DAR: Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema mara kadhaa Rais Samia amekuwa akichafuliwa Mitandaoni lakini amekuwa kimya huku akisisitiza yasichukuliwe maamuzi yatakayowadhuru Raia
Nape amesema “Kuna jamaa fulani walimshambulia sana Rais na Familia yake kwenye Mitandao, huku ndani wakaanza kuuliza tunafanyaje? Mjadala ukawa mkubwa tuwachukulie hatua. Tukasema kwa hawa au kwa jukwaa lote lililotumika?”
Ameongeza “Lakini wakati majadiliano yakiendelea, Rais Samia aliniita na kuniambia nataka utatue jambo hili kwa busara. Nilitangaza 4R, mojawapo ni kuvumiliana, hata kama mnataka kufanya lolote, hakikisheni hamuingilii Uhuru wa Watu kujieleza."
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.