#HABARI Jeshi Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemkamata Mariam Fransisco Renatus (22) kwa tuhuma za kumuiba mtoto wa (Miezi 10) Miracle Ayoub eneo la Gongo la Mboto, Dar es Salaam na kwenda nae Geita, kijiji cha Bugalama.
Imeelezwa kuwa Mwizi huyo alijifanya msaidizi wa kazi na baadae kupata fursa ya kumuiba mtoto huyo.
Uchunguzi wa Jeshi la Polisi umebaini kuwa mtuhumiwa alimuiba mtoto huyo kwa lengo la kuwaridhisha familia ya wakwe zake baada ya kuwadanganya kuwa alijifungua mtoto tangu mwezi wa Mei, 2023 baada ya kuwa na mahusiano na kijana wao. #EastAfricaRadio
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.