joseph1989
JF-Expert Member
- May 4, 2014
- 19,406
- 41,534
Braza mshana kidogo mm swali langu lipo nnje ya mada miaka ya nyuma, nilikuwa nakaa na bibi yangu uswahilini, si unajua uswahilini mara mtu kaomba mboga, mara chumvi, moto na kadhalika, lkn bibi alikuwa hatoi moto kama akiombwa, ukimwomba kitu chochote anakupa, Kuna siku nikamuuliza hv kwa nini ukiombwa moto huwaga hutoi, akanijibu kwa kifupi watu huwa wanatumia kwa mambo yao ya kishirikina, ila hakuniweka wazi, je kaka mshana Kuna ukweli juu ya hii ishu ya moto?