Vyombo vya habari haviutendei haki UKAWA

Vyombo vya habari haviutendei haki UKAWA

sasa kama nyie mnavinjio hata sisi tunavo na zaidi sisi tunawachinjaji wenyewe sio wa kukodi...politics ni propaganda kutumia slogan zenu ni propaganda kuwachanganya tu...

Haohao wa kukodi wanajua wanajua mnachinjikaje. Kila siku nanyi si mnatafuta mamluki kwenye upinzani? mbinu za kupata mamluki zinawashinda na sasa mmevamia slogan. pamoja na kwamba nalalamika media hazitutendei haki, nashukuru watu kama magufuli na timu yake wanainadi ukawa, japo hamtachomoka kwani mna kesi ya kujibu
 
Kitu usichokujua ni sawa na usiku wa giza, ukiwa muda wote unafikiria UKAWA atimaye utakua chizi, asilimia kubwa ya magazeti yapo chini ya ukawa, ns ndo maana ubovu wa mgombea wa ukawa hausemwi sana kwenye magazeti, sitegemei mtu kamaKubenea leo amseme vibsya Lowasa, lakini wakati ule ulimtolea maneno mengi sana, lakini pia kwa pesa aliyonayo mgombea wa ukawa anaweza kufanya live mikutano yake mingi, ww unalalamika wao wanajisikia freshi kabisa, kwani wakifanya live mtaipata aibu yenu, huwezi kufanya live wakati unaongea dk3 muda mwingine huwezi hata kuongea. Kwa hiyo kwao ni jambo jema, ili watz wengi wasifuatilie sana, ila kwa ww ambae hujui ndo unauzunika. POLE SANA!

unaweza ukawa uko sahihi ila haimaanishi naafikiana na wewe. kila jambo lina namna yake ya kufanya. Sio lazima hata hivyo mikutano iwe live kama pana tatizo sehemu. wakati mwingine hata hizo dk tano zinatosha sana kwani haongei peke yake. si tunaona ya magufuli? si tunaona anavyochemka? si tunaona snavyoishiwa na hoja majukwaani? si tunaona anavyotoa vitisho? unakuta kamaliza kuongea ya msingi na matokeo yake anavyoendelea ndio tunachokishuhudia.

nia hapa si kuona mikutano live kwenye tv bali habari (ikiwezekana sema propaganda) zinazoubeba ukawa pamoja na vibwagizo vya hapa na pale. tunajua ccm wanashambulia kila kona na wanashambulia vibaya na wakati mwingine wanapatia. ukawa wanashambuliaje kupitia media?
 
ACT ndo hatuandikwi kabisa iwe kwa mabaya au mazuri
 
Nimecheka sn jana kuona takwimu za eafuasi wa wagombea facebook
Makufuli wafuasi 7,000
Lowasa WAFUASI 254,000 MAFURIKO
 
Kitu usichokujua ni sawa na usiku wa giza, ukiwa muda wote unafikiria UKAWA atimaye utakua chizi, asilimia kubwa ya magazeti yapo chini ya ukawa, ns ndo maana ubovu wa mgombea wa ukawa hausemwi sana kwenye magazeti, sitegemei mtu kamaKubenea leo amseme vibsya Lowasa, lakini wakati ule ulimtolea maneno mengi sana, lakini pia kwa pesa aliyonayo mgombea wa ukawa anaweza kufanya live mikutano yake mingi, ww unalalamika wao wanajisikia freshi kabisa, kwani wakifanya live mtaipata aibu yenu, huwezi kufanya live wakati unaongea dk3 muda mwingine huwezi hata kuongea. Kwa hiyo kwao ni jambo jema, ili watz wengi wasifuatilie sana, ila kwa ww ambae hujui ndo unauzunika. POLE SANA!

Miaka 54 viongozi yote viongozi wa ccm wamekuwa wakiongea sana masaa kibao hotuba ndefu maneno matamu na ahadi nyingi zisizotekelezeka, watanzania wa sasa hawataki mbwembwe za maneno kwenye mikutano hata Kama mgombea anazungumza dakika moja tu inatosha kumwelewa maana sasa ni mda wa mabadiliko kwa vitendo wananchi wamechoka na maneno mengi pasipo Vitendo.
 
ACT ndo hatuandikwi kabisa iwe kwa mabaya au mazuri

ACT ni chama cha wanafiki hakuna mwenye time nacho waendelee kujikongoja tu labda wataweza kuambilia mbunge hata mmoja kwa mbinde.
 
ACT ni chama cha wanafiki hakuna mwenye time nacho waendelee kujikongoja tu labda wataweza kuambilia mbunge hata mmoja kwa mbinde.

Haya matusi hayafai.
Tukianza kuwapa Ukawa na CCM matusi yao patakuwa hapatoshi
 
Tangu majuzi nafuatilia media za hapa nchini, iwe televisheni au magazeti. Habari zilizotamalaki ni za CCM zaidi kwa upande wa chanya. Kwamba ccm wametoa ahadi hizi, Magufuli awakosha wananchi wa sehemu fulani, wanaccm wafurika mikutano ya Magufuli, Pinda sijui kafanya nini, n.k. Alimradi tu habari njema za ccm zinatamalaki.

Kwa upande wa pili unasikia NCCR wajitoa UKAWA, wanachadema wakamatwa Bukoba kwa maandamano, fujo zatawala mikutano ya UKAWA, Lowassa kabanwa, n.k.

