habari, kama ulitumiwa pesa hiyo na mteja mwingine ana haki ya kurudishiwa pesa yake endapo ataripoti kuomba kurudishiwa. Tunaomba namba yako ya simu pm kwa msaada zaidi.
transaction reverse kivipi !'? Na hujapokea wala kutumiwa pesa sijakuelewa mkuuVodacom Tanzania WAMENIPORA elfu hamsini kama mchezo. Huu mtandao hakika ni majizi walioshindikana.
Nina zaidi ya mwezi sijapokea wala kuweka Mpesa. Nimeshangaa ghafla napata meseji eti TRANSACTION REVERSED. Nikadhani utani, kucheki account yangu wamekomba 50,000.
Vodacom ni kwamba hizo fedha mnazodai kuwapa watu mamilioni ndio mnaziiba kwetu? Hata kama mnawahonga TCRA hii nawafikisha mbali.
==========
Majibu kutoka Vodacom Tanzania
Hata mimi ninamalalamiko na voda na nileishapiga simu lkn hakuwa msaada wowote walionipatia zaidi ya kunizungusha tu..ni hivi, mimi no wakala wa mpesa sasa huwa kuna kamisheni zinatoka kila mwisho wa mwezi lkn cha kushangaza walituma kamishen ktk 2nd na mm kuihamishia kwenye akaunt ya kazi fedha hiyo haijafika mpaka leo hii na nikiwapigia cm wala ooh..wasiliana na wakala mkuu na nikimpigia wakala ananambia ntakupigia baadae yani imekuwa ni kama nawakera vile..sasa uamzi niliofikia ni kupata msaada wa kisheria ili niweze kuwafungulia mashtaka maana walicho kifanya ni wizi mtupu..