Vituko mitandaoni. Tupia chako

Vituko mitandaoni. Tupia chako

Wananchii
JamiiForums364867911.jpg
 

Faini​

Polisi alimdaka jamaa anakojoa pembezoni mwa ukuta.
Polisi: Wewe huoni hicho kibao kuwa panakatazwa kukojoa hapa?
Jamaa: nilibanwa sana afande, samahani!
Polisi: Faini yake elfu tano.
Jamaa akatoa noti ya elfu 10.
Polisi: Sasa chenji tunaipataje?
Jamaa: Tafuta chenji unipe changu.
Polisi: Basi kojoa tena…
 
Update: Pichani wanandoa hao ambao mume amepitwa miaka 37 na mke wake huyo wametangaza kutaka kupata mtoto ambapo watatumia shilingi milioni 333.7 na tayari wamempata mwanamke wa kumuajiri awabebee mimba

Mke huyo anaitwa Cheryl ana miaka si chini ya 61 wakati mume wake huyo anaitwa Quran McCain(24) ambapo kwasasa wanaishi Rome, Italia baada ya kufunga ndoa mwaka 2021

Cheryl tayari alishazaa watoto 7 na ana wajukuu 17 katika mahusiano yake ya mwanzo, lakini Quran yeye bado hana mtoto kwahiyo wameamua ili kulinogesha zaidi penzi na ndoa yao basi wapate mtoto ambapo mbegu tayari wameshapata mwanamke wa kumuajiri awabebee hiyo mimba na watatumia jumla ya gharama £120,000 ambazo si chini ya milioni 333.7 za Kitanzania

Wamesema wanapendana sana kila mmoja anamfurahia mwenzie ambapo penzi lao lilianza kipindi cha nyuma baada ya mwanamama huyo kuachia video mtandaoni akicheza muziki kisha watu kuanza kumchamba na kukosa furaha ambapo Quran alianza kumfariji na baadaye penzi kuchanua na hatimaye kufunga ndoaView attachment 2283164
hii stori huijui vizuri! huyo mbibi alifariki hotelini katika mazingira ya kutatanisha akiwa na huyo mshikaji! jamaa kala bingo kama mume kurithi mizigo wa huyo mkewe! sasa unavosema kwa saivi wanaishi italy unazingua
 
Back
Top Bottom