Honey Faith
JF-Expert Member
- Aug 21, 2013
- 15,782
- 11,838
Pole sana mdada na inaonekana ulimzoesha toka zamani sasa ukianza kumsema hiki kipindi hana kazi utaambiwa unamsimanga japo unaweza kujaribu kumueleza anaweza akakusikia
Sijawahi kuwaza kwa vile hana kazi kwani najua hii kitu inaweza kumtokea mtu yoyote,
Ninachojiuliza hapa hata Kutengeneza Chai yako mwenyewe ni ngumu?
Mbali na hapo huoni mwenzio ananyonyesha mtoto anasumbua ,mama hulali hata kusema mke wangu ngoja nimsaidie hata kutandika kitanda?
ama mtoto amekaa karibu na wewe anacheza akilia unamwangalia tu?
Na nikikaa nae sasa ataona ninamsema kwa vile hana ajira ..
mmh?
Sasa mkuu we unaona suala la kutoa au kutotoa neti ni la kuleta hapa jamvini kweli? Unadhani mumewe anaiona hii post? Mshikemshike wake angeumudu? Kama hivyo unamshauri nini huyu dada kuhusu neti?
Kila mume au mke ana udhaifu wake tena pengine wa kawaida tu kama huo. Si kila kitu kina ushauri, mahali pengine unaijua tabia ya mtu wako na masuala yasiyokuwa na athari kubwa mkavumiliana. Kama kila kinachodhaniwa kuwa tatizo kitaletwa hapa hili jamvi halitakuwa na mada zingine tena.
Kuna mambo ktk ndoa unaweza kudhani ni tatizo kumbe ni tabia ya maumbile ya mtu; na hii KILA mtu anayo. Na hayo ndiyo mambo ya kuvumiliana na kukubaliana, kama mfano wa mtu mwenye wivu uliozidi. Ni lazima umjue mtu, ujue jambo fulani ni asili yake, ndipo utaweza kuishi naye. Ukisikia jubilei ya miaka hamsini ya ndoa usidhani wamefika hapo kiwepesi tu. Maisha yana milima na mabonde mengi, juaneni, vumilianeni, mtapendana na mtafika!
we mwanamke wewe leo lazima nikulime talaka urudi kwenuHivi Ladies kuolewa maana yake ni nini?
Mimi kuna vijambo vinanichosha mpaka imekuwa kero na kuona kama ndoa ni ngumu. Ni takribani mwaka mmoja na nusu sasa mme wangu kazi iliisha yupo nyumbani huku akiangaika kutafuta kazi sehemu zingine .
Hiyo sio big deal mie nafanya kazi thanks God kamshahara kangu kanasaidia kucover matatizo yote ya nyumbani ingawa sio kama tukiwa wawili. Kinachonichosha sana ni ratiba ya mme wangu.
Mimi nina watoto wawili wa kiume mmoja 5 years na mwingine 9 month. Mme hata mtoto akiwa analia eti yeye hawezi kumbembeleza anamwangalia tu ukimuuliza anasema yeye amfanyeje wakati hana maziwa ya kumnyonyosha, mimi hapa usiku silali mtoto anasumbua asubuhi kuamkia kazini, jioni kufika kumwangalia mtoto na kuandaa maakuli ya familia.
Nina binti anaenisaidia nikiwa kazini. Lakini mme anaamka saa nne kitanda hagusi kutandika mpaka nitoke kazini nakikuta hivyo hata net haijatolewa kutandika ndio basi tena pia hata akivua nguo za ndani atarundika hapo nije kufua mie.
Anapiga mswaki na kukaa kwenye kochi kusubiri atengenezewe chai na apelekewe, atabadilisha chanel mpaka lunch atakula atabadilisha Chanel zake baadae anawasha gari kwenda kutembea. Saa mbili au saa tatu atarudi atakula atakamata tena remote mpaka saa sita ataingia kulala na ukali sasa kitu kidogo tu manung'uniko.
Hivi jamani wanaume mkioa kazi yenu huwa inakuwa kutoa matumizi ,kula na kulala tu?
Hakuna mnachoweza kusaidia?
Ladies hivi wote mko kwenye hali hii??
Last week nilikuwa naosha Vyombo ,akaniita mama F naomba unitengenezee coffee akiwa ameshika remote anaangalia TV
Nikamwambia naosha vyombo my dear ila kila kitu kipo mezani please nisaidie kutengeneza wala hakunyanyua mguu anasubiri nikatengeneze ,na hapo mtoto nimeweka mgongoni wangu alikuwa mgonjwa
Nikatengeneza kikombe chake nikampa akasema asante basi
Wewe mwanamke your selfish
Hivi Ladies kuolewa maana yake ni nini?
Mimi kuna vijambo vinanichosha mpaka imekuwa kero na kuona kama ndoa ni ngumu. Ni takribani mwaka mmoja na nusu sasa mme wangu kazi iliisha yupo nyumbani huku akiangaika kutafuta kazi sehemu zingine .
Hiyo sio big deal mie nafanya kazi thanks God kamshahara kangu kanasaidia kucover matatizo yote ya nyumbani ingawa sio kama tukiwa wawili. Kinachonichosha sana ni ratiba ya mme wangu.
Mimi nina watoto wawili wa kiume mmoja 5 years na mwingine 9 month. Mme hata mtoto akiwa analia eti yeye hawezi kumbembeleza anamwangalia tu ukimuuliza anasema yeye amfanyeje wakati hana maziwa ya kumnyonyosha, mimi hapa usiku silali mtoto anasumbua asubuhi kuamkia kazini, jioni kufika kumwangalia mtoto na kuandaa maakuli ya familia.
Nina binti anaenisaidia nikiwa kazini. Lakini mme anaamka saa nne kitanda hagusi kutandika mpaka nitoke kazini nakikuta hivyo hata net haijatolewa kutandika ndio basi tena pia hata akivua nguo za ndani atarundika hapo nije kufua mie.
Anapiga mswaki na kukaa kwenye kochi kusubiri atengenezewe chai na apelekewe, atabadilisha chanel mpaka lunch atakula atabadilisha Chanel zake baadae anawasha gari kwenda kutembea. Saa mbili au saa tatu atarudi atakula atakamata tena remote mpaka saa sita ataingia kulala na ukali sasa kitu kidogo tu manung'uniko.
Hivi jamani wanaume mkioa kazi yenu huwa inakuwa kutoa matumizi ,kula na kulala tu?
Hakuna mnachoweza kusaidia?
Ladies hivi wote mko kwenye hali hii??
Hiyo red hapo imeonyesha weledi wako,,,ni facts! ila huyu bidada kwann ameliingiza hili la kutokuwa na kazi kwa mmewe, kwani angesema jamani mme wangu yuko hivi na hv nishaurini nimbadilishe....anatakiwa kuelewa mmewe yuko kwenye wakati mgumu mno na yeye ndo mfariji pekee...so aache mbwembwe na kufikiria hasi zaidi.