Price tag ya milioni 20 imepata matumizi mengine kwenye shopping za Tanzania baada ya Duka maarufu la vifaa vya majumbani la ABC Emporio Dar es salaam kuonesha choo kipya cha kukaa kinachouzwa kwa shilingi milioni 20 za Kitanzania.
Ni choo ambacho kinampa Mtumiaji massage wakati anapokitumia, kinamtawaza, kumpa joto kama anahisi baridi pamoja na huduma nyinginezo ambazo Mtumiaji anaweza kuzichagua kwa kutumia rimoti maalum inayokuja na choo hicho.
Meneja Masoko wa Emperio Rashid Ally amemwambia Mwandishi wa @AyoTV_ Paschal Mwakyoma kuwa tayari vyoo vya aina hii visivyopungua vitano vimeshanunuliwa, video nzima kuhusu choo hiki ipo hapa youtu.be/zH-tDsKJyY8
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.