Vyombo vya Habari vinamdhulumu Dr. Shika

Vyombo vya Habari vinamdhulumu Dr. Shika

Pamoja na Hayo Mkuu, Wabongo tumezidi Sana,kaishu kadogo tu, yaani tunajadili Karne nzima, kila kukicha ni hicho hicho, Wakati kuna watu ktk jamii yetu wana matatizo lukuki, km vile Ukosefu wa maji, Umeme, Barabara, Huduma za Afya, Masoko kwa mazao ya kilimo, n. K. Sasa kwanini tupoteze muda kujadili ishu zisizo na faida?. Tubadilike.
Matatizo yote hayo yameletwa na CCM na siyo Dr Shika
 
Sasa nawe kwanini unaleta habari zake hapa kama hutaki?
Sio kwamba sizitaki, isipokuwa Wabongo tumezidi mno, yaani Kila siku ni Shika, mbona hatujadili juu ya Akina mama wanaokufa kutokana na kukosa huduma Bora za Afya?.
 
Yaani huyu jamaa, tokea ashindwe Kukamilisha malipo kwenye ule Mnada wa Nyumba za Lugumi, yaani sasa hivi kila kukicha ni Dr. Shika tu, Ukigeuka kushoto ni Shika,nenda kulia ni Shika, Angalia Kusini Ni Shika,nenda kaskazini ni Shika,. Mashariki, Magharibi ni Shika, looh!!, Tushachoka Fanyeni mambo mengine ya Msingi, mbona kuna Mambo mengi tu ya msingi na Sekondari!!, Kuna Changamoto nyingi Jamani ktk Jamii valieni njuga Hayo.
Ww ndio unamfikilia huyo mzee....nani ana muda nae
 
Watanzania tunaishi kwa matukio. Anzisha jipya tuhamie. Ni dalili ya kukosa ya msingi yakufanya. It's very serious.
 
Ni dalili ya jamii iliyokosa matumaini katika mambo ya msingi.

Inatafuta vitu vya kuji distract.

Mara Babu wa Kikombe. Mara Dr. Shika. Na huyu akipita kitatafutwa kingine cha kuji distract tu.

Jamii yetu imekuwa kama mhanga wa madawa ya kulevya, bila ya kupata dozi mhanga hajisikii kuwa sawa.
Hongera mkuu
 
Pamoja na Hayo Mkuu, Wabongo tumezidi Sana,kaishu kadogo tu, yaani tunajadili Karne nzima, kila kukicha ni hicho hicho, Wakati kuna watu ktk jamii yetu wana matatizo lukuki, km vile Ukosefu wa maji, Umeme, Barabara, Huduma za Afya, Masoko kwa mazao ya kilimo, n. K. Sasa kwanini tupoteze muda kujadili ishu zisizo na faida?. Tubadilike.
Yote hayo watu washajadili sana na hawaoni chochote kubadilika.

Wamesoma na hawana kazi.

Watu wanaona bora wajidunge tu sindano za madawa ya kulevya ya mijadala ya Dr. Shika.

Ndiyo maana wengine ukiisema vibaya mijadala hii utakosana nao.

Kwa sababu ni kama umkute mteja anatumia madawa yake ya kulevya halafu uanze kumsomea risala kuhusu ubaya wa madawa ya kulevya.

Atakutukana na kukwambia unamkatia stimu zake.
 
Back
Top Bottom