Vituko vya wanafunzi ndani ya mitihani!

Vituko vya wanafunzi ndani ya mitihani!

Slim5

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2014
Posts
28,433
Reaction score
38,402
WanaJF nawataka hali!

Katika harakati za kimasomo kuanzia primary (cc wengine hatujapitia zile shule zenu ambazo curricullum inasisitiza mtoto aimbe, anywe uji wa maziwa na baadae alale) hadi College au University kwa waliobahatika, huwa kuna vituko ama visanga wakati wa mitihani!

Kwa O-level na A - level sana sana ktk mitihani ya mwisho ya NECTA, na kwa upande wa vyuo visanga ama vituko unaweza kuviona kwenye semester exams ama hata final UE!

Mimi nimependa ku-share na wadau vile visanga ktk mitihani nilivoona ni vituko wakati wa harakati za kimasomo, vichache vyake ni hivi:

  1. kuna rafiki yangu mmoja, miaka yote ya kujuana pale shuleni, tumemzoea kuwa jamaa ni mpole na ni mwenye aibu sana, si kwa wasichana tu, mpaka kwa sisi boys wenzake! wakati tunafanya mtihani wa CSEE mwaka huo, ktk mtihani wa somo la Kiswahili, jamaa ktk chumba chetu cha mtihani alikuwa amekaa mbele kabisa (ktk alphabetical arrangement jina lake linaanza A)! Pepa ya Kiswahili inaendelea, utulivu uko juu, watu wako busy, kimya kimya! Ghafla jamaa anagonga meza kumuita Invigilator. Kuangalia mbele, ni mshikaji. Msimamizi akamsogelea na kumuuliza shida yake, jamaa akasema ana shida na Calculator! Msimamizi hakuyaamini masikio yake, akamuuliza tena unataka nini? Jamaa akasisitiza Calculator! Ktk somo la kiswahili haikutegemewa kuwa na mwanafunzi hata mmoja mwenye calculator, ikabidi msimamizi amuombe mwl mmoja wa pale pale shuleni kwetu akamletee jamaa calculator. Ikaletwa na akapewa! Darasa tulipigwa na taharuki na kuanza kuhaha tukitafuta ni wapi ktk mtihani ule wa Kiswahili, labda ile calculator imetajwa, hatukuona! Baada ya mtihani yule msimamizi na mwl walimwita awaeleze nini kazi ya ile calculator ktk mtihani wa Kiswahili, jamaa akawajibu alikuwa anatafuta TOTAL ya marks anazotarajia kuscore kwa pepa ile! Tulichoka.
  2. Hii ya pili nayo ilikuwa ktk pepa hizo hizo za NECTA za O-level. Sikumbuki ilikuwa ktk somo gani lakini katikati ya mtihani, ktk harakati za kusaidiana wanafunzi kwa wanafunzi ndani ya chumba cha mtihani. Jamaa jirani yangu kamgeukia mwenzake wa nyuma yake kumuomba msaada. Muomba msaada alisema kwa sauti na sote tukaskia (sijui kwa nini pamoja na ukubwa wa shule yetu na wingi wa wanafunzi, usimamizi ndani ya exam room huwa wa kawaida sana, sijui ni kwa vile govt sch ama vp, na kuna wakati tulisimamiwa na walimu wetu wa ndani). Jamaa kamuuliza mwenzie kama Zanzibar ipo Afrika! Wengi tuliskia lile swali, tulicheka sana, yaani mpaka msimamizi aka-mind! cha ajabu pepa nzima ya lile somo (sikumbuki somo gani) hakuna sehemu ama hata Multiple choices ilipotajwa zanzibar, achilia mbali hata ule upande wa maswali ya essay, Zanzibar haikutajwa pepa nzima!
  3. Hii nyingine boys ilitupa tabu sana! Ktk pepa ya Maths, tumepewa booklets vizuri! Tukapewa answer sheets. Tukaambiwa tujaze zile details za nje ya booklets, tukajaza vzr! Msimamizi akataja time, ile anaruhusu tuanze mtihani tu! Ghafla jamaa yetu mmoja anatetemeka! Mara anamaliza kutetemeka, akamwita msimamizi, anaomba ruhusa aende toilet! Yaani hata dk 5 bado tangu turuhusiwe kuanza pepa. Msimamizi akamkomalia aseme amepatwa na nini. Jamaa akawa anamgomea, wakabishana kama dk 10! Msimamizi akaenda kumwita mwl wa pale shule, mwl kuja akanong'ona na yule mwanafunzi! Baadae mwl nae akaongea na msimamizi! Wakawa wamefikia muafaka jamaa aruhusiwe kutoka, jamaa kasimama atoke (alikaa siti za nyuma) suruali chapa chapa eneo lote linalozunguka zip! Tulichoka!
  4. Chuoni nakumbuka kuna bidada aliweka kali "alijichora majibu" juu ya mapaja kisha akapiga min 1 matata! cha kupendeza zaidi yule bi dada alikuwa mrembo wa haja. Basi kila baada ya muda kuna invigilator anakuja kuangalia yale mapaja! kila baada ya muda anakuja, anaangalia as if na yeye anahamisha majibu kutoka ktk mapaja ya bidada! Mwisho wa pepa invigilator akamuita (tukaanza kutaharuki na kujua tayari mrembo wetu wa class kasha-disco), ukistaajabu ya Musa.......si akamuuliza kama yale majibu juu ya mapaja aliandika mwenyewe ama aliandikwa na mtu? Bidada akamjibu aliandikwa na mtu, invigilator akamwambia siku nyingine hiyo kazi apewe yeye!

