Virusi vya korona vyaja kivingine!

Virusi vya korona vyaja kivingine!

hatarii cha muhimu uingereza ni kufunga mipaka ili virus wasiendelee kusambaa ulimwengunii
 
Wakati Dunia inapata matumaini ya kudhibiti virusi vya korona baada ya kuidhinishwa chanjo kadhaa, hali ya sintofahamu imeukumba ulimwengu na Sayansi ya utafiti baada ya aina mpya ya virusi vya korona kugunduliwa nchini Uingereza ambayo inaambukiza kwa haraka zaidi ya aina ya kwanza hivyo kutia shaka kuwa hatua zilizopigwa kwenye kupata chanjo zikawa kazi bure!!

Kitaalamu aina hii mpya imetokea baada ya virusi vya korona kubadilika kutoka umbo la awali na kutoa kirusi chenye sehemu za mwili tofauti(new variant). Wataalam wanasema baadhi ya mabadiliko yaliyotokea ni pamoja na kujibadili sehemu inayotumika na kirusi kunasa katika seli ya binadamu, mbaya zaidi ni kuwa chanjo zilizopo zinafanya kazi kwa kuwezesha kinga ya mwili kushambulia sehemu hii ya kirusi inayonasana na seli ya binadamu!! Sasa kwa kubadili umbo hapo itabidi utafiti upya kufanyika kupata chanjo inayoweza kukabili umbo husika!!

Nchi nyingi za Ulaya na sasa India zimezuia usafiri kutoka Uingereza ili kujikinga na aina hii mpya ya virusi vya korona!

Mungu atusaidie sana!

Chanzo: BBC NEWS
Tanzania HATUNA corona
 
Kirusi mpya ameenda kuibukia palepale chanjo ilikoanzia.

Hii ni kawaida sana sijui kwa nini hawa wanaojifanya wana akili sana hawakuliconsider hili, ama ni kutuchezea akili tuu.

Yani ni kwamba tabia za kirusi kikiona kuna sintofahamu kinaletewa basi kinajibadili na kutoa aina iliyo madhubuti zaidi ya ile ya kwanza (mutation). Hii ndio tunaiita tembo aliyejeruhiwa sasa, hasira zake zinakuwa next levels[emoji1783]

Nadhani imefika wakati hawa wenzetu wakubali kumuangamiza huyu kirusi kwa conservative methods, waachane na mambo ya chanjo maana wanaweza zalisha bomu la dunia.
Unforgetable
 
Yani mwenzenu nikionaga hizi nyuzi za Corona naishiwa pozi kabisa...punguzeni Basi.
Ndiyo habari ya Dunia kwasasa hii mkuu, vumilia tu na ukizingatia kitu kuitwa janga la Dunia, sasa ukiambiwa kitu flani ni janga maana yake ni kukitangazia vita kitu hicho, mengine yote yanawekwa pending kukabili janga!
 
"Tanzania has the third largest population at risk of malaria in Africa: over 90% of population live in areas where there is malaria. Each year, 10 to 12 million people contract malaria in Tanzania and 80,000 die from the disease, most of them of them children."

Pambaneni na matatizo yenu kenge nyie
 
Kuna nchi fulani hapa duniani, eneo lake fulani lenye wakazi wengi lilikuwa karibu sana na sehemu ambayo ilikuwa na mlima wenye Volcano hai. Sehemu hiyo ilikuwa na mandhari nzuri sana, na wakazi wake wengi walikuwa watu wenye uwezo. Wakatembelea Wataalam wa mambo ya volcano sehemu hiyo. Wakatoa tahadhari, kwamba baada ya muda fulani volcano italipuka vibaya sana. Ilikuwa ni baada ya kupita muda mrefu kidogo. Lakini wakashauri watu wahame maeneo hayo. Wataalamu wakaondoka. Maisha yakaendelea kama kawaida.
Muda ukapita, kukaanza kuonekana kama mvukemvuke hivi. Mmm! wenye uelewa wakaanza kuhama.
Hali ya mvuke ikaendelea kama miaka mitatu hivi, aaah! watu wakazoea hali, maisha yakaendelea.
Ee bwana eee!! Siku ya siku, muda wa usiku, volcano ililipuka, sehemu yote ile ilifukiwa, hakupona mtu.
This is a true story, ukitafiti utaijua sehemu husika.
 
Back
Top Bottom