Hapa tukiangalia juu juu tunaweza kutoa ushauri mbovu wa kuharibu ndoa! Nawashauri wadau msichukulie poa poa sana!
:focus:
Kitendo cha kusema hana kazi na mambo yote unafanikisha wewe, huo sio uungwana! Mwenyewe si umesema kama anahangaika kutafuta?
Naamini hayo manung'uniko yako yamerise kwa kasi kubwa baada ya kuona masuala ya misosi unafanikisha wewe! Unataka malipo kana kwamba naye achukue jukumu lako! Naamini akiosha vyombo utafurahia kitu ambacho si kizuri!
Hizo kazi unazonung'unikia hapo ni wajibu wako wa msingi!
Nakubaliana nawe 100% kwamba mapenzi ni kusaidiana! But unahitajika kuwaza zaidi ya hapo! Kitendo cha kufukuzwa/kusimamishwa/kuacha kazi kimeathiri huyo mmeo! Kisaikologia ana adjustment disorder! Unatakiwa kumpa moyo na kumfariji na sio kumnung'unikia tu!
Nna uhakika huyo mme anakupenda sana!
In nature kuna me hawapendi kufanya kazi ulizojitaja especially wanapokutwa na majanga eg: kufukuzwa kazi!
Huenda huyo mmeo anajiuliza hivi: "Kwa kua sina kazi, na kwa vile mkewa wangu ana kazi na anawajibika, jee fact hizo zinifanye nifanye kazi za kike? How if ikiwa ni ubushoke? Kwanini kufukuzwa kazi iwe sababu ya kuondoa amani yangu!
...
Nakushauri kaa naye chini uongee naye kwa upendo, acha kumlalamikia sana! Malalamiko hayajengi yanabomoa tu! Naamini na nitaendelea kuamini kwamba ukifanya hivyo mtaishi kwa amani!
...
Waweza pita na hapa huenda ukajifunza kitu:
https://www.jamiiforums.com/mahusiano-mapenzi-urafiki/696522-makundi-manne-ya-binadamu.html
Wish you all the best!