuu hua haoni jinsi chaguzi za Tanzania na nchi nyingi zinavyogubikwa na vitendo Vya Wizi,maiaji na Rushwa Kwa lengo la kupata madaraka Ili wapate Mali kupitia ofisi za umma ?
Sasa Kiongozi aliyepata ubunge Kwa kuua au Wizi au Rushwa na hatimaye uwaziri ni Vipi anaweza kuwaona Wananchi maskini Kuwa Wana roho Mbaya kuliko yeye aliyepata Kwa dhulma !?

Ama kweli CCM imejawa na watu wenye kiburi sana na kujiona Kuwa wao ni miungu wanafanya wanachotaka na kusema wanachotaka na kujipigia makofi .

Na Bado Kwa kauli za Sasa za kuhamasisha starehe na Matumizi makubwa na kuwakejeli wale walikosa fursa kutokana na mazingira yasiyo na usawa miongoni mwa watumishi Wa umma na Hata kwenye siasa tutegemee uhalifu Kuwa mkubwa sana . Watu watajitahidi kukwapua popote au kupora Usiku na mchana wataonekana wanakula bata kwa Raha zao na kuwasifia Matajiri Ili waonekane Kuwa Hawana roho Mbaya.

Tulitegemea Serikali iipe nguvu Tume ya maadili ya uongozi Wa umma na PCCB Ili wafuatlie na kuhoji wale watu wanaotajitika ghafla wakati Hawana biashara yenye miaka Hata miwili Ili Hali ni watumishi Wa umma na wanalalamikiwa au wmetajwa kwenye ripoti ya CAG kwenye wizara au idara wanazosimamia badala yake Naibu waziri mkuu anawakatisha tamaa Hata Tume ya maadili na PCCB mana nao ni watu wakianza kumfuatilia MTU wataonekana Wana roho Mbaya . Matokeo yake wanaacha Kila mtu ale Kwa urefu Wa kamba yake huku Wananchi wakipandishiwa Kodi na Tozo na watumishi wakiumizwa na Kikokotoo badala ya kupewa pesa zao Ili nao wawe Matajiri wananyanganywa na kiinuamgongo chao wakilalamika wanaambiwa Wana roho Mbaya.
Sijui Nani mwenye roho Mbaya Kati ya Serikali yake ya CCM iliyoweka Sheria ya kikokotoo Ili watumishi Wa umma wastaafu na kubaki na malalamiko ya kiinua mgongo chao kuchukuliwa Ili Wachache wenye madaraka wakanunue magari ya kifahari na kufanya vikao na makongamano na kulipa posho za safari Kila Siku huku jasho halali la wastaafu likiishia kwenye kikokotoo na Wananchi wakilalamika Naibu waziri mkuu anawakejeli KUWA Wana roho Mbaya. Anasahau KUWA walipitisha ni wabunge na Serikali Yao inayoongozwa na wazawa na Sio Wageni kutoka Ulaya.

Naibu waziri ajifunze Kwa Paulo Makonda au Polepole au Bashiru Ali au Au Hata Kwa Sipriani Musiba .
Hawa ni Watu waliofanikiwa wakiwa ndani ya Serikali lakini hawajawahi kujitoa ufahamu na kuwakejeli watanzania kujifanya kuwa kuna watu wanajipatia utajiri Kwa dhulma na kukwepa Kodi . Hawa muda Wote wanaonekana kuwa upande Wa wananchi na kukemea vitendo Vya Wizi Wa Mali za umma na kuonyesha kukerwa na watu wanaokwapua Mali za umma Kwa lengo la kujitajirisha.

Paulo Makonda na Hamfrei Polepole wanazidi kuwa mashujaa Kwa sababu wanasimamia kile wanachokiamini pamoja na kupewa madaraka makubwa ndani na nje ya chama .

Tatizo la Panya Rodi linatokana na Tamaa za kutaka Mali Kwa njia ya short cut na Ili wasionekane kuwa Wana roho Mbaya ni Lazima wawe na pesa na MTU akiwakemea Panya Rodi na pesa wanazozipata ataambiwa Ana roho Mbaya.
Polisi nao wanatafuta pesa Kwa Udi na uvumba Ili wasije wakajikuta wanaangukia kwenye kundi la watu wenye roho Mbaya.

NB:
Hivi Kama kuna MTU anatoa mpaka Katara Watoto wake na mama yake Ili awe Tajiri ,unawezaje kusema kuwa ana roho nzuri Kwa sababu tu Ana pesa . Yaani pesa imemtakasa na kumfanya mtakatifu.
Kejeli ya Naibu waziri mkuu ni Hatari sana kwenye nyakati hizi za watu kupenda fedha kuliko vitu vyote.
Mkuu umeandika kwa uchungu sana 😭😭😭
 
Fanyeni kikao Cha mtaa!wanaume wahusike ulinzi shirikishi!!

Kwa Sasa kama nchi na taifa kuna kipindi kigum Dana tunaenda pitia!!

Msitegemee polisi!ugum wa maisha plus ajira hamna ni tatizo kubwa !polisi wamechoka na ni kama Kuna sabotage inafanyika Kwa aliekalia kiti!!
Kwa lifestyle ya wakazi wa dar..ni ngumu.wengi hawashirikiani labda maeneo ya mitaa mikongwe
 
Tanzania ni nchi inayoparaganyika Kwa Kasi sana.

Sijui kama utawala na siasa hizi za CCM zikidumu miaka 10 ijayo mbele na Katiba iliyopo Hali itakuawaje.

Kwa Sasa WanaCCM na watawala akiwemo Naibu waziri mkuu msimamizi Wa shughuli za Serikali anawakejeli watu wanapinga utafutaji Wa Mali Kwa njia haramu kama wanavyofanya Panya Rodi.
Sasa kama Kiongozi mkuu Wa Serikali na Waziri Wa Madini anasimama hadharani na kuwakejeli wananchi 80% kuwa ni wajinga na wana Roho mbaya na hawajui watu wanaotafuta Mali Kwa njia halali na wale wanaotafuta Kwa njia haramu .

Jambo la kukera zaidi Kutoka Kwa Naibu Waziri Mkuu ni Kuwa amejawa na dharau na kiburi na kujifanya KUWA hajui Kuwa watanzania wengi ni maskini na wanafahamu wazi Kuwa wanaowapendelea Wageni na kuwekeza mapesa Mengi yanayotokana na ufisadi ni watawala akiwemo yeye na Sio Kuwa watanzania Wanyonge wanawapenda watu kutoka nje.

Anajifanya Kuwa haoni Kuwa waliowanyanganya Wazawa Bandari na kuwapa Wageni ni yeye na Serikali yake na Sio wananchi . Hivyo wenye raho Mbaya ni watawala akiwemo yeye na Sio Wananchi ambao wakipinga kupewa Wageni .

Hoyo Naibu waziri mkuu ametoa kauli ya kejeli sana Kwa watanzania .
Kauli yake ya kejeli anajua wazi Kuwa unatokana na kiburi anachokipata Toka Kwa wale walioshika Dola na waliompa Cheo kinyume na Katiba Ili aje kuwadharau na kuwatukana wanyonge katika nchi Yao.
Hivi ni Nani aliyewanyanganya wamasai Ardhi Yao akawapa Wageni ?
Hapo nani mwenye roho mbaya Kwa watanzania Kati ya Serikali yake ya CCM na Wananchi aliposema Kuwa Wana roho mbaya na wanawapenda zaidi Wageni wafanikiwe kuliko wazawa?

Hivi mmasai mwenye n'gombe 5 unaweza ukamwita maskini Kwa sababu tu ya kujiona Bora ndani ya V8 la serikali linalonunuliwa Kwa Kodi ya Wananchi huku Hospitali zikiwa zinashindwa Hata kutoa Chanjo ya Homa ya ini.

Doto awaombe radhi watanzania na afute kauli yake inayochochea uhalifu na Wizi Wa Mali za umma na kuwafanya Wananchi waadilifu kuitwa wenye roho Mbaya.
Hivi Kama watu watakaa kimya wanapoona wajanja wanakwapua Mali za umma na kujilimbikizia Mali Nani atalinda Mali za umma.?
Yaani Kwa Sasa wanaowindwa na kukamatwa ni vidagaa na Sio mapapa . Mapapa yanachekelea pelee wakijiona wao Wana roho nzuri.

