Vurugu Umbwe-Lyamungo: Miaka 12 baadae

ah sio poa, mama sasa alivyokua analia, dogo alikua anaitwa Ayubu, mama aliletwa na defender ya magereza Karanga, gari lipo speed imewasha taa, ametua tuu pale mama ni mayowe, "uuwih mwanangu Ayubu, mbona wenzako waliweza kukimbia, tuseme wewe ndo ulishindwa kukimbia kati ya hawa wote?" hapo tupo Parade tunamsikiliza RPC na mkuu wa wilaya, huku ugeni wa waziri wa elimu ukiwa njiani.
.
.
aisee na ubishi wangu mimi na wa jamaa mmoja hivi kiranja wa ulinzi, tulilia!! yaan tulijiona na hatia, maneno yale yameshindwa kutoka kichwani miaka 12 sasa, hizi ni story tuu, ila ungetazama tukio ungeshangaa, hizi roho madogo wametolea wapi,
.
.
asubuhi watu wamefunga mashati kama kundi la kigaidi la alqaeda, wanasalimiana kwa lugha za Code kama majasusi, saa kumi usiku kibosho na zile kahawa ni giza, tunakutana na kina mama wa kibosho wanatulilia, jamani wanangu rudini, mmezaliwa na wanawake kama sisi, msiende! hakuna anaelewa!!
mlikatazwa kwenda baada ya kifo cha ayubu au kabla ya ayubu kufariki poleni it was sad indeed
 
Sasa ukweli si ndo huo mkuu mbona kama umepaniki? Pia kuna washkaji kibao waliumia nashukuru Mungu sikupata hata jeraha. Kuna marafiki zangu kibao wana makovu mpaka leo. Na je? Wewe uliona ni sahihi kuja shuleni kufanya fujo? Nadhani uliona maamuzi yaliyotolewa. Nyie mlilipa faini ya uharibifu tsh.53,000/= sisi hatukulipa hata mia.

Sent using Jamii Forums mobile app
kaka haya ndo yaliyosababisha vurugu zile, kusoma hizi shule ni kama kupigwa muhuri wa moto, taarifa fake, kwa vizazi vinavyobaki halafu hata viongoz wa shule hawasemi, ndo maana nasema labda vile vita vya umachame na ukibosho unahusika,,, mimi nilikua kiongoz pale hatukuchangishwa fedha zozote, taarifa zilikua zinatolewa hivyo kama kuwatuliza tuu na kuona kuna adhabu, hata sisi tuliambiwa nyie kuna fedha mmetoa na tuliambiwa hayo tukiwa kwenye kikao cha serikali ya shule na walimu..
.
.
heb niambie madogo kule na zile mori waambiwe aidha last revenge lyamungo walipigwa, au last revenge umbwe walipigwa, ndo maana hizi fujo haziishi,
 
Na hapo form four ya Umbwe ya 2009 wahuni kibao walifukuzwa 2008, sipati picha wakina Baghdad wangekuwepo

Kuna kipindi kilikuwa na bifu na wanakijiji ukikutwa kombo au maeneo yeyote ya kijijini usipochezea mabapa basi utaibiwa kwa lazima, ilifikia wanakijiji wanaingia maeneo ya shule usiku kama uwanjani wakikuta lazima wakuibie

Kilichokua kinaharibu Umbwe na lyamungo ni watoto wa Arusha wengi wao ndo walikua wakorofi, na usela mavi
ni kweli, kwa umbwe ni zile bangi za Arusha, kuna jamaa alikua na beto kama jambazi, zile za kubonyeza ina fyatuka, mshkaji akitoka prepo usiku anaitoa alafu anaifyatua, fyaah!
.
.
ila lyamungo ni ukurya na mr. wandiba, kwakweli, kwenye vikao vya shule mzee yule kama vile alikua anaenjoy zile, ila lyimo walau alikua anatimua timua,
 


Nimekuwa nikisikiliza hii track ya dre na snoop na nate dogg - lil ghetto boy, na mara nyingi huwa na refference ile ishu na hii nyimbo.

Coz mara nyingi tunafanya decisions mbaya za maisha tukiwa vijana wadogo ila baadae zile decisions zinakuja kutu-haunt ukubwani.

Kama mimi naumia kutokana na ile vurugu na maafa ,Hivi unadhania je wale waliohusika na kuwashambulia wale marehemu hadi mauti, kwa sasa wana remorse ya aina gani.

"Whatchu gonna do when you grow up, have to face responsibilities"

Mkuu respect una feelings sana.
Mpaka una sound track ya hizi memories.
Dah...
 
Nafikiri Songea boys ndo wamepigana Vita na wapinzani wengi zaidi.
Moja kulikua na Vita ya hatari Kati ya Songea boys na Chuo cha Ualimu Songea(Matogoro) kwenye historian Vita hii ilishawahi ua mtu, wanachuo walikua wanapigika vibaya Sana

Pili, kulikua na Vita Kati ya Songea boys na Shule ya sekondari(ya jeshi) Ruhuwiko: Vita hii ulikua inaanzia Uwanja wa Majimaji then inasambaa mtaani. Ruhuwiko walikua wanaumia Sana kwenye mapigano haya
Songea boys ulikua ni zaidi ya Jeshi
Ha ha ha Vita ya Box 2 na Ruhuwiko ilikua mbaya maana jamaa walikua mpka wanasaidiwa na walimu wao wanajeshi...

Ilikua kikinuka ile njia ya kwenda Tunduru usikatishe maana Boys wanajaa njia yote....
 
Nyuzi kama hizi ndo zinatofautisha JF na platform nyingine uchwara kama Instagram na Facebook..

Mafuta ya taa yanatumiwa sana nowdays tuliza munkari kwa vijana lakini bado..mfano hao Lyamungo mwaka jana walitimuliwa wote baada ya kugoma, na wakarudishwa baada ya mwezi mmoja.
 
ah sio poa, mama sasa alivyokua analia, dogo alikua anaitwa Ayubu, mama aliletwa na defender ya magereza Karanga, gari lipo speed imewasha taa, ametua tuu pale mama ni mayowe, "uuwih mwanangu Ayubu, mbona wenzako waliweza kukimbia, tuseme wewe ndo ulishindwa kukimbia kati ya hawa wote?" hapo tupo Parade tunamsikiliza RPC na mkuu wa wilaya, huku ugeni wa waziri wa elimu ukiwa njiani.
.
.
aisee na ubishi wangu mimi na wa jamaa mmoja hivi kiranja wa ulinzi, tulilia!! yaan tulijiona na hatia, maneno yale yameshindwa kutoka kichwani miaka 12 sasa, hizi ni story tuu, ila ungetazama tukio ungeshangaa, hizi roho madogo wametolea wapi,
.
.
asubuhi watu wamefunga mashati kama kundi la kigaidi la alqaeda, wanasalimiana kwa lugha za Code kama majasusi, saa kumi usiku kibosho na zile kahawa ni giza, tunakutana na kina mama wa kibosho wanatulilia, jamani wanangu rudini, mmezaliwa na wanawake kama sisi, msiende! hakuna anaelewa!!
I can feel it mzee..Waziri alifika?
 
ni kweli, kwa umbwe ni zile bangi za Arusha, kuna jamaa alikua na beto kama jambazi, zile za kubonyeza ina fyatuka, mshkaji akitoka prepo usiku anaitoa alafu anaifyatua, fyaah!
.
.
ila lyamungo ni ukurya na mr. wandiba, kwakweli, kwenye vikao vya shule mzee yule kama vile alikua anaenjoy zile, ila lyimo walau alikua anatimua timua,
Kipindi Cha makange (Mungu amlaze mahali pema peponi) umbwe ilifika hatua tukaiita college kulikua na ufree uliopitiliza, migomo isiyoisha, walikua kupigwa ilikua ni mwendo wa uharamia, watu mda wowote wanaenda kulewa mpaka wanazima wanaletwa shuleni hawajielewi

Kipindi hicho form one mpaka six sare moja ya kaki ukija mgeni ukikaa vibaya unaingizwa mjini sababu huwezi tofautisha uyu ni form one au form four
 
Nyuzi kama hizi ndo zinatofautisha JF na platform nyingine uchwara kama Instagram na Facebook..

Mafuta ya taa yanatumiwa sana nowdays tuliza munkari kwa vijana lakini bado..mfano hao Lyamungo mwaka jana walitimuliwa wote baada ya kugoma..

Sent using Jamii Forums mobile app
Sio tu mwaka Jana lyamungo form three na form four ya 2008 walitimuliwa wote walikua ni wakorofi sana, kwa hiyo 2008 na 2009 hawakua na matokeo ya kidato Cha nne
 
Haha

Acha kulialia na kuleta hisia kama mtoto wa kike, thus is manhood mwanaume lazma uwe na dark side katika ukuwaji wako (from boys to men) na kikubwa nikujua jinsi ya kuji control mwenyewe mbeleni, huwezi ukaishi ki slope tu kama demu eti tukio lililotokea 12 yrs ago liku hunt hadi leo, bro upo serious?

Nyie hamkuwa na umoja mkakimbia na kumuacha mwenzenu, nae alifanya mistake ilo cost maisha yake kutotii matakwa katika himaya ya watu unachotakiwa kukubali ni kwamba Lyamungo walifanye self defense

Na hiyo kusema kuna mtu alikufa lymungo halafu hakuna hata jina lake wala makumbusho take kama ilivyo kwa Ayubu ni stori za nyie kwa nyie kujifariji
Sio kukimbia na kumwacha Ile ilikua ni ambush na jamaa alikua anaumwa na pumu ikambana ndo kilichomkuta

Waliattack na wakakimbia kumbuka walikua ugenin kulikua hakuna mda wa kupoteza
 
Nyuzi kama hizi ndo zinatofautisha JF na platform nyingine uchwara kama Instagram na Facebook..

Mafuta ya taa yanatumiwa sana nowdays tuliza munkari kwa vijana lakini bado..mfano hao Lyamungo mwaka jana walitimuliwa wote baada ya kugoma..

Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo idadi ya wanafunzi, wakati tunasoma Kuna wanafunzi kama 2000, munalala wanafunzi wawili kitanda cha futi 2 na nusu, matundu ya vyoo hata 10 hayafiki Maputo huko. Kula chakula vurugu, prepo vurugu, darasani vurugu, kwenye mpira vurugu, kila sehemu vurugu.

Vyoo vya mabweni vya kisasa vina space unakuta vimefungwa na wababe wanaishi huko, Dorm leader na marafiki zake.

Just imagine mamia ya wanafunzi wanakaa kwenye bwalo la shule Wana Angalia Ngono, hizo guts wanazitoa wapi? Viongozi wenyewe wa shule wanachaguliwa kwa kuangalia nguvu na influence, wengi nguvu nyingi kichwani sifuri. Unakuta mtu ana miaka kama 20 ama 30 hivi yupo form 1, hajielewi hata kidogo.
 
Tatizo idadi ya wanafunzi, wakati tunasoma Kuna wanafunzi kama 2000, munalala wanafunzi wawili kitanda cha futi 2 na nusu, matundu ya vyoo hata 10 hayafiki Maputo huko. Kula chakula vurugu, prepo vurugu, darasani vurugu, kwenye mpira vurugu, kila sehemu vurugu.

Vyoo vya mabweni vya kisasa vina space unakuta vimefungwa na wababe wanaishi huko, Dorm leader na marafiki zake.

Just imagine mamia ya wanafunzi wanakaa kwenye bwalo la shule Wana Angalia Ngono, hizo guts wanazitoa wapi? Viongozi wenyewe wa shule wanachaguliwa kwa kuangalia nguvu na influence, wengi nguvu nyingi kichwani sifuri. Unakuta mtu ana miaka kama 20 ama 30 hivi yupo form 1, hajielewi hata kidogo.
Mimi Advance nimesoma mixture (girls+boys) na idadi ilikuwa ya wanafunzi haikuwa kubwa..ilikuwa ni nadra sana kuona hata watu wakigombana..

So naungana na wewe idadi kubwa ya wanafunzi ni chanzo kimojawapo cha mavurugu na migomo kwenye hizi shule.
 
Back
Top Bottom