Mama wa vita vyote (mother of all battles) yuko CCM. Hii vita haina mshindi na lazima itakirarua chama. Mamvi ameweka jeshi lake imara na anazo silaha za kisasa kabisa kupambana na fitna zote dhidi yake. Kwa upande mwingine joka la mdimu baada kuona jeshi lake linaelemewa na lile la mamvi ameamuamua kuunda alliance na wababe wengine WA kivita akina six na wenzake ambao wamepeleka wanamgambo wao kwenda kupigana sambamba na jeshi la joka la mdimu.Silaha zinazotumika kwenye vita hii ni rushwa,vyombo makanjanja vya habari,ushirikina,viongozi njaa wa dini,pesa chafu kama za escrow,kuchafuana na Hata silaha za sumu. Inasemekana Hata kamanda wa majeshi ya mamvi mzee wa msituni aliyefariki dunia ghafla hivi karibuni alipewa sumu na majasusi wa vikosi vya joka la mdimu.Propaganda kwamba CHADEMA au UKAWA kuna vita si za kweli ila maccm wanataka kuficha vita vinavyoendlea kwenye chama chao.