Bibi na babu..
Bibi na Babu walisafiri mbali wakielekea kwa mtoto wao ambae hawajamuona siku nyingi.
Walipofika njiani wakawa wamechoka Sanaa. Wakaamua kutafuta hotel ili walale.
Wakakubaliana walale kwa masaa 4. Wakalala,
Walipoamka, mfanyakazi wa Hotel akawatoza Tsh. 500,000/=
Wale wazee wakashangaa hata kama ni hotel ya kisasa lakini sio laki 5 kwa masaa 4.
Babu akagoma kulipa akasema aitiwe meneja.
Meneja akaja kuwasikiliza
Babu: ” Kwanini bili ni kubwa hivi hata kama ni hotel ya kisasa?”
Manager;“kuna maswiming puli, ya kisasa sana hapa “
Babu; “Lakini hatukuyatumia”
Manager; “Ah ah ah... Lakini mngeweza kutumia kama mngetaka”
Babu: “Hata hivo bado haistahili kuwa laki 5”
Meneja: “Pia Kuna waimbaji kutoka Sauzi, Uganda , Rwanda, Congo, nk."
Babu: “Lakini sisi hatukuwasikiliza”
Meneja: “Ndiyooo, ni kweli.... Lakini mngeweza kama mngetaka”
Babu; aka give up na kumwambia mkewe aandike cheki uwape,,
Bibi akaandika akampa meneja.
Meneja anaangalia anaona sh. 50,000
Akashangaa na kusema. “VP mbona hamsini'”
Bibi akajibu “450,000 ya kulala na mimi”
Meneja akajibu; “Ebooo! Duh, Lakini sijalala na wewe Bibi !!!”
Bibi :“ "Ungeweza kama ungetaka 😎"