Vyombo vya habari haviutendei haki UKAWA

Vyombo vya habari haviutendei haki UKAWA

Usilalamike sana, oo media sijui nini!!! Majibu unayo, Lowasa hafai …………

Eti watu waache kuandika kuhusu mambo ya msingi na watu wa maana waanze kuandika wauza unga na Saccos yao
 
Mkuu umenena vyema ila ninachoona mimi tutumie ule msemo usemao ''kuteleza si kuanguka bali ni kusonga mbele"
namaanisha hivi pale media zinapousema vibaya UKAWA sisi tuelewe kuwa wameshikwa pabaya
tuendeleze msimamo wetu,tusitegemee jema kutoka kwa waandishi waliowengi wanaotegemea
kutunukiwa ukuu wa wilaya,Hapa ni kujishughulisha wenyewe kutafuta habari,hata pale ambapo
tutalazimika kusikiliza vyombo vya habari tuwe na msimamo mioyoni mwetu
kwani kile alichokisema mwenyekiti wa wazazi wa ninyim kimenifungua macho
kwamba kumbe hii ni vita sawa na ile iliyomng'oa mkoloni.

Watu wasivunjwe moyo na kinachosemwa,tusitegemee kuletewa
mabadiliko na media tujiandae kujiletea mabadiliko wenyewe
maana wanahabari walipotaka kuleta mabadiliko mwenzao
Mwangosi aliuawa ila kwa sasa wameishasahau
hivyo si watu wa kutegemea sana,tujiletee wenyewe mabadiliko.

mkuu sio wote wenye upeo kama wa kwako. wengi tu huwa wanashawishika na wakionacho kuliko kutegemea mbongo zao kufanya maamuzi. la msingi ni ukawa nao kudindisha hadi huyo kigori aone haya
 
Si ndiyo ukweli wenyewe huo,au mnataka vyombo vya habari viandike hata yale ambayo hayapo
 
Tangu majuzi nafuatilia media za hapa nchini, iwe televisheni au magazeti. Habari zilizotamalaki ni za CCM zaidi kwa upande wa chanya. Kwamba ccm wametoa ahadi hizi, Magufuli awakosha wananchi wa sehemu fulani, wanaccm wafurika mikutano ya Magufuli, Pinda sijui kafanya nini, n.k. Alimradi tu habari njema za ccm zinatamalaki.

Kwa upande wa pili unasikia NCCR wajitoa UKAWA, wanachadema wakamatwa Bukoba kwa maandamano, fujo zatawala mikutano ya UKAWA, Lowassa kabanwa, n.k.

SAsa kiukweli kwa wanaofuatilia vyombo vya habari tu wanapotoka mno! Hivi vyombo vinaipendelea sana ccm na serikali yake. Tafadhali UKAWA, hizi propaganda za media kweli itafika hatua zitawachafua. Hamna jema linalozungumziwa la UKAWA zaidi ya kulikuta kwenye gazeti la Tanzania DAima. Lifanyike jambo tafadhali. Media haiko upande wa mabadiliko. Yafanyieni kazi haya.

mkuu, acha kutazama TBCCM~~huwa hawatangazi mafanikio ya UKAWA au udhaifu wa CCM hata siku moja.
 
mkuu sio wote wenye upeo kama wa kwako. wengi tu huwa wanashawishika na wakionacho kuliko kutegemea mbongo zao kufanya maamuzi. la msingi ni ukawa nao kudindisha hadi huyo kigori aone haya
Ni kweli mkuu,ushauri wako uzingatiwe.
 
mkuu, acha kutazama TBCCM~~huwa hawatangazi mafanikio ya UKAWA au udhaifu wa CCM hata siku moja.
Tatizo hawafikirii mbele, tena keshokutwa tu hali itakuwaje. Ila bahati mbaya na wao wamekaliwa kooni
 
Ukawa kikundi haramu ndo kiandikwe ili iweje? tuache kuandika vyama waanze kuandika habari za makundi ya kigaidi, ukawa siyo chama cha siasa ..ni Saccos ya mbowe

Eti watu waache kuandika kuhusu mambo ya msingi na watu wa maana waanze kuandika wauza unga na Saccos yao
Mara kundi haram, mara wauza unga... Angalia tutahitaji uthibitisho toka kwako.
 
Asanteni media, hasa kwa magazeti ya leo, hasa Nipashe, Mwananchi, Raia mwema na Tanzania Daima. Naona kilio chetu kinasikika sasa
 
Back
Top Bottom