Vodacom ni wezi wa bundle za wateja?

Vodacom ni wezi wa bundle za wateja?

kudaadaaadeki zao...
awa jamaa ni wezi hatari, jan nmeweka bundle la mb 10 mo0bile, naingia tu watsup natuma yx moja wananipa msg, salio lako la bundle linakaribia kuisha..!!!
hee nikashangaa nkajua utani assee..kumbe hawatanii
akat Tigo naweka hadi nasahau kama nliweka na waxup kama kawa
voda...sina hamu nao tena, siwataki hata bure dadeki zao!!
 
Shikamoo HALOTEL! Wadau ambao bado hamjahamia halotel mnachelewa bure...tangu nizaliwe sijawahi kuona SPIDI ya umeme kama hii ya Halotel. Asante VODACOM kwa kuniharakisha kuhamia Halotel kama vile Dr Makufuri anavyoharakisha kuhamia Dodoma. Jamani mkimbieni huyo SHETANI (Vodacom)....njooni huku kwa YESU (Halotel). HALOTEL ndio mpango wa MUJINI!!!!!!!!!!!!!

upload_2016-8-1_17-24-1.png
 
hili sasa ndo povu lenyewe ushameza ndoo ya omo kifupi voda ni wezi hiyo mitandao yote uliyoorodhesha hapo wako safi kinoma kifurushi cha jero unapata mb 300 wakati wezi voda unapata 150 na bado kwa dakiki 4 wanakula mb zaidi 37
 
Nyie mnaotetea voda....Ina maana watu hao wote wanaolalamika hawajui walisemalo??? Unataka kuniambia wote hawajui kama kuna mambo ya apps zinazo run kwa background???? Me nahisi hao wanaolalamika wana akili timamu na wanajua nini wanasema....kuhusu apps kurun kwa background kwan sisi tunaotumia halotel unafikir hamna hio kitu???? Au hizo apps hu run according to line unayotumia???(si kweli)...mbona sisi hizo apps hurun kwa background lakini hazili mb kihivyo (i know it depends na wingi wa apps,but still sitaki kuamini kuwa wateja wa voda wana apps nyingi kuliko wengine)kama ambavyo wenzetu wa Voda wanavyolalamika...
I think kuna ukwel hapo wenzetu wanaibiwa....
 
Juzi nimeingia mkenge, yaani hapa tumbo linawaka moto mda wote. Jamani juzi 22 August 2016 nimenunua kifurushi cha mwezi kwa njia ya M-pesa, elfu kumi nimepewa dakika 300. Niliongea max dak 30, jana nimeongea max dak 20, leo nimeongea na mtu hazijafika hata dakika 20 naletewa sms eti kifurushi kinakaribia kuisha dakika zipo chini ya 10. Natamani kufakufa wala sielewi, nahitaji faraja ya moyo wangu maana huu mtandao unanifilisi sana..........Sijui ibilisi gani aliniingia juzi hadi kujiunga!!!!!!, yaani halotel wananipaga dakika 1200+ na huwa sizimalizi kwa mwezi mzima. Huko nje nikimuona mtu ametaja voda moyo wangu unatenda dhambi maana namtukana sana kimoyo moyo tena matusi mazito mazito.........Kuna mitandao kama huu wa Voda haufai kuendelea kuwa nchini!!!!!!!
 
Mi cjawahi kusikia halotel wezi au wanalalamikiwa kiasi hichi,kwanza wanavifurushi bora kuliko hyo mitandao yenu yakizamani
 
Back
Top Bottom