Neema Nyangige (19) Mkazi Kata ya Buswahili, Wilaya ya Butiama mkoani Mara amemlalamikia mme wake ambaye ni Bi. Wegesa Msheshe (75) aliyemuoa Nyumba Mbokhe (mwanamke kumuoa mwanamke) kumlazimisha kufanya mapenzi na vijana wake wanne au kurudisha mahari zote endapo akikaidi.
Neema amesema kuwa alipata mimba za utotoni jijini Mwanza hivyo hamjui baba wa mtoto na aliporudi kijijini akakuta wazazi wake wanadaiwa pesa kwenye kikundi, hivyo ikabidi wamuozeshe kwa bibi huyo ambaye alitoa mahari ya ng'ombe tano na mbuzi watatu.
Wazazi wangu waliuza mahari yangu ili kulipa madeni sasa huyu mme wangu (Bibi) pamoja na vijana wake wamekuwa wakinipiga mara kwa mara kisa nimekataa kuwakubalia kile wanachotaka, mpaka sasa nimefukuzwa na wameniambia nirudishe ng'ombe na mbuzi zote walizoniolea," amesema Neema
View attachment 2448276