Hiki ndiyo kizazi cha 3 cha VW touareg, cha kwanza kilikuwa 2002, cha pili kuanzia 2010 na sasa 3.
ukiangalia wameboresha sana hasa kiteknolojia!
Siyo tu Matairi ya mbele bali hata
matairi ya nyuma pia
hukata kona!
Sound system ya ukweli 7.1 dolby surround, kuna
speaker 14 gari nzima!
A.C kila mtu
anachagua nyuzi joto anayotaka, yaani kama dereva anataka nyuzi joto 20 atapata na abiria anataka 21 vyote vinawezekan kwa wakati mmoja, yaani kila mtu anapata ubaridi wake kwa wakati mmoja!
Kufungua buti hauhitaji kuligusa bali kuna
sensor ukiweka mguu tu chini buti linafungunguka lenyewe hivyo
huhitaji kutua mzigo chini na kufungua buti.
Enzi za kubamiza mlango ili ufunge vizuri zimekwisha na sasa kidogo ukivuta mlango unajifunga wenyewe kabisa!
3 liter, 286 HP!