Vita ya Urusi na Ukraini inaendelea mashariki ya kati.

SUTAGI-

JF-Expert Member
Nov 9, 2018
269
511
Wenye nguvu huiongoza dunia na kuamua namna wanavyotaka.

Ili uwe na nguvu, uheshimike na uogopeke, lazima uwe na matumizi sahihi ya akili.

Matumizi sahihi ya akili huzaa mipango sahihi ambayo humfanya binadamu acheke na Mungu.

Kwa muda mrefu sana Marekani ilijinasibu kama taifa kubwa, na hilo halipingiki. Taifa kubwa na imara linahitaji mshindani aliye imara na mkubwa pia.

Mshindani mkubwa wa Marekani na aliyewahi kumtunishia misuli na ataendelea kuwa imara dhidi ya Taifa hilo ni Urusi.

Marekani alitumia ukaribu wake na Ukraine kumdhoofisha Urusi.. lakini Urusi alisimama kidete kuhakikisha kuwa analinda hadhi yake na kuonesha uwezo wake wa vita katika dunia hii.

Urusi inapigana vita nyingi tusizoziona dhidi ya Marekani, na kwa sasa kama Marekani alivyomtumia Ukraine dhidi ya Urusi sasa huenda Urusi alimtumia Hamas kudhoofisha juhudi za Marekani kuisapoti Ukraine.

Ni kwa mipango hiyo ya wababe hao wa Dunia, kwamba hadi leo Marekani amehamisha fikra zake na pesa toka kuiwezesha Ukraine hadi Israeli. Kwa muda huu Urusi anayo kazi nyepesi sana kuitindua Ukraine atakavyo.

Ni matumaini yangu kuwa mwendelezo wa vita ya Urusi Vs Ukraine, vita ya Israel Vs Hamas zitaendelea kuzaa vita nyingi zikiwemo za kiuchumi hadi pale litakapoibuka taifa jingine litakalokuwa na nguvu sawa au zaidi ya Marekani.

Sisi tusiokuwa na matumizi sahihi ya akili tuendelee kuomba huruma za Mungu ili tusijekumbwa na mwendelezo wa vita hizo huku kwetu machakani.

Sent from my TECNO KA7O using JamiiForums mobile app
 
Umejaribu kufikiri lakini fikra zako sio sawa. Israel kupigana na wanamgambo wa Hamas hiki ni kikundi kidogo mno. Labda kama angeingia kwenye vita na nchi kama Iran, Yurkey na Misri. Hapo Marekani angevurugwa haswa. Sio hamas ambao wanapatikana kwenye eneo dogo, tunaambiwa lina ukubwa wa wilaya ya Bagamoyo.

Ingekuwa nchi kwa nchi ningekuelewa.
 
Njia pekee ya Urusi kufanikiwa katika hilo ulisemalo, ni kuhakikisha Hizbollah wanaingia kwenye hiyo vita... Hapo kwa kiasi fulani USA anaweza kuingia hasara kubwa maana itailazimu Israel kuingia Jordan na itakues rahisi kuifanya Jordan kuwa proxy kupitia Iran na Syria na inaweza kuipa taabu Israel maana wapiganaji wengi wataingia kutokea Afghanistan, Yemen na nk na hata Urusi kupenyeza wapiganaji hasa kutokea Chechnya na hapo ndio hatari kwa USA na Israel inaweza kuwa kubwa lakini kwa kuisacrifice Jordan kama West na USA walivyoamua kuisacrifice ukraine.
 
Sio kwamba vita ya Ukraine ndio ilianzishwa ili kumkeep Russia bz ili watu wakiingia middle East wafanye yao bila kikwazo.

Naona mchina na yeye katupiwa pumba ya mazungumzo na yeye katulia tuli na sasa Israel anafanya yake na mwarabu yeyote atakayesogeza kanzu yake anashuhulikiwa fasta na maisha yanaendelea.

