Kupiga simu chooni, kuvuta mjani, kugonja walimu wa kikeni waliokuwa wakija field, kuuza biskuti, kuvunja makontena ya vilaza, watu tulikuwa na funguo zaidi ya 500 hizi ni za kupampu makufuli, wakati tuko shule, tunamiliki shamba bondeni, la nyanya na miwa, kupiga walimu wanoko mida ya prep, kutoroka usiku tunaenda mlima zinaa, kulala ktk mabweni ya wasichana na wasichana kujichanganya ktk mabweni ya masela, kuingia class na vi-bom, kupiga simu chooni, disko vumbi, kuwekeana mafuta ya taa ktk chakula, kuchambia godoro, kulamba sahani baada ya kula, kupiga passpot size,
Njuka mnyonge alibanduliwa au kunyonya rungu, kufunga mawe ktk mataulo kisha taa inazimwa dakika tano, muda wa kufunzana adabu, hii kila siku saa tano usiku, kupakana losheni, au kuvunjiwa yai ukilala kisha wanasingiziwa vibwengo, kuuza magodoro ya walioingia darasani wiki dume, godoro linabadilishwa na sahani ya wali maharage, mchaka mchaka saa kumi za usiku kisha mnafuata maji ya kuoga chini ya mlima..na mwisho tukachoma shule moto kisa hawakutupikia wali wiki mbili mfululizo
Nilikuwa waziri wa chakula, kampani yangu walijaziwa kuliko maadui zetu, sisi chakula tulikuwa tukiweka katika ndoo ya lita 20 watu watano, tulikuwa wanafunzi 1200 lakini nyama inapikwa kilo kumi na tano tuu, hapo waziri wa msosi nachoma kilo moja na ikiiva najaza kisado, wengine wanakunywa supu...tulibadilishana wali kwa penzi....pamoja na yote, darasani tulikuwa vizuri... mvua ikinyesha wote tulitoka nje uchi tukioga...kutokana na utukutu niliokuwa nao, pesa ya matumizi nilipewa buku na panadol tu, lakini nikirudi rikizo nilikuwa na zaidi ya laki tatu...