SAsa kiukweli kwa wanaofuatilia vyombo vya habari tu wanapotoka mno! Hivi vyombo vinaipendelea sana ccm na serikali yake. Tafadhali UKAWA, hizi propaganda za media kweli itafika hatua zitawachafua. Hamna jema linalozungumziwa la UKAWA zaidi ya kulikuta kwenye gazeti la Tanzania DAima. Lifanyike jambo tafadhali. Media haiko upande wa mabadiliko. Yafanyieni kazi haya.

kama mlipa kodi katika nchi hii, tatizo langu kubwa ni vyombo vya habari vya umma - yaani TBC, Habarileo na Daily News.

badala ya kunung'unika ndani ya blanketi, hivi ni kwa nini UKAWA wasipeleke official complaint kwenye tume na pia kutawanya waraka kwa vyombo na taasisi za kimataifa (EU, etc) kuhusu hii democratic infringement?

hivi vitu ni muhimu viwekwe kwenye kumbukumbu just in case involvement ya ICC itatakiwa beyond 25 Oktoba.

UKAWA lifanyieni kazi hili haraka sana (I mean kama bado) kwani mwezi ujao (Oktoba) mara nyingi ndiyo huwaga kuna faulo nyingi kutoka chama tawala.
 
kama mlipa kodi katika nchi hii, tatizo langu kubwa ni vyombo vya habari vya umma - yaani TBC, Habarileo na Daily News.

badala ya kunung'unika ndani ya blanketi, hivi ni kwa nini UKAWA wasipeleke official complaint kwenye tume na pia kutawanya waraka kwa vyombo na taasisi za kimataifa (EU, etc) kuhusu hii democratic infringement?

hivi vitu ni muhimu viwekwe kwenye kumbukumbu just in case involvement ya ICC itatakiwa beyond 25 Oktoba.

UKAWA lifanyieni kazi hili haraka sana (I mean kama bado) kwani mwezi ujao (Oktoba) mara nyingi ndiyo huwaga kuna faulo nyingi kutoka chama tawala.

sawa kabisa. chombo cha umma kwa manufaa ya umma na si genge fulani. pamoja na ukweli kwamba malalamiko yao yanaweza yasitekelezwe na mfumo uliopo, inatosha tu kuwa na kumbukumbu za matukio kwa matumizi ya baadae ya kudai haki iliyoporwa.
 
act ndo hatuandikwi kabisa iwe kwa mabaya au mazuri

act-wz iandikwe na nani na kwa lipi. Hivi hujui kuwa karibu tv zote na magazeti yote ama yamenunuliwa ama yanaupendeleo na kujikomba kwa wale wanaodhani watashinda urais ili wakumbukwe.
 
Ukweli ni kwamba ccm wanashambulia mno na kwa rafu zote. Hatimaye wakifika golini na kwa rafu hizo ndio unakuta na goli la mkono linapatikana hapo. Siwasifu ccm kwa lolote ila nawatahadharisha tu wanabamadiliko. Kama usemavyo, wakitegemea mafuriko watayaona kweli.

Umetolewa ushauri wa kila aina kwenye mitandao lakini hawashiki hata moja na asiyesikia la mkuu huvunjika guu; watasema mafuriko ya Mrema na sasa ni tofauti ila hawajui kuna mafuriko makubwa zaidi hayaji viwanjani yanafatilia mambo kupitia vyombo vya habari. Wasubiri kulia kilia kikuu
 
Mkuu umenena vyema ila ninachoona mimi tutumie ule msemo usemao ''kuteleza si kuanguka bali ni kusonga mbele"
namaanisha hivi pale media zinapousema vibaya UKAWA sisi tuelewe kuwa wameshikwa pabaya
tuendeleze msimamo wetu,tusitegemee jema kutoka kwa waandishi waliowengi wanaotegemea
kutunukiwa ukuu wa wilaya,Hapa ni kujishughulisha wenyewe kutafuta habari,hata pale ambapo
tutalazimika kusikiliza vyombo vya habari tuwe na msimamo mioyoni mwetu
kwani kile alichokisema mwenyekiti wa wazazi wa ninyim kimenifungua macho
kwamba kumbe hii ni vita sawa na ile iliyomng'oa mkoloni.

Watu wasivunjwe moyo na kinachosemwa,tusitegemee kuletewa
mabadiliko na media tujiandae kujiletea mabadiliko wenyewe
maana wanahabari walipotaka kuleta mabadiliko mwenzao
Mwangosi aliuawa ila kwa sasa wameishasahau
hivyo si watu wa kutegemea sana,tujiletee wenyewe mabadiliko.
 
ACT ndo hatuandikwi kabisa iwe kwa mabaya au mazuri
ACT mlishaandikwa kwenye biblia,
kasome habari za Yuda aliyemsaliti Yesu kwenye injili ya Luka,pamoja na mambo
mazuri aliyotendewa bado alimsaliti.

Hawa waandishi wa bongo hata wasipowaandika haina madhara maana
tayari mpo kwenye kitabu kitakatifu.
 
ACT mlishaandikwa kwenye biblia,
kasome habari za Yuda aliyemsaliti Yesu kwenye injili ya Luka,pamoja na mambo
mazuri aliyotendewa bado alimsaliti.

Hawa waandishi wa bongo hata wasipowaandika haina madhara maana
tayari mpo kwenye kitabu kitakatifu.

Mnatumai mazigazi mkiyafikia hamtakuta maji.......tafakari
 
Ukawa kikundi haramu ndo kiandikwe ili iweje? tuache kuandika vyama waanze kuandika habari za makundi ya kigaidi, ukawa siyo chama cha siasa ..ni Saccos ya mbowe
 
Back
Top Bottom