Vua gamba vaa gwanda karibu kusini

Ukana Shilungo

JF-Expert Member
Apr 17, 2012
3,041
2,422
m4c karibuni kusini.Possible ya kupata majimbo ilikuwa ni Nachingwea na Masasi kama mtandao wa chadema ungekuwa umeimarika ile 2010.kwanini?
  1. Mgombea wa Nachingwea Mathias Chikawe alikuwa amechuja hakubaliki na wanainchi,hivyo pangekuwa na mgombea makini toka upinzani angeshinda,kura za Maoni alielekea Kushinda Albert Mnaly yule Dc aliyewashikisha adabu kwa bakora walimu Bukoba,ila kwa kushirikiana Na Benard Membe wajumbe walirubuniwa eti Baba Rz 1 ana mpango nae na rushwa ikatembea,hv huyu Mnaly angeingia let say cdm na kama ingekuwa na mtandao imara Nachingwea ingekuwa na mbunge mvaa Gwanda.
  2. Masasi,aliyeshinda kura za maoni alikuwa mfanya Biashara ajulikanaye Kama Kazibure,akachakachuliwa akapewa Mama kasembe kwa maelekezo toka baba Rz 1,Kazibure aliogopa kugombea toka upinzani kwa kushauriwa na watu ,hasa Fitina za magamba na TRA,hivyo basi pangekuwa na Chadema Kimtandao immara,tungeongea mengine sasa.
  3. Mtwara mjini alishinda ule uchaguzi mgomea wa cuf anaitwa Uledi,redio fm zote zilitangaza matokeo ya kila kituo kilichobandika,na ccm walikuwa wana shindwa vibaya,baadae polisi walizuia kutangaza,mwishomwishoni matokeo yote yakageuka hasa sehemu ccm walizoshindwa awali zilionekana wameshinda,kimsingi watu walichoka baada ya Murji kutangazwa mshindi,kwa taarifa leo hii hata ikitokea by election ikawa fair magamba hawana lao Mtwara.
  4. Tandahimba ni wazi kabisa ccm ilianguka wakashinda cuf wakachakachua mchana kweupe,ndio maana kuna mgogoro mkubwa,uliohamia kwenye malipo ya korosho,lakini mzizi mkuu ni makovu ya uchaguzi mkuu uliopita 2010.
  5. Wito wangu kwa viongozi wa Chadema waje huku kwani ni promissing area kwa kuimarisha network ya cdm ili 2015 tuingie madarakani tukiwa na mtandao nchi nzima na kulizika joka hili liitwalo CCM.nimekuwa nikiwasiliana Na DR Slaa juu ya ujio wao kusini.
  6. Pendekezo lingine wakija Masasi wsisahau kufanya mkutano Mji Mdogo wa Ndanda ni potential area kijiografia,na penyewe palivyo,natumaini viongozi wa CDM wanatembelea Jamvini,attention Katibu Mkuu.
nawasilisha ,ni mimi mpiganaji katika M4c,
UKANA SHILUNGO NDANDA MTWARA.
 
:photo: Wapendwa wanaharakati wa kusini, karibu na mjiandae vema na M4C:-
1. Mtu mmoja aweke uzalendo mbele chukua hatua amia CDM
2. Fikiri mambo makuu yanyowezekana kupitia CDM yaweke mbele
3. shirikisha si chini ya watu 5 wawe na maamuzi na malengo kama yako
4 2015 tumia haki yako chagua CDM hakika saa ya ukombozi imefika Kusini
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom