Aliyekueleza kuwa Kampeni za Uchaguzi wa Rais nchini Tanzania mwaka 2025 hazijaanza basi huyo ni wale bahaji (wachawi)! Wenzako wameshaanza kampeni zao kitambo. Nenda kajionee mabango yaliyotamalaki Jijini Dar es Salaam katika Barabara ya Morogoro, Barabara ya Pugu na kwingineko! Tazama mabango yale na maudhui yake. Unafikiri mabango yamebeba picha na kaulimbiu za Mgombea Udiwani wa Kata ya Mchafukoge? Mawe! Mambo haya yanamhitaji Askofu kuyaongelea kwani yeye hata akifa atakuwa amefia kazini kama Yohana Mbatizaji! Wengine kuleni nazi au kuleni kobisi!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.