Wata wanamipango na katu hawakurupuki
 
ila vita sio poa, raia wa gaza na wa ukraine wanatesekaq sana, nadhani viongozi kabla ya kuingia vitani wapime faida na hasara... ateast kwa ukraine naweza kuelewa maana RUSSIA aliianzisha na alikiwasha UKRAINE Yote kabla hajabadilisha malengo na kuamua kukomaa na mikoa ile minne,hivyo UKRAINE hakuwa na option ila huko gaza, HAMAS wamekurupuka kama wamekalia upupu,leo gaza imegeuka vifusi, bora ile amani kidogo waliyokuwa nayo na maisha yalikuwa yanaendelea, kuliko sasa hivi hata maisha yenyewe hamna.
makosa ya viongozi, yanawaumiza raia.
 
Njia pekee ya Urusi kufanikiwa katika hilo ulisemalo, ni kuhakikisha Hizbollah wanaingia kwenye hiyo vita... Hapo kwa kiasi fulani USA anaweza kuingia hasara kubwa maana itailazimu Israel kuingia Jordan na itakues rahisi kuifanya Jordan kuwa proxy kupitia Iran na Syria na inaweza kuipa taabu Israel maana wapiganaji wengi wataingia kutokea Afghanistan, Yemen na nk na hata Urusi kupenyeza wapiganaji hasa kutokea Chechnya na hapo ndio hatari kwa USA na Israel inaweza kuwa kubwa lakini kwa kuisacrifice Jordan kama West na USA walivyoamua kuisacrifice ukraine.
Wameisacrifice vp ukraine
 
Sio kwamba vita ya Ukraine ndio ilianzishwa ili kumkeep Russia bz ili watu wakiingia middle East wafanye yao bila kikwazo.

Naona mchina na yeye katupiwa pumba ya mazungumzo na yeye katulia tuli na sasa Israel anafanya yake na mwarabu yeyote atakayesogeza kanzu yake anashuhulikiwa fasta na maisha yanaendelea.

Wata wanamipango na katu hawakurupuki
Nani alianzisha vita vya ukraine ili kumkip bize mrusi
 
ila vita sio poa, raia wa gaza na wa ukraine wanatesekaq sana, nadhani viongozi kabla ya kuingia vitani wapime faida na hasara... ateast kwa ukraine naweza kuelewa maana RUSSIA aliianzisha na alikiwasha UKRAINE Yote kabla hajabadilisha malengo na kuamua kukomaa na mikoa ile minne,hivyo UKRAINE hakuwa na option ila huko gaza, HAMAS wamekurupuka kama wamekalia upupu,leo gaza imegeuka vifusi, bora ile amani kidogo waliyokuwa nayo na maisha yalikuwa yanaendelea, kuliko sasa hivi hata maisha yenyewe hamna.
makosa ya viongozi, yanawaumiza raia.
Umenena sikujua kwanini hamas walikurupuka vile nafikiri iran iliwadanganya
 
Wameisacrifice vp ukraine

Target kuua ya USA na NATO ni kuidhoofisha Urusi kwa gharama ya kuiharibu UKRAINE.

NATO na USA wanajua kabisa kutimiza lengo lao la kuimaliza kabisa Urusi ni lazima Ukraine ibaki magofu, watu wengi wafe ukraine nk... japo wanajua kwa gharama zao wanaweza kuijenga upya Ukraine.

Kulikuwa hakuna ulazima wa Vita kama Ukraine angebaki neutral bila kuside na upande wowote kwa maana abaki kuwa Uraine sio Nato wala Russia.
 
Huwa hakuna vita ndogo.. Distortion inayofanyika Israel na Palestina ni kubwa sana, chanzo ni hao unaowaita wanamgambo.

Ku_breach ulinzi imara wa Israel siyo jambo dogo.. so hao jamaa usiwaone wadogo.

Vita inayoendelea ni pigo kubwa kwa amani ya mashariki ya kati pia inaongeza chuki ya mataifa mengi dhidi ya Marekani.

Sent from my TECNO KA7O using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom