APEWA SIKU 15 ARUDI URAIANI, AMPE MKE WAKE MIMBA KISHA ARUDI JELA
Jamaa anayetumikia kifungo cha maisha jela mahakama yampa ruhusa siku 15 kurudi uraiani kumpa mimba mke wake kisha arudi jela
Mwanaume husika kwa jina la Nandlal(34) , mke wake kwa jina la Rekha ameenda kuililia mahakama ya Jodhpur/Rajasthan nchini India akitaka apewe mimba na mume wake anayetumikia kifungo cha maisha jela
Mahakama iliamua kupitia vifungu kadhaa vya sheria na imani mbalimbali za kidini ikiwemo Uhindu, Ukiristo, Uislamu, Judaism na kuona mojawapo ya mambo muhimu katika maisha ni pamoja na mtu kuendeleza vizazi/koo pale anapoamua iwe hivyo ndio Rekha akasikilizwa ombi lake
japokuwa mume huyo amefungwa maisha kwa makosa yake lakini kwa upande mwingine mahakama imeona hali hiyo imemuathiri mke wake kihisia na haki yake ya kupata tendo la ndoa licha ya kuwa yeye mke hana makosa yoyote ndio maana amesikilizwa
Pia imeelezwa, kipindi cha nyuma mahakama ilimpa mwanaume huyo ruhusa ya kwenda uraiani kwa siku kadhaa halafu muda ulipoisha akarudi mwenyewe jela kuendelea kutumikia kifungo chake cha maisha hivyo alionesha nidhamu na utii wa sheria ndio maana wamempa tena siku 15 arudi uraiani kumpa ujauzito mke wake afurahie maisha yake na ya ndoa halafu mume arudi zake gerezani
Follow hii page kwa Habari zaidi
Millard Ayo Breaking News, Дар-эс-Салам. Отметки "Нравится": 970 · Обсуждают: 2 997. Award winning Tv/Radio personality /Amplifaya CLOUDS FM/A Journalist covering East africa video.
www.facebook.com
#JAYSADIAN___UPDATES