Na kwenye huo uwanja wako hayo mambo ndiyo yamejichimbia hasa. Inaaminika kabisa kuwa bila hivyo huwezi kutoboa.

Mama unayemzungumzia ni yule wa juzi kule Arusha? Inasikitisha sana!
Siyo huyo.
Mwingine kabisa ni kitambo cha miaka zaidi ya 20 iliyopita mzee.
Hata wewe uchawi unajua vizuri.
Maana nimepita pita sana maeneo yenu huko Shinyanga, Mwanza, Geita nimewaona wenyeji wa huko wanavyoupa kipaumbele.
Nadhani kama kuna maeneo ambayo elimu ya uchawi imejikita ni huko.
 
Wewe mwenyewe bro umekiri Umesikia!

Haya mambo hata kama yapo ila sio kama hivi visa vinavyotokea huku kwetu, mf kisa kama hiki cha kulala mbea kuamkia juu ya mti mtwara.
Mkuu binafsi mambo haya hayana nafasi. Imani imeonya sana juu yake lakini yapo.

Huyu mama wa rafiki yangu alijidai mganga, akaleta dharau mbele ya wajuaji.
Asubuhi moja alijikuta juu ya mwembe Kinondoni Moscow, ingawa usiku alikuwa amelala Sharif Shamba Ilala. Nadhani ilikuwa 1989.
Tukio hilo lilipelekea maradhi hatimaye kifo.
Ni kisa furani cha kishirikina ingawa unaweza sema mazingaombwe.
 
Uchawi ndiyo mila pekee tunayoweza kujivunia.
Ni vema tuiendeleze, tuiboreshe na tuiweke vitabuni hatimaye tuanzishe vyuo ili watu wa mataifa waje wajifunze.
Jivunie chako.
Sayansi ya NASA ni yao mzee
Kwa kweli hata sijui tunakwama wapi. Imagine mtu unaruka na ungo tu yaani. Hakuna cha mafuta wala injini. Mtu analala Mbeya anakuja kuamka yupo kwenye mti Mtwara. Kafikaje hakuna ajuaye. Yaani tumekalia teknolojia ya kiwango cha juu na isiyokubaliana na nadharia za sayansi zilizopo.

Tuiboreshe tufundishane mashuleni. Miaka 10 tu wazungu tutakuwa tumewaacha mbali sana!
 
Siyo huyo.
Mwingine kabisa ni kitambo cha miaka zaidi ya 20 iliyopita mzee.
Hata wewe uchawi unajua vizuri.
Maana nimepita pita sana maeneo yenu huko Shinyanga, Mwanza, Geita nimewaona wenyeji wa huko wanavyoupa kipaumbele.
Nadhani kama kuna maeneo ambayo elimu ya uchawi imejikita ni huko.
Huko Usukumani kila kitu ni uchawi. Kila kifo ni uchawi. Hata mtu akigongwa na gari laivu ni uchawi kachukuliwa msukule. Ukifa na UKIMWI ni uchawi.

Mwaka fulani dogo mmoja aliumwa na mbwa. Tukawaambia mpelekeni akadungwe sindano ya kichaa cha mbwa wakapuuzia. Lilipokuja kubumburuka dogo kachanganyikiwa kichaa cha mbwa hichoo. Madaktari wakampima kweli akakutwa na rabies. Na kwa vile hakuna tiba dogo akafa. Moto sasa ukawaka eti karogwa kachukuliwa msukule. Vurugu tupu!

Ndo maana kule kucharangana mapanga hakutaisha na ndiyo kikwazo kikubwa kimojawapo cha maendeleo japo sasa kidogo hali inabadilika. Zamani kidogo tu watu walikuwa wanaogopa hata kujenga nyumba ya bati kisa kurogwa. Yaani badoooo sanaaa!
 
Huko Usukumani kila kitu ni uchawi. Kila kifo ni uchawi. Hata mtu akigongwa na gari laivu ni uchawi kachukuliwa msukule. Ukifa na UKIMWI ni uchawi.

Mwaka fulani dogo mmoja aliumwa na mbwa. Tukawaambia mpelekeni akadungwe sindano ya kichaa cha mbwa wakapuuzia. Lilipokuja kubumburuka dogo kachanganyikiwa kichaa cha mbwa hichoo. Madaktari wakampima kweli akakutwa na rabies. Na kwa vile hakuna tiba dogo akafa. Moto sasa ukawaka eti karogwa kachukuliwa msukule. Vurugu tupu!

Ndo maana kule kucharangana mapanga hakutaisha na ndiyo kikwazo kikubwa kimojawapo cha maendeleo japo sasa kidogo hali inabadilika. Zamani kidogo tu watu walikuwa wanaogopa hata kujenga nyumba ya bati kisa kurogwa. Yaani badoooo sanaaa!
Nimeshangaa sasa watu wanajenga majengo mazuri sana pande hizo, tofauti na huko nyuma, lakini uchawi bado ni tatizo aisee.
Utamkuta mdada ni mzuri, mzima wa afya, lakini kabla hajalala lazima aoge nyungu 3 tofauti.
Nyungu ya mawe, nyungu ya kivumbasi, nyungu sijui ya nini, ukimuuliza anakwambia kinga.
Mdada amekula chale mwili mzima, khaaa
 
IMG-20211229-WA0072.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom