Nimesoma post nimeielewa ila sijasoma comments
Mimi nilikuwa mtumiaji bora wa vodacom kwa takriban miaka sita, simu za laini mbili zikaniamsha kuwa na matumizi ya laini zaidi ya voda, niliweka utaratibu wa kuweka salio kwa zamu na kwa matumizi yaleyale kama hakuna dharula, lakini nilibaini uwepo wa makato yasiyo ya kawaida na mipango ya ki wiziwizi,
kwa mifano:
umenunua bando la 500 la saa 24 saa 11 jioni, kesho asubuhi saa tatu unaambiwa kifurushi chako kimekwisha muda wake,
Ama
Unaona meseji inaingia kwenye simu, eti umefanikiwa kujiunga na huduma ya...... (mtu akikupigia asikie mziki) wakati hujabonyeza chochote na simu ipo kwenye lock
Zaidi ya hapo ni tofauti za muda wa matumizi ya dakika sawa, yaani kila ukijiunga kifurushi cha voda ukiongea kinaisha haraka hata kama kina dakika sawa na cha airtel ambacho huwa kinadumu zaidi.
Huwa nina special numbes, ila nimeshaiweka voda pembeni, na jana nimeiweka kwenye simu ili niwazuge kidogo wasiifunge ilikataa kusoma nadhani wameiswap, siweki voda tena!!!!
Pole na wewe, umefanya vyema lakini kuanzisha uzi huu nimepata pa kusemea!!!