Tukumbushe visanga ama vituko wakati wa mitihani shuleni ama chuoni kwenu!
 
Mi nakumbuka pepa la form 4 maths lilivuja ilikua shangwe kwa vilaza wote kila mtu alikua ns majibu ilikua tunaenda kuyajaza tu kweny ansasheets..lahaura kuingia kwenye chumba cha mtihani maswali yalikua ni tofauti kabisaa na yale yaliyo vuja..kilaza mmoja alipanic akagonga meza akamwita msimamiza akamwambia mtihani sio wenyewe aliongea kwa sauti.watu wotu atukua na mbavu kwa kucheka.
 
Tukiwa kwenye paper ya history kuna mwanafunzi aligonga meza then alipayuka kwa sauti NAOMBA FOURFIGURE
 
Hii ni kweli,pepa ya mock form two,shule ni boys tu.

Paul akamuomba invigilator ruhusa aende toilet,invigilator akamgomea akamwambia kama anashida akojoe mule mule exam room.

Paul akasogeza kiti na akakojoa chini then akendelea kupiga pepa.
 
Nakumbuka pepa ya banking law chuoni, kwavile lilipangwa kuwa la mwisho kati ya mitihani yooote ss watu janayake c wakakesha club ili wakija wapige waue maana likizo time inafuata. Kama kawaida keshoyake saa 2asbh prof. kaingia exam room na kuanza kugawa pepa bas jamaa mmoja baada tu ya kugawiwa lake akamwita tena sorry ticha, ticha akaja, jamaa kamwambia kwa sauti kubwa hii co bili yangu, hlf akaanguka kutoka kitini had chin, bas darasa zima kwi..kwi.. kwi, ss prof. kauliza anasemaje huyu? Watu huku wanambeba frm class to hostel ana malaria tokea jana ticha! Hlf huyo jamaa na kichwa hataree alipangiwa pepa yake sk nyngine akapasua A
 
Nakumbuka nikiwa Primary School STDs 4 tukiwa tunafanya Papers za Mwezi Juni,ilikuwa Paper ya Kiswahili nilikaa jirani na Kilaza fulani hivi Bonge la Mtu,nikawa namwonyesha Paper ili adese Jamaa alidesa mpaka Jina langu. Kimbembe ikawa wakati wa usahishaji then kugawiwa Paper,Mwl akakuta Frank Wanjiru wawili kwenye karatasi mwingine ana hati nzuri mwingine kama bata kaharisha,Mwl akanibana nieleze nilkaa na nani nikawataja kama 4 hivi ili Mwalimu acheki ambae jina lake halipo ndio muhusika.
 
