Vituko mitandaoni. Tupia chako

Eti mwanangu wanamsingizia newton wa watu eti alikuwa mboga wakati yy alikuwa anafikiria tu kutafiti physics na kusoma biblia basi

Yaani huyu Mungu kweli kaumba baadhi ya watu ili tu watekeleze adhma flani duniani

Mchizi alishawahi kupiga hadi siku 5 bila kulala,, kisa ma research yake,,, kula anasahau yaani


He was built different aseee ile plague yao inayofananishwa na kizazi chetu (corona)
Ndo alitumia kuandika ma principia na kututesa nayo japo yameijenga dunia sana
 

Mbali na kuweka misingi ya Optics, Gravity na mambo mengine, muda huo pia ndiyo aliutumia kugundua Calculus....japo kuna mzozo mpaka leo kuhusu mgunduzi hasa wa Calculus kati yake na mwamba mwingine wa kuitwa Leibniz....

Hawa ni watu wa kipekee ambao Mungu huwaleta ili kufungua njia mpaka watu wa conspiracies wanadai kwamba pengine hawakuwa binadamu wa kawaida bali aliens waliotumwa kuja kumsaidia binadamu kupiga hatua katika sayansi na teknolojia...Na wengine wanadai kwamba kila binadamu ana uwezo huo kama tu akiweza kujifunza jinsi ya kutumia inner power na ubongo wake sawasawa....

Imagine kama huyu mwamba kutoka India aitwaye Srinivasa Ramanujan. Huyu alijifundisha hesabu mwenyewe na hakusoma lakini aliishangaza dunia kwa ujuzi wake wa hesabu mpaka kufikia kuwekwa level moja na miamba katika taaluma hiyo. Mpaka leo kuna mzozo kama hili linawezekana kwa binadamu wa kawaida. Japo alikufa akiwa na miaka 32 tu (kuna tetesi kuwa aliuliwa maana uwezo wake wa hesabu ulikuwa unatisha) lakini ameacha alama ya kudumu katika Hisabati....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…