Pichani ni moja ya vivutio vikubwa kwenye banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye Maonesho ya Nanenane Nzuguni Jijini Dodoma ambao ni kuku aina ya Brahama wenye asili ya Saudi Arabia na kwa pamoja (wawili) wanauzwa shilingi milioni 1.
Wizara ya Mifugo imesema hao ni kuku wa pili kwa ukubwa Ulimwenguni ambao hufikia mpaka uzito wa kilo 7 na ni kuku wa mapambo na biashara na ni rahisi kufuga kwasababu hufugwa kwa njia za asili kama kuku wengine.
Kuku Jike anaanza kutaga mayai akiwa na umri wa miezi 6 na hutaga mayai yasiyopungua 20 na huweza kuishi mazingira yoyote.
Kuku hao walikuwa sita kwenye maonesho na tayari wanne wameuzwa na kwa sasa wamebaki wawili.
#MillardAyoUPDATES
View attachment 2709392
Sent using
Jamii Forums mobile app