

HUWEZI KUAMINI LAKINI NDIO HAYA


Wanaisababishia Serikali hasara bilioni 71.... Adhabu yake.... kifungo miaka 4au faini milioni 12.

Najaribu kufikiria haya mambo najisikia vibaya sana....

Jana tu tumepata habari za kutisha mwanamke mmoja amekutwa na vipande 12 vya nyama ya Swala amehukumiwa kwenda jela miaka 22 hivi Msomaji wangu Unaweza kuelewa hii??

Usifikiri ni nje ya Tanzania,ni humu humu Tanzania, halafu Watawala wanahubiri eti.....Kuna utawala wa Sheria na Haki.....hii ni kweli???

Iko wapi Haki hapa? Viongozi mnayasikia haya na mnapata Usingizi?

Mheshimiwa Rais unayasikia hayaaa?

Mheshimiwa Makamu wa Raisi, Waziri Mkuu, Waziri wa sheria mnayasikia hayaa?

Kwetu sisi hii ni maumivu Makubwa, hatuelewi Mnatarajia tuyachukulie vipi.


Kama huku ni kuchoka tokeni madarakani waongoze Wengine, mahakamani tunaambiwa ndipo mtuhumiwa anapata haki yake Kweli?Je ni Kweli mahakamani ndipo haki inapotafisiriwa??


Tusaidieni Nchi yetu isiingie kwenye Laana, hatuhitaji laana tunataka baraka Ondoeni watendaji mahakamani wabovu hawa ni Aibu kwa Taifa na mbele za Mungu ni #Chukizo.!!
View attachment 2807416
Sent using
Jamii Forums mobile app