Vodacom acheni wizi, Masaa 24 yako wapi hapa??

Vodacom acheni wizi, Masaa 24 yako wapi hapa??

Shark

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2010
Posts
29,917
Reaction score
30,030
Vodacom wamekuja na ofa mpya ya Super Cheka Internet ambapo wanaitangaza kwamba ni masaa 24. Lakini cha ajabu ukijiunga muda wowote ule, mwisho wa ofa ni Saa sita usiku.

Ina maana ukijiunga saa moja usiku utadumu kwenye ofa kwa masaa matano tu mpaka saa sita usiku, badala ya masaa 24.

Nimejiunga na hii ofa dakika chache zilizopita na nikapata meseji hii hapa chini

" Hongera!Umenunua dakika 30 kupiga Vodacom-Vodacom, SMS 100 kwenda mitandao yote na 50MB .Tumia kabla ya 5:59 usiku leo.Piga *149*01# ili kujua salio lako"
 
Hao nao ni wehu mie kila siku nanunua lkn hakuna masaa 24 wala nini ni wezi tu kama wezi wengne
 
Usisahau na ile bonus ya Tshs 50 mimi inanichekesha sana
 
Yaani kama nimejiunga saa moja kamili ya usiku huu, masaa 24 yalitakiwa kuishia dakika moja kabla ya saa moja kamili usiku wa kesho, sio leo saa sita usiku.

Otherwise wasingesema ni masaa 24, bali wangesema tu tumia kabla siku ya leo haijaisha, wangeeleweka!!
 
Cheka inaanza saa 6 usiku mpka saa 5 dk 59.. Sijui haya ni masaa 18!!!??
 
Mtandao umechoka mbaya. Leo mawasilano yalikuwa sifuri kabisa achilia mbali wizi.Msisahau mafisadi papa ndio wenye hisa.
 
Mtandao umechoka mbaya. Leo mawasilano yalikuwa sifuri kabisa achilia mbali wizi.Msisahau mafisadi papa ndio wenye hisa.
Jana roho iliniuma kweli,nilinunua 50 minutes za voda kwa buku,hapo hapo mtandao ukazingua nikashindwa kuzitumia hata sekunde moja.
 
Back
Top Bottom