Ilikua 1997 nipo kidato cha tatu Kitomondo Sekondari-Mafia
Nilipigwa suspension kurudi mitihani imeanza nikafanya mbinu zangu nikapata paper ya Maths,unaambiwa kazi ikanipata hakuna wa kuweza kunisaidia kusolve maswali na alienipa aliniambia nisimshirikishe mtu.
Kuingia ktk mtihani matokeo nina marks 23%.
 
pratical biology necta form 6 tulipewa chura tumdisecte in situ yaani tumchane na kuonesha viungo vya ndani bila kukata kiungo chochote.njemba moja ikakata moyo bahati mbaya ikabidi aumeze kuogopa f..jamaa akamuita invegilator na kumuambia chura wangu hana moyo...mwalimu katafuta mpaka mwishowe akampa chura mwingine
 
Nakumbuka paper ya form four, kuna jamaa alipata mtihani wa maths. Kipindi kile booklet haziandikwi mwaka na zilikua zinazagaa tu. Jamaa alichofanya kaandika Kila kitu kabla hajaingia room. Kuingia room kaandika Namba tu. Na booklet alopewa chumba cha mtihani kaificha. Baada labda ya dkk 15 tu anaomba kutoka keshamaliza. Msimamizi kuangalia pepa jamaa kajibu fresh. Ilibidi msimamizi amwambie jamaa 'akili unayo lkn speed huna'

Mwengine kaandika kibomu kwenye karatasi msimamizi kamkamata nalo, waling'ang'aniana Mpk jamaa kalipata na kulimeza kuondoa ushahidi.

Mi nakumbuka mtihani wa chuo nlisahau.neno advice Mpk nkamuuliza Jirani yangu.
 
Chuoni mdada kaingia kwenye mtihani wa mwisho wa semester kajichora majibu mikononi, bana si akazimia kwenye mtihani, wakamchukua kumpeleka hosptal wakamtoa nguo wakakuta yale majibu alipo amka kesho yake academic suspension ikamhusu
 
Kuna mwingine aliliaa kwenye mtihani na kumwambia mwalimu kua hayo yalitoka hawajawah kufundishwaaaaa hahhhhhhahha
 
Kwenye mtihani wa language 1 A level,jamaa kaingia darasani yuko nzwiii msimamizi kamuuliza kwanini unaingia kwenye exam umelewa? Jamaa akajibu teacher nataka niandike kiingeleza kizuri!
 
Mzee Es,

uncle huyu jamaa kenda mbali sanaa. Huwezi kutishia na bastola na kisha kuua kwa kisingizio cha bahati mbaya.
Kwanza kabisa ktk kesi za mauaji, ku-withdraw bastola ina maana moja tu unataka kuitumia!..
Pili huwezi kuondoa safety ikiwa huna kusudio
Na mwisho huwezi kuielekeza kwa mtu ikiwa kidole chako hapo ktk trigger na kudai bado bahati mbaya.
Kuua kwa bunduki na hasa bastola hakuna bahati mbaya unless mtu huyo ni mtoto mdogo asiyejua anachofanya.

Huyu, mshikaji kaua na haki lazima isimame!

Angel kwa hii ya mwisho nimeshakupenda!
 
pratical biology necta form 6 tulipewa chura tumdisecte in situ yaani tumchane na kuonesha viungo vya ndani bila kukata kiungo chochote.njemba moja ikakata moyo bahati mbaya ikabidi aumeze kuogopa f..jamaa akamuita invegilator na kumuambia chura wangu hana moyo...mwalimu katafuta mpaka mwishowe akampa chura mwingine

Dr chichi umetisha!
 
Chuoni mdada kaingia kwenye mtihani wa mwisho wa semester kajichora majibu mikononi, bana si akazimia kwenye mtihani, wakamchukua kumpeleka hosptal wakamtoa nguo wakakuta yale majibu alipo amka kesho yake academic suspension ikamhusu

Roho mbays
 
Chuoni mdada kaingia kwenye mtihani wa mwisho wa semester kajichora majibu mikononi, bana si akazimia kwenye mtihani, wakamchukua kumpeleka hosptal wakamtoa nguo wakakuta yale majibu alipo amka kesho yake academic suspension ikamhusu

alafu akazimia tena hahahahaha
 
Ahasante mi napenda jamii forum hasa wikend ikiwa ndefu mi sitaki kukumbuka mbali , ila nilifaulu vzr japo daah kuna wakali zaidi tangu niliwaacha ila nakubali walikuwa wakali sana .. Big up OBEDI ULIJA wew ulikuwa mkali class acha
 
Back
Top Bottom