Vodacom ni wezi wa bundle za wateja?

Vodacom ni wezi wa bundle za wateja?

Mkuu, pole sana. Huo mtandao wa Voda Lowasa na Rostam ndio wenye hisa nyingi. Lowasa kafilisika kutokana na kutumia fedha nyingi kwenye uchaguzi. Rostam Aziz naye kafilisiwa na Lowasa. Hivyo hawana namna ya kuongeza kipato zaidi ya kuwabana wateja wa kampuni yao

Iv we lizaboni akil yako ipo vzur kweli? We muda wote Ni siasa tu unawaza. Umemsaidia nn mtoa mada kwa Hilo jibu lako.
 
Sasa wanchokifanya tigo wao wanakupatia speed ya Kobe, utakesha nayo aiseee, Tigo na Airtel ndio mchezo wao yaani unataka kufanya mambo ya maana ikishafika saa nne usiku tu, hamna kitu kabisa TCRA wako busy kukamata watu wanaotuma maoni yao
 
Nimesoma post nimeielewa ila sijasoma comments
Mimi nilikuwa mtumiaji bora wa vodacom kwa takriban miaka sita, simu za laini mbili zikaniamsha kuwa na matumizi ya laini zaidi ya voda, niliweka utaratibu wa kuweka salio kwa zamu na kwa matumizi yaleyale kama hakuna dharula, lakini nilibaini uwepo wa makato yasiyo ya kawaida na mipango ya ki wiziwizi,

kwa mifano:

umenunua bando la 500 la saa 24 saa 11 jioni, kesho asubuhi saa tatu unaambiwa kifurushi chako kimekwisha muda wake,

Ama
Unaona meseji inaingia kwenye simu, eti umefanikiwa kujiunga na huduma ya...... (mtu akikupigia asikie mziki) wakati hujabonyeza chochote na simu ipo kwenye lock

Zaidi ya hapo ni tofauti za muda wa matumizi ya dakika sawa, yaani kila ukijiunga kifurushi cha voda ukiongea kinaisha haraka hata kama kina dakika sawa na cha airtel ambacho huwa kinadumu zaidi.
Huwa nina special numbes, ila nimeshaiweka voda pembeni, na jana nimeiweka kwenye simu ili niwazuge kidogo wasiifunge ilikataa kusoma nadhani wameiswap, siweki voda tena!!!!
Pole na wewe, umefanya vyema lakini kuanzisha uzi huu nimepata pa kusemea!!!
 
Du nilikuwa nadhania Ni mie peke yangu kumbe tumaibiwa Ni wengi , Vodcom acheni wizi wa mb
 
Wanabebwa na M - Pesa kule Mikoani kwetu Chenga sana hao majamaa.
 
Kabla hamjatumia vitu (mashikolo) muwe mnauliza kwanza ili mpewe maelekezo na wenye utaalamu na mambo hayo sio kulalamika tu bila point ya msingi, hivi wewe hujui kuwa laptop huwa ina-setting za background updating (yaani kuna software zinaji-update zenyewe kimya kimya tafuta mtu akusaidie settings mimi ni mtumiaji wa Vodacom toka enzi izo 0744 especially kwenye upande wa Internet huko kuliwa kwa mb tatzo ni laptop yako.
Si kweli net sijaanza kutumia leo. Nimeanza kutumia neti kabla systeam ya vifurishi haijaanza na nimetumia TIGO VODA ZANTEL AIR TELL TTCL ishu za computer na IT nazielewa lakini kifurishi kukatwa kabla ya matumizi kufanyika ni trend mpya niliyo experience kwa tigo na voda so far. Nilinunua modem ya 4g ya tigo na offer ya 90 gb kwa miezi mitatu kwa maana kila mwezi 30gb nikajua nimepata kumbe wapi. Ukichomeka tu modem usifanye chochote muda wa masaa matatu mpaka matano utakuta gb 3-4 hamna ilichukua wiki 1 na siku chache kukausha 30gb same thing ikajirudia kwenye 60gb zilizobakia. Sasa jiulize ni application gani hizo zinazo kula 30gb ndani ya wiki? HAPA WIZI TU
 
Sahivi wana app yao hovyo kabisa ukijiunga na kifurushi wanaanza kukutumia updates wakati mwingine picha za kipumbavu kabisa, hawa jamaa dawa ni kuwahama jumla
 
Kwel kabisa hawa sio..mim nilinunua mb 500 net ikasumbua sikufanikiwa kufany lolote..kesho yake vodacom wakanilipa mb 100 za usumbufu wa jana..hawa ni jipu
 
Voda.wezi.aisee..nilidhan my b simu yangu ina kaprogram kana jidowload maana mb zinakata bila sababu ya msingi
 
mim voda nina mwaka na miezi MITATU sasa tangu niwaache nashaanga mpaka leo kuna watu wangangsnia vodacom,
halotel ndo mtandao bora wako stable internet ya uhakika na gharama nafuu
 
Ni kweli kabisa mtandao wa Voda ndo unaongoza kwa wizi wa mb
 
sitasahau... walinipiga GB 2 mchana kweupe... nilipowapigia simu wakanambia wanafuatilia... mpaka leo...
 
Daaaa nimefurahia kwel uzi huu kwani nilijua tatizo ni kwangu tu,Vodacom ni WEZI period!!!!!!
 
Mkuu naomba kukuuliza Swali la kawaida? Kwenye simu yako au laptop yako hauna app yoyote? Kama unatumia laptop windows yoyote iwe 7,8,10 huwa inajiupdate automatically unless uniambie ulienda kwenye update ukaisete isijiupdate automatically, kwenye simu mkuu kama una app ambazo umeziinstall nazo huwa zinatumia bundle bila hata kutaka na apps hizo zipo nyingi tu, mfano BBC,CNN,ALJAZEERA,WHATSAPP na nyingine nyingi ambazo unaziona hapo kwenye screen yako yote. Vitu vingine kama sio mtaalamu unaweza kuona kama mazingaombwe mkuu a vumilia kidogo kidogo utaelewa tu. Nadhani kipindi cha nyuma mambo yalikuwa mazuri hata bundle wakati linatumika kwa vitu hivi hukuwa unajua ila Magufuli kabana ndio umegundua!
Asante nilitaka nimuulize kuhusu auto download hasa kwa Pc
 
Back
Top Bottom