Nakumbuka mwaka 2009 wakati nilipokwenda kumtembelea kaka yangu Mbeya (anafanyakazi almashauri pale mjini)....Kuna siku tulikwenda kulamba povu pendelevu (beer) kwenye bar karibu na pale almashauri. Kabla ya kufika pale kuna vinjia vya uchochoroni vya hajabu, yaani njia za mkato mpaka unafika pale bar. Nakumbuka ilikuwa kama saa mbili kasoro hivi, tukapita pale uchochoroni tukakuta pochi imejaa imetuna, nikashindwa kuikota kwa sababu nilishasikiaga habari za tego la kichawi juu ya Mbeya. Yaani mtu anakutegea kitu kama hela chini, ukiinama kuichukua unageuka kuwa mbuzi ama kuku, kisha unachukuliwa msukule kwenda kuuzwa Congo DR ama Zambia. Nikamtonya kaka, akasema ngoja aikote yeye.....kuhesabu zile pesa kukawa na laki 6 cash, na hapa tulikuwa njiani kwenda bar na shilling elfu 20 tu, hivyo tukawa na laki 6 za ziada. Ile kufika mbele tu, si chini ya mita 20 karibu na kijipori hivi, akatokezea jamaa yuko uchi huku kashika boxer mkononi anavaa akipiga kelele kaangusha pochi yake. Kusimama kumwangalia anakokwenda, akatokea demu kule kule porini alikokuwa yule jamaa, kutuona sie akashangaa na kuganda kwa mshangao huku akisema shemeji Samahani usimwambie mwenzio....tutaongea kesho, yaani yeye alikuwa mke wa rafiki wa kaka yangu alikuwa analiwa kule porini na yule jamaa. Kwa kifupi, tulichukua zile hela ila pochi tuliitupa mbele ya safari ili aione na kuiokota kwani kulikuwa na vitambulisho vyake mle.