Kwa hiyo jpm Jana amekurupuka na yy kushangaaa hakuna signature ssa hivi hanaga washauri ,tukisema anajifungia mwenyewe anakuja kuongea hata asilojua kujifanya unajua kila kitu utaumbuka,namuonaga hata sefue akisoma mateuzi yake usoni hana Amani kabisa,kukumbusha ni kwamba nida tulipeleka mavyeti ya shule,ya kuzaliwa,maleseni ya magari na hata kadi za kura na walichukua muda kuhakiki taarifa.Sasa ile kadi ya lubuva tulienda bila id yoyote unaulizwa jina,ulipozaliwa mwaka na tarehe wanaingiza ktk database hivi nani hapo atakuwa na taarifa sahihi kama sio nida so jpm asimsifu lubuva kwa kuwa alimbeba aangalie ukweli sitetei matumizi mabaya ila facts tuziongee
Meta Stress Free Zone
Tusiwe washabiki wa mambo tusiyoyaelewa,tatizo lililopo ni kuwa uelewawa wa watanzania kuhusu national ID ni mdogo.Id haikutengenezwa kwa minajili ya kusomwa kama kadi zilizozoeleka mfano bima ya afya,voters ID.
National ID ina content ya taarifa zote za mwananchi na ni taarifa nyingi kuliko ID yeyote katika taifa letu.Kilichopo ili uweze kuziaccess taarifa za kitambulisho cha taifa ni lazima uwe umeunganishwa katika mfumo wa mamlaka hapo ndio unapata kitu kinaitwa wadau wa kitambulisho cha taifa mfano mabenki,tra,bodi ya mikopo na taasisi mbalimbali ambazo zinahitaji kupata taarifa kwa matumizi mbali mbali.
Hivi sasa mabenki katika mkoa wa Dsm wanasisitiza kutumia national ID kwakuwa wameshapewa elimu,wameunganishwa na mfumo wameona umuhimu wa taarifa zilizopo ambapo biometric finger prints iliyomo ndani ya national ID ni feature kubwa zaidi ya signature ambayo mtu yeyote anaweza akaiguess iwapo kama sahihi ya nje ikiwa ndio kigezo.
Namba nne katika national ID ni mwaka wako wote na tarehe yake,
Inayofuatia mfano 12105 ni postcode ya eneo husika mfano tabata,namba zinazofuatia mfano 00004 ni namba yako katika mtaa husika kwa watu wenye Mwaka kama wako.namba mbili za mwisho ni unique namba ya mmiliki Wa ID.
Tatizo lililopo elimu haijatolewa ya kutosha ili watu wapate uelewa.
19841213121050000512 mfano Wa namba hiyo ndio kielelezo cha maelezo yaliyotolewa juu.
Kuhusu expire date inatumika ili kuja kuapdate taarifa za muombaji.
Kwakifupi naamini tutapata mwanga.
Ni kweli mkuu unayonena..National ID za nchi nyingi zipo hivyo kimfumoMeta Stress Free Zone
Tusiwe washabiki wa mambo tusiyoyaelewa,tatizo lililopo ni kuwa uelewawa wa watanzania kuhusu national ID ni mdogo.Id haikutengenezwa kwa minajili ya kusomwa kama kadi zilizozoeleka mfano bima ya afya,voters ID.
National ID ina content ya taarifa zote za mwananchi na ni taarifa nyingi kuliko ID yeyote katika taifa letu.Kilichopo ili uweze kuziaccess taarifa za kitambulisho cha taifa ni lazima uwe umeunganishwa katika mfumo wa mamlaka hapo ndio unapata kitu kinaitwa wadau wa kitambulisho cha taifa mfano mabenki,tra,bodi ya mikopo na taasisi mbalimbali ambazo zinahitaji kupata taarifa kwa matumizi mbali mbali.
Hivi sasa mabenki katika mkoa wa Dsm wanasisitiza kutumia national ID kwakuwa wameshapewa elimu,wameunganishwa na mfumo wameona umuhimu wa taarifa zilizopo ambapo biometric finger prints iliyomo ndani ya national ID ni feature kubwa zaidi ya signature ambayo mtu yeyote anaweza akaiguess iwapo kama sahihi ya nje ikiwa ndio kigezo.
Namba nne katika national ID ni mwaka wako wote na tarehe yake,
Inayofuatia mfano 12105 ni postcode ya eneo husika mfano tabata,namba zinazofuatia mfano 00004 ni namba yako katika mtaa husika kwa watu wenye Mwaka kama wako.namba mbili za mwisho ni unique namba ya mmiliki Wa ID.
Tatizo lililopo elimu haijatolewa ya kutosha ili watu wapate uelewa.
19841213121050000512 mfano Wa namba hiyo ndio kielelezo cha maelezo yaliyotolewa juu.
Kuhusu expire date inatumika ili kuja kuapdate taarifa za muombaji.
Kwakifupi naamini tutapata mwanga.
