_Kuna kipindi inabidi uupige mkwara umasikini. Utishie...Siyo Kila siku umezungukwa na mazingira ya ovyo._
_Piga mkwara , nenda hata hoteli ya kitalii , agiza kitu kula._
_Tembea mitaa wanayotembea matajiri, Kama akina Dewji kwa ujasiri kabisa, jidai kama tajiri. Tupa stress za Kodi japo kwa saa_.
_Ingia kwenye Kona za matajiri ili ujue raha ya kuwa tajiri._
_Nenda kaulize Bei ya Benz hata Kama hununui, uliza Bei ya Landrover Vogue_
_Fanya majaribio ya kuendesha , Kama mteja. Hakikisha unaonekana mteja. Vaa ujasiri._
_Utishie umasikini, upige mkwara wa kufa mtu ...ili umasikini ubabaike hata wanaokucheka washindwe kukuelewa Wala kujua kinachofuata._
_Kumbuka, ukifanya kitendo hiki utajenga akili kichwani itakayoleta usumbufu kwenye ufahamu wako ...utavutiwa na unaweza kuamsha mengi uliyonayo ambayo hukuyajua. Muda mwingine unaweza kukutana na watu ambao hukutegemea_
Jr