Viwanda zaidi ya 3000 na vilivyokufa vimefufuliwa. Tupeane taarifa ya viwanda hapo ulipo

Tulimumu

JF-Expert Member
Mar 11, 2013
14,305
12,969
Kwa mujibu wa mwenyenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, ni kuwa zaidi ya viwanda vipya 3000 vimejengwa na vya zamani vimefufuliwa. Nchi hii ni kubwa inawezekana hapo hapo ulipo wilayani kwako au mkoani kwako hakuna lakini mkoa au wilaya nyingine vipo.

Hebu tupeane taarifa hapo ulipo wilayani au mkoani je kuna kiwanda kipya kimejengwa hapo? Ni kiwanda cha nini? Je kuna kilichokuwa kimekufa na sasa kimefufuliwa? Ni kiwanda cha nini? Hii itasaidia pia kupeana taarifa za ajira

Mimi hapa Kinondoni/Ubungo hakuna kiwanda kipya kilichojengwa. (Nasema mimi sijakiona kama kipo mnirekebishe) Vilivyokufa kama URAFIKI na UFI havijafufuliwa bado. Ila Ubungo kuna ujenzi wa Flyover na jengo refu la Tanesco linavunjwa
 
Soon watatwambia kila mwanaume ni kiwanda kwani mwanaume mashine na wauza pweza,vvumbi la congo na mikuyati ni viwanda vidogo vinavyoboresha ufanisi wa mwanaume mashine!!!

Awamu ya V-WONDERS!!
 
Nakikodolea macho machine toools, tarneries, kilitex, general tyre, hadi sasa naona tu nyasi zikiongezeka hadi getini. Labda viwanda vya matofali, vijiwe vya welding na kujaza pancha ndo viwanda pekee ninanvyoviona
 
kwa kweli viwanda ni vingi sana kama ni vyerehani mm hapa nilipo ninavyo viwanda viwili tayari koz Nina vyerehani 8.
 
Hayo matamasha ya uzalendo yanafanyika ili kulisha watu ujinga wa kukubali huo uongo wa mchana kweupe. Viwanda 3000 halafu hata picha hakuna. Hizo nyumba zilizovunjwa picha zake zimejaza server, inakuwaje hivyo viwanda 3000 picha zisionekane? Viwanda vipya kweli vipo ila havizidi 50 na vingejengwa tu hata kama kusingekuwa na hiyo ajenda fake ya viwanda.
 
Mwenyekiti wetu anajivunia hata viwanda vya Azam ..., Manji ..., MO ...

Viwanda alivyojenga Nyerere, vilijengwa na pesa ya Watanganyika kwa ukweli na uhalisia ..., sio pesa ya "wanyonyaji, mabepari au makabaila" .., kama wafanyabiashara walivyokuwa wakiitwa wakati huo ...

CCM ya sasa ni dude la ajabu kabisa ..., ili kuliamini ni lazima uwe kiazi kikuu ...!
 
Kwa mujibu wa mwenyenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, ni kuwa zaidi ya viwanda vipya 3000 vimejengwa na vya zamani vimefufuliwa. Nchi hii ni kubwa inawezekana hapo hapo ulipo wilayani kwako au mkoani kwako hakuna lakini mkoa au wilaya nyingine vipo.

Hebu tupeane taarifa hapo ulipo wilayani au mkoani je kuna kiwanda kipya kimejengwa hapo? Ni kiwanda cha nini? Je kuna kilichokuwa kimekufa na sasa kimefufuliwa? Ni kiwanda cha nini? Hii itasaidia pia kupeana taarifa za ajira

Mimi hapa Kinondoni/Ubungo hakuna kiwanda kipya kilichojengwa. (Nasema mimi sijakiona kama kipo mnirekebishe) Vilivyokufa kama URAFIKI na UFI havijafufuliwa bado. Ila Ubungo kuna ujenzi wa Flyover na jengo refu la Tanesco linavunjwa
Mi nina kiwanda cha kufyatua tofali kwa mkono. Mfuko mmoja kila mwezi.
 
Back
Top Bottom