Vodacom ni wezi wa bundle za wateja?


Iv we lizaboni akil yako ipo vzur kweli? We muda wote Ni siasa tu unawaza. Umemsaidia nn mtoa mada kwa Hilo jibu lako.
 
Sasa wanchokifanya tigo wao wanakupatia speed ya Kobe, utakesha nayo aiseee, Tigo na Airtel ndio mchezo wao yaani unataka kufanya mambo ya maana ikishafika saa nne usiku tu, hamna kitu kabisa TCRA wako busy kukamata watu wanaotuma maoni yao
 
Nimesoma post nimeielewa ila sijasoma comments
Mimi nilikuwa mtumiaji bora wa vodacom kwa takriban miaka sita, simu za laini mbili zikaniamsha kuwa na matumizi ya laini zaidi ya voda, niliweka utaratibu wa kuweka salio kwa zamu na kwa matumizi yaleyale kama hakuna dharula, lakini nilibaini uwepo wa makato yasiyo ya kawaida na mipango ya ki wiziwizi,

kwa mifano:

umenunua bando la 500 la saa 24 saa 11 jioni, kesho asubuhi saa tatu unaambiwa kifurushi chako kimekwisha muda wake,

Ama
Unaona meseji inaingia kwenye simu, eti umefanikiwa kujiunga na huduma ya...... (mtu akikupigia asikie mziki) wakati hujabonyeza chochote na simu ipo kwenye lock

Zaidi ya hapo ni tofauti za muda wa matumizi ya dakika sawa, yaani kila ukijiunga kifurushi cha voda ukiongea kinaisha haraka hata kama kina dakika sawa na cha airtel ambacho huwa kinadumu zaidi.
Huwa nina special numbes, ila nimeshaiweka voda pembeni, na jana nimeiweka kwenye simu ili niwazuge kidogo wasiifunge ilikataa kusoma nadhani wameiswap, siweki voda tena!!!!
Pole na wewe, umefanya vyema lakini kuanzisha uzi huu nimepata pa kusemea!!![emoji109][emoji109]
 
Du nilikuwa nadhania Ni mie peke yangu kumbe tumaibiwa Ni wengi , Vodcom acheni wizi wa mb
 
Kumbe ulikuwa youtube . Sasa unacholalamika nini..
 
Wanabebwa na M - Pesa kule Mikoani kwetu Chenga sana hao majamaa.
 
Si kweli net sijaanza kutumia leo. Nimeanza kutumia neti kabla systeam ya vifurishi haijaanza na nimetumia TIGO VODA ZANTEL AIR TELL TTCL ishu za computer na IT nazielewa lakini kifurishi kukatwa kabla ya matumizi kufanyika ni trend mpya niliyo experience kwa tigo na voda so far. Nilinunua modem ya 4g ya tigo na offer ya 90 gb kwa miezi mitatu kwa maana kila mwezi 30gb nikajua nimepata kumbe wapi. Ukichomeka tu modem usifanye chochote muda wa masaa matatu mpaka matano utakuta gb 3-4 hamna ilichukua wiki 1 na siku chache kukausha 30gb same thing ikajirudia kwenye 60gb zilizobakia. Sasa jiulize ni application gani hizo zinazo kula 30gb ndani ya wiki? HAPA WIZI TU[emoji47]
 
Sahivi wana app yao hovyo kabisa ukijiunga na kifurushi wanaanza kukutumia updates wakati mwingine picha za kipumbavu kabisa, hawa jamaa dawa ni kuwahama jumla
 
Kwel kabisa hawa sio..mim nilinunua mb 500 net ikasumbua sikufanikiwa kufany lolote..kesho yake vodacom wakanilipa mb 100 za usumbufu wa jana..hawa ni jipu
 
Voda.wezi.aisee..nilidhan my b simu yangu ina kaprogram kana jidowload maana mb zinakata bila sababu ya msingi
 
mim voda nina mwaka na miezi MITATU sasa tangu niwaache nashaanga mpaka leo kuna watu wangangsnia vodacom,
halotel ndo mtandao bora wako stable internet ya uhakika na gharama nafuu
 
Ni kweli kabisa mtandao wa Voda ndo unaongoza kwa wizi wa mb
 
sitasahau... walinipiga GB 2 mchana kweupe... nilipowapigia simu wakanambia wanafuatilia... mpaka leo...
 
Daaaa nimefurahia kwel uzi huu kwani nilijua tatizo ni kwangu tu,Vodacom ni WEZI period!!!!!!
 
Asante nilitaka nimuulize kuhusu auto download hasa kwa Pc
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…