Hivi Nani mwenye roho Mbaya Kati ya Yule anayeua Ili apate madaraka au mwananchi anayewapinga Hao wauaji wanaosaka madaraka?

Hivi Kwa tafsiri ya Doto Naibu Waziri Mkuu roho Mbaya ni ipi Kati ya kukosa pesa au kuzipata Kwa kudhulumu wengine?
Mwenye roho Mbaya ni Yupi Kati ya Yule anayechukua mabilioni ya fedha za umma na kwenda Kununua magari ya kifahari Kila mwaka ilihali Wananchi wake wanalipa pesa ya chanjo ya Homa ya ini ambayo Hata Bima inagoma .?

Yaani Naibu waziri mkuu hua haoni jinsi chaguzi za Tanzania na nchi nyingi zinavyogubikwa na vitendo Vya Wizi,maiaji na Rushwa Kwa lengo la kupata madaraka Ili wapate Mali kupitia ofisi za umma ?
Sasa Kiongozi aliyepata ubunge Kwa kuua au Wizi au Rushwa na hatimaye uwaziri ni Vipi anaweza kuwaona Wananchi maskini Kuwa Wana roho Mbaya kuliko yeye aliyepata Kwa dhulma !?

Ama kweli CCM imejawa na watu wenye kiburi sana na kujiona Kuwa wao ni miungu wanafanya wanachotaka na kusema wanachotaka na kujipigia makofi .

Na Bado Kwa kauli za Sasa za kuhamasisha starehe na Matumizi makubwa na kuwakejeli wale walikosa fursa kutokana na mazingira yasiyo na usawa miongoni mwa watumishi Wa umma na Hata kwenye siasa tutegemee uhalifu Kuwa mkubwa sana . Watu watajitahidi kukwapua popote au kupora Usiku na mchana wataonekana wanakula bata kwa Raha zao na kuwasifia Matajiri Ili waonekane Kuwa Hawana roho Mbaya.

Tulitegemea Serikali iipe nguvu Tume ya maadili ya uongozi Wa umma na PCCB Ili wafuatlie na kuhoji wale watu wanaotajitika ghafla wakati Hawana biashara yenye miaka Hata miwili Ili Hali ni watumishi Wa umma na wanalalamikiwa au wmetajwa kwenye ripoti ya CAG kwenye wizara au idara wanazosimamia badala yake Naibu waziri mkuu anawakatisha tamaa Hata Tume ya maadili na PCCB mana nao ni watu wakianza kumfuatilia MTU wataonekana Wana roho Mbaya . Matokeo yake wanaacha Kila mtu ale Kwa urefu Wa kamba yake huku Wananchi wakipandishiwa Kodi na Tozo na watumishi wakiumizwa na Kikokotoo badala ya kupewa pesa zao Ili nao wawe Matajiri wananyanganywa na kiinuamgongo chao wakilalamika wanaambiwa Wana roho Mbaya.
Sijui Nani mwenye roho Mbaya Kati ya Serikali yake ya CCM iliyoweka Sheria ya kikokotoo Ili watumishi Wa umma wastaafu na kubaki na malalamiko ya kiinua mgongo chao kuchukuliwa Ili Wachache wenye madaraka wakanunue magari ya kifahari na kufanya vikao na makongamano na kulipa posho za safari Kila Siku huku jasho halali la wastaafu likiishia kwenye kikokotoo na Wananchi wakilalamika Naibu waziri mkuu anawakejeli KUWA Wana roho Mbaya. Anasahau KUWA walipitisha ni wabunge na Serikali Yao inayoongozwa na wazawa na Sio Wageni kutoka Ulaya.