Kwa namna MAGUFULI alivyoongea Juzi.....Pamoja na kumuunga Mkono RAIS wangu...lakini naona tunayo safari Ndefu Sana .....ILE hotuba anayeweza kuishangilia NI Mtu ambaye hajaenda shule ....NI aibu KUWA hotuba ILE imetolewa Mbele ya Majaji ...ingetolewa pale Jangwani wala nisingeshsngaa
Kama RAIS kuna lugha stahiki kuongea Mbele ya kila hadhira .....Iwe kwenye kampeni,Mbele ya mabalozi, ( kwanza hadi Sasa hajaandaa state house cherry ..kusherekea mwaka mpya na mabalozi) ...Mbele ya wanasheria ...kuna maeneo hutegemewi kutoa hotuba kwa hisia ...PENGINE alikuwa na hotuba iliyoandaliwa ...namshauri kwenye formal events wasaidizi wake wahakikishe anasoma hotuba Yake .....hata marais wenye akili Kama Obama hawezi kuongea na Baadhi ya makundi bila kusoma hotuba.....maana kosa au sentensi moja tu UNAWEZA kuharibu kila kitu na ikawa scandal ..
Namshauri watu wa mawasiliano Ikulu wasitishe kuirusha ile hotuba ...maana inaenda Kuleta mjadala mkali Sana KUANZIA kwa Wasomi...na watu wa kawaida wanaweza kuelewa
hapa ndio niliuliza hivi katika zile gharama zilizotajwa zimetumika je ?Hizo id hazina shida, shida n kwamba zimetumika hela nyingi kwa id chache
Napingana na wewe. Hotuba ya Magufuli ilikuwa nzuri sana, tena sana. Amesema ukweli bila kuremba maneno. Tatito Watanzania tumezoea kusikia yale tunayotaka halafu kesho yake tunaanza kulalamika tumedanganywa. Ifike mahali mkuu wa nchi atueleze mambo kwa uwazi na ukweli hata kama ukweli huo ni mchungu lakini walau tutakuwa tunajua ndio ukweli na tutafute tiba yake.
Ingekuwa hotuba ya Magufuli ni ya kuremba maneno kuna uwezekano watu wasingekuwa wanakumbuka karibu nusu kama si yote aliyoyasema. Lakini aliongea kama (a) Mtanzania anayeguswa na utendaji mbovu kwenye public sector na (b) kama kiongozi mwenye dhamana ya kurekebisha utendaji huo mbovu. Sasa hivi akichukua hatua wananchi wanajua where is coming from.
Nashawishika kusema watu wengi wanapinga hotuba ya Magufuli kwa sababu wana maslahi na mambo aliyotaja. Mfano hizo kesi 400 za wakwepa kodi!
mahakama nazo zisiweke mazingira ya rushwa. kila kukicha kesi zinaahirishwa kwa sababu za kitoto sana! huu ni uzembe na kuandaa mazingira ya rushwaHEKIMA KWANZA;
Laiti kweli ungekuwa na hekima kwanza. Hivi weye hukuona kuwa JPM alikuwa anahalalisha jipu lake alilotumbua kule NIDA? Alikuwa anataka asiseme alikosea kumtumbua Maimu tu. Hivyo vitambulisho hata kama vilikuwa vimetengenezwa na "Fala" asingekuwa mjinga kiasi hicho awe amekula mihela yoote hiyo, awe amewapa wakuu vitambulisho vyao, halafu nao wasione hizo hitilafu zote.
Kuhusu kesi za mihela lukuki, kuiambia mahakama ifanye chap chap ili awape robo ya hiyo mihela, NASEMA; Alikosea. Hukumu ikiharakishwa bila uangalizi nayo ni haki ilio uliawa. Hatutaki ichukue miaka, ila isiwe fasta. Itaua haki za watu. Je, ikijagundulika baadaye kuwa haki haikutendeka kama ile issue ya meli za samaki wa magufuli, hiyo hasara itabebwa na nani??
Aiache mahakama itende haki kwani ndo chombo pekee tunacho tumainia.
mahakama nazo zisiweke mazingira ya rushwa. kila kukicha kesi zinaahirishwa kwa sababu za kitoto sana! huu ni uzembe na kuandaa mazingira ya rushwa
Hata benki za Manzese hazikitambui,mwaka wako wa kuzaliwa upo ndio code ya kitambulisho chako anagalia zile namba za kitambulisho chako zinaonyesha siku,mwezi na mwaka uliozaliwa zimeunganishwa kwapamoja,mengineyote uliyosema ni kweliMimi ni mmoja wa Watanzania mwenye kitambulisho cha taifa ambaye hotuba ya Rais jana kufungua mwaka wa Mahakama imenigusa. Nimekiangalia kwa umskini, kinakosa sifa zote za "smart card" kama ifuatavyo:
1) Hakina nembo ya siri kama vike vya "road licence" na "kupiga kura".
2) Hakina mwaka wangu wa kuzaliwa kuthibitisha nina unri gani mimi Mtanzania.
3) Hakina sahihi yangu kuthibitisha hiyo picha na mimi niliye nayo ni changu.
4) Kina mwaka wa kikomo kwamba mimi Utabzania wangu utakoma hiyo siku hadi niombe upya!!!
TUTAFAKARI TUCHUKUE HATUA