Wezi sana hawa jamaa, na hiyo TCRA hawajali kitu, utadhani wana ubia nao kutuibia
Kuna kitu makampuni haya ya simu yanajiamini kupita kiasi, ndio maana
TCRA ianonekana kama hiko likizo vile!! We kampuni inawezaje kulazimisha mteja services ambazo hawaja-subscribe i.e matangazo yasiyo na tija, yaani hata kama una simu ya emergency unaanza kisikiliza milolongo ya matangazo ya kuhudhi tu, mara una ambiwa umejiunga kwenye voice mail wakati huja toa maagizo ya namna hiyo, mara sijui
MAHELA na sijui nani kawapa kibari cha kuchezesha kamari/bahati nasibu wakati kuna Shirika la Taifa linalo husika kuchezesha bahati nasibu!
Kampuni hizi zina-rip off wateja kwa kiwango cha kutisha na hawalipi kodi stahiki ya kuchezesha bahati nasibu - chukulia mchezo huu wa bahati nasibu unao endelea, Vodacom wanasema wana wateja karibu Millioni 12 na ushee kama sikosei, ukijibu maswali yao unakatwa karibu shilling 300 kila jibu na inaonekana wameweka lengo la kukusanya shilling 1,200/- kutoka kwa mteja ambaye anaweza kuingia mtego wa kujibu maswali yao yote kwa siku; sasa kama nusu ya wateja wao wanajibu, hebu piga mahesabu ni kiasi gani cha fedha Vodacom na wenzake wanakusanya kutoka kwa raia masikini kila siku, ni nyingi sana!!
Je watu wa
TRA na bahati nasibu ya Taifa wanafatilia vipi swala hili, Je
TCRA ina kipengele ambacho kinazungumzia/ruhusu makampuni ya mawasiliano kijihingiza katika biashara ya bahati nasibu? Mbona kuna kampuni ya Kirusi iliwahi kuingiza vifaa vya kuchezesha bahati nasibu kwa njia ya kisasa kabisa lakini Shirika la bahati nasibu ya Taifa likavikamata vifaa hivyo na kuviteketeza eti hawaruhusiwi, ukija makampuni ya simu hayo ni ruksa!! Kuna umuhimu wa TCRA kudhibiti mwenendo wa makampuni haya ya simu nchini kwa manufaa ya wananchi.