Naibu waziri ajifunze Kwa Paulo Makonda au Polepole au Bashiru Ali au Au Hata Kwa Sipriani Musiba .
Hawa ni Watu waliofanikiwa wakiwa ndani ya Serikali lakini hawajawahi kujitoa ufahamu na kuwakejeli watanzania kujifanya kuwa kuna watu wanajipatia utajiri Kwa dhulma na kukwepa Kodi . Hawa muda Wote wanaonekana kuwa upande Wa wananchi na kukemea vitendo Vya Wizi Wa Mali za umma na kuonyesha kukerwa na watu wanaokwapua Mali za umma Kwa lengo la kujitajirisha.

Paulo Makonda na Hamfrei Polepole wanazidi kuwa mashujaa Kwa sababu wanasimamia kile wanachokiamini pamoja na kupewa madaraka makubwa ndani na nje ya chama .

Tatizo la Panya Rodi linatokana na Tamaa za kutaka Mali Kwa njia ya short cut na Ili wasionekane kuwa Wana roho Mbaya ni Lazima wawe na pesa na MTU akiwakemea Panya Rodi na pesa wanazozipata ataambiwa Ana roho Mbaya.
Polisi nao wanatafuta pesa Kwa Udi na uvumba Ili wasije wakajikuta wanaangukia kwenye kundi la watu wenye roho Mbaya.

NB:
Hivi Kama kuna MTU anatoa mpaka Katara Watoto wake na mama yake Ili awe Tajiri ,unawezaje kusema kuwa ana roho nzuri Kwa sababu tu Ana pesa . Yaani pesa imemtakasa na kumfanya mtakatifu.
Kejeli ya Naibu waziri mkuu ni Hatari sana kwenye nyakati hizi za watu kupenda fedha kuliko vitu vyote.
HuYo anaandaliwa kushika stronghold mkuu!!

Ni swala la Muda tu!!
 
WE naye kilaza. Kaz gani nzuri wamefanya wakalaumiwa? Kazi ya kwenda na bunduk kuvamia nightclub kusaka wadada poa ndio kazi unayoeleza hapa. Ficha ujinga. Kama sio askari wewe basi ni chawa wa askari unaishi kwa huruma hapo sebuleni kwa mume wa dada yk askari
Kilaza mama yako
 
Nadhani polisi walikuwa wameanza kuwadhibiti hao Panya Road kelele zikawa nyingi wakaacha. Wananchi wakishapata joto watawaachia polisi wafanye kazi yao.
Hilo ndo namaanisha pia.Polisi wakianza kazi wanaolaumu ni wananchi.
Polisi wanawajua wapumbavu wote ila ushahidi na sheria zetu ndo tatizo
 
Wakishikwa watu wa haki za binadamu watakuja juu..

Hao ni kupiga chuma ,weka kweny kiroba maneno coco beach ..

Hao jamaa wamelanduka yaani bangi kabisa full roho mbaya.
 
Hii nchi usalama wako upo mikononi mwako mwenyewe. Nawakumbusha tutumie sheria ya "self defense" ipasavyo.

Mimi mtu yoyote anayehatarisha uhai wangu akijaa kwenye 18 ndugu zake wataenda kumtoa kwenye jokofu.
 
Vibali vitolewe watu wamiliki kitu ya bunduki , hii ya kutegemea majambazi waliovaa nguo za polisi wawe walinzi wa amani mtaani ,wakati wao wenyewe ni vibaka na majambazi kama hao panya road ni uzoba
Kila mtu akiwa na mtutu ,heshima itakuwepo .
Huu upumbavu utaisha , ukivamia kwangu nakumwaga ubongo tu
 
Ccm haitaki watu wamiliki silaha za moto waendelee kuwa slaves na submissive WA mfumo wa ukandamizaji kama misukule
Ujinga
 
Dawa yao ipo sema wa Tz hatueleweki .....ikiputa operation utasikia haki za binadamu.....
Hamna cha operation ,hizo zuga tu na maigizo kupata political mileage na wala tatizo haliishi .
Watu raia wema wafanyiwe background checks , waruhusiwe kumiliki bastola na bunduki kwa ajili ya self defense ,pia ulinzi shirikishi ,hii programu iwezeswe ipasavyo ,mfano patrol za sungusungu usiku ,
 
Back
Top Bottom