Vitu vinavyonikera ndani ya ndoa

Vitu vinavyonikera ndani ya ndoa

hii point uneshaisema mara nyingi, 'kuoana ndio muoane', sijui kama unaeleweka.

Lakini ndoa bila wenza 'kuoana' ni majanga.

Tatizo hapo ni kuwa umeolewa. Ingekuwa mmeoana kusingetokea tatizo kama hilo.

Tatizo lingine, ni pale mume anapokuwa mwizi akiwa kazini, akiachishwa kazi maisha yanakuwa magumu X 3.

Ukiona mwanamme mvivu namna hiyo ujuwe ni mvivu kazini pia na mvivu bedroom. Kwa situation kama hiyo usitegemee kama kuna ufumbuzi wowote utapatikana, hicho ndio kichocheo kikubwa cha wewe kutembea nje ya ndoa kama bado hujaanza mpaka leo.
 
Hapo issue ni kuwa jamaa sasa kawa mzigo maana kama hizo tabia nina uhakika hazijaanza leo lkn ukawa unamvumilia sababu na yy anachangia tena labda zaidi kwenye pato la familia!

Jamaa kachokwa sababu haleti chochote home kuchangia na hii ndiyo zenu madada wengi!Yalinikuta kama haya nilifukuzwa kwa kuitwa "mbweha"usiku wa manane miezi 7 baada ya kupoteza kazi ehehehehe

inategemea na m/ke last year mwenza wangu hakua vizur kibiashara yani mimi ndo nlitake responsibilities zote ila sikuwahi kumfanya chochote kibaya wala kumdharau na alikua anashnda home ila mimi nkirudi nifanye kazi zote na sikuwahi kumsemanga mpaka aliporevival MUNGU WANGU shahidi yangu
 
aissshh! alipokuwa anafanya kazi ulikuwa na manung'uniko haya?
 
Last week nilikuwa naosha Vyombo ,akaniita mama F naomba unitengenezee coffee akiwa ameshika remote anaangalia TV

Nikamwambia naosha vyombo my dear ila kila kitu kipo mezani please nisaidie kutengeneza wala hakunyanyua mguu anasubiri nikatengeneze ,na hapo mtoto nimeweka mgongoni wangu alikuwa mgonjwa

Nikatengeneza kikombe chake nikampa akasema asante basi

nlishakutwa na situation km yako last year ila mi hata haikunipa shida kwa sababu nlishamzoesha toka mwanzo maisha ya mimi kufajya kazi zote ye ametulia tuli so mi nlikua nachukulia poa tu japo sometimes unachoka ila kikubwa alichokua ananiambia pole na majukumu ila hakua ananosaidia chochote na mi binafsi wala sikuwahi kumuuliza au kumnunia
 
Sio sawa.
Ila ndio malezi aliyolelewa.
Unachotakiwa kufanya ni kujua madhaifu ya mumeo na kuyakubali kutoka vilindi vya moyo wako. Niamini ukiyakubali madhaifu yake utaona maisha rahisi sana.

Maana utamhudumia kwa moyo mkunjufu hata kama anashinda na remoti.

Ila swala la malezi mketishe chini. Afanye jukumu lake kama baba. Watoto wanahitaji ukaribu wa baba na malezi yake.

Ila ukirudi job tandika tu kitanda.
Muandalie chai na huduma nyingine....

Hilo ni lako libebe tu






jamani hivi kweli ni sawa unaamka asubuhi unamwacha amelala unarudi jioni hata net haijatolewa hiyo ni sawa??mmmh
 
Pole sana mdogo wng ila jambo lililo zuri na bisara jitahidi umeeleze kuhusu tabia yeke kuwa uhifurahii pia nakusii zungumza naye taratibu (inaonyesha hajuwi dhamani yako huyo)

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
inategemea na m/ke last year mwenza wangu hakua vizur kibiashara yani mimi ndo nlitake responsibilities zote ila sikuwahi kumfanya chochote kibaya wala kumdharau na alikua anashnda home ila mimi nkirudi nifanye kazi zote na sikuwahi kumsemanga mpaka aliporevival MUNGU WANGU shahidi yangu

Mwenzako anamuona jamaa mzigo sababu hana kazi!Angekuwa na kazi hata kama angekuwa hambebi mtoto angevumiliwa tu ahahahaha
 
we umechoka ndoa... tuvitatizo tudogo kama uto unakuja kulia huku!!!! wenzio wanapgwa kila siku au hawaachiwi hela ila wameuchuna.... ngoja akutafutie msaidizi aweke ndani ushike akiri
 
Huyu mleta mada hajakuwa wazi sana kuhusu mazingira yote ya ndoa yake. Hata hivyo hapa hapakuwa mahali muafaka sana pa kukimbilia, ilikuwa kwanza waongee wenyewe ikishindikana ndio achukue hatua zingine

Ndiyo ndoa za siku hizi usipoleta kitu home anakuhesabia siku!Mm ishafukuzwa mara 2 tena usiku wa manane baada ya kuishiwa ili hali wkt nina pesa walionyesha mapenzi ya kweli!!
 
Hivi nyie wanaume kweli hauwezi kufika kipindi uone mkeo kazidiwa na wewe upo hata kumsaidia tu kuweka chai kwenye Kikombe ni ngumu?
Hata kufua nguo zako za ndani ni kazi??
Mie sijasema aje kuosha vyombo no..basi wakati mie nadeki na kupika kuna ugumu wa kufua Boxer zako mwenyewe?
Kutoa net Kitandani na kuweka shuka vizuri ni kazi??

Bado naona una tatizo zaidi ya hapa. Kwani hapa unazungumzia wanaume wangapi, si mumeo tu?

Mimi huwa nampikia mke wangu, naweza hata kumuandalia maji ya kuoga, nahakikisha usiku nimemuwekea neti na kumfunika vizuri, nk, lakini hayo ni mambo ya mapenzi tu na si wajibu. Na hii inategemea sana mfumo wa mapenzi wa pande mbili. Chunguza nyumba yako zaidi.

Nakusihi tena, mambo ya ndani sana hivi usipende kuyatoa hadharani sana, labda ikibidi. Hapa unaona boxer za mumeo zinatuhusuje? Mimi mke wangu hunifulia siku zote na bado tunapendana na kuheshimiana sana. Kumfulia mumeo boxer na kumtayarishia kahawa si dalili kwamba mume ana mfumo dume, inaweza pia kuwa namna ya yeye kutambua uwepo wako. Mapenzi yana sura nyingi, msome mumeo zaidi.
 
Mwenzako anamuona jamaa mzigo sababu hana kazi!Angekuwa na kazi hata kama angekuwa hambebi mtoto angevumiliwa tu ahahahaha

Mimi naona kama mkuu unaenda mbali sana, hebu rudi tu nyuma kidogo, kutoa neti kitandani ukaitupia juu inajalisha kama una kazi au huna? Mbona mimi naona kama nikitu kidogo sana ambacho wala hakiwezi kuudhalilisha 'uanaume'?
 
Sijawahi kuwaza kwa vile hana kazi kwani najua hii kitu inaweza kumtokea mtu yoyote,
Ninachojiuliza hapa hata Kutengeneza Chai yako mwenyewe ni ngumu?
Mbali na hapo huoni mwenzio ananyonyesha mtoto anasumbua ,mama hulali hata kusema mke wangu ngoja nimsaidie hata kutandika kitanda?
ama mtoto amekaa karibu na wewe anacheza akilia unamwangalia tu?
Na nikikaa nae sasa ataona ninamsema kwa vile hana ajira ..
mmh?

Dah! Kusema kweli mtihani!
But don give up ktk kutafuta suluhu (nna uhakika suluhu ipo tena ya amani save kuachana!) Jaribuni hata kuwashirikisha wazee!
 
Hivi nyie wanaume kweli hauwezi kufika kipindi uone mkeo kazidiwa na wewe upo hata kumsaidia tu kuweka chai kwenye Kikombe ni ngumu?
Hata kufua nguo zako za ndani ni kazi??
Mie sijasema aje kuosha vyombo no..basi wakati mie nadeki na kupika kuna ugumu wa kufua Boxer zako mwenyewe?
Kutoa net Kitandani na kuweka shuka vizuri ni kazi??

Eheee!! Hapo umenena!! Halafu usiseme nyie wanaume coz huyo ni wako na ulimchagua kwa mapenzi yako mwenyewe!! Nimekuuliza swali kuwa tabia hiyo alikuwa nayo tangu mpo wachumba au ameanza baada ya kupoteza kazi??
 
Mimi naona kama mkuu unaenda mbali sana, hebu rudi tu nyuma kidogo, kutoa neti kitandani ukaitupia juu inajalisha kama una kazi au huna? Mbona mimi naona kama nikitu kidogo sana ambacho wala hakiwezi kuudhalilisha 'uanaume'?

Sasa mkuu we unaona suala la kutoa au kutotoa neti ni la kuleta hapa jamvini kweli? Unadhani mumewe anaiona hii post? Mshikemshike wake angeumudu? Kama hivyo unamshauri nini huyu dada kuhusu neti?

Kila mume au mke ana udhaifu wake tena pengine wa kawaida tu kama huo. Si kila kitu kina ushauri, mahali pengine unaijua tabia ya mtu wako na masuala yasiyokuwa na athari kubwa mkavumiliana. Kama kila kinachodhaniwa kuwa tatizo kitaletwa hapa hili jamvi halitakuwa na mada zingine tena.

Kuna mambo ktk ndoa unaweza kudhani ni tatizo kumbe ni tabia ya maumbile ya mtu; na hii KILA mtu anayo. Na hayo ndiyo mambo ya kuvumiliana na kukubaliana, kama mfano wa mtu mwenye wivu uliozidi. Ni lazima umjue mtu, ujue jambo fulani ni asili yake, ndipo utaweza kuishi naye. Ukisikia jubilei ya miaka hamsini ya ndoa usidhani wamefika hapo kiwepesi tu. Maisha yana milima na mabonde mengi, juaneni, vumilianeni, mtapendana na mtafika!
 
pole sana mdada....
mwanaume wako hukumsoma alam zanyaati wakati wa urafiki na uchumba wenu kma ungekuwa makin hizi tabia ungzijua

kuna wanume wasafi na wapenda watoto ile mbaya,..kumsaidia mkewe kazi ....

vumilia tu kwa maana ukiongea sana na kazi hana utaleta ugomvi
 
Stress zinamfanya nini mtu?
Je mwanamke nae akiwa na stress awe hivyo?
Hiyo ni tabia tu ya mtu kiukweli.
Hata kama una stress ukikaa na mtoto na kucheka nae stress zinapungua.

Naamini wewe ni muelewa, stress unaijua vizuri?? Ubaya wa stress inaweza kuangukia sehemu ambayo unaona ni chimbuko la tatizo mfano kama huyu anaweza kuwa anaona familia ni mzigo sababu hana kazi na ndoto zake zimezimika, sijui umenielewa hapo!! Anaweza kuwa amechukia familia yake yote na kila kitu bila kujua chanzo ni nini na wengine ndiyo huishia kuwa walevi!!

Pata picha mjamzito anapotokea kumchukia mumewe, unaweza kusema anajifanyisha lakini ndiyo mambo ya ujauzito! Ni hivyo hivyo kwenye stress

Ndiyo maana nikauliza tabia hii alianza nayo toka mwanzo akiwa na kazi au imeibuka baada ya kupoteza kazi?? Kama imeibuka baada ya kupoteza kazi basi ni stress za kupoteza kazi hizo

Swala hapa siyo mwanamke au mwanaume, tunaangalia chanzo cha tatizo!! Keshasema mumewe hana kazi so usikurupuke kulaumu utajikuta unaharibu badala ya kujenga!! Mwanaume kutokuwa na kazi ni ishu nyingine sana heri mwanamke asiwe na kazi ila mumewe awe na